MWANAMKE AINGIZWA CHUPA SEHEMU ZA SIRI NA KUSHAMBULIWA KWA NYAYA ZA UMEME

0 comments

Mkazi wa Kitangiri jijini Mwanza, Biera Edwin (22) amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure akipatiwa matibabu baada ya kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili wake kwa tuhuma za kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mume wa mtu.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola hakupatikana kuzungumzia tukio hilo, lakini Biera mwenyewe alisema kabla ya kufanyiwa kitendo hicho mama ambaye ni jirani yao alimtuma mtoto wake amwite nyumbani kwao, alipokwenda mama huyo alianza kumshambulia.
Alisema alimshambulia akishirikiana na marafiki zake na kumjeruhi vibaya kwa nyaya za umeme, kumwingizia chupa kwenye sehemu zake za siri na baadaye kuchoma nguo zake.
Binti huyu kwa sasa amelazwa katika wadi ya majeruhi kwenye Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure akipatiwa matibabu na alisema baada ya kufanyiwa ukatili huo pia waliteketeza nguo zake kwa moto.
Kama da wa polisi mkoa wa mwanza,Valentino mlowola

Naye dada wa majeruhi, Nice Cosmas anaeleza kuwa akiwa nyumbani kwao, mama huyo wa jirani alituma watoto wake ambao walieleza kuwa wakamchukue mtu wao.
Alisema walipokwenda hapo jirani alimkuta ndugu yake akiwa hana nguo huku akiwa amejeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake.
Alisema walilazimika kurudi nyumbani kumchukulia nguo za kumvisha na kisha kutoa taarifa kwa mamlaka husika kabla ya kumpeleka hospitali kwa matibabu.
Baadhi ya viongozi wa mtaa wa Kitangiri A walisikitishwa na kitendo hicho na kuomba vyombo vya sheria kuwachukulia hatua kali wahusika.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Kitangiri A, Issa Salum alisema wanataka haki itendeke kwani kitendo hicho ni nusu ya mauaji.
Naye Mjumbe wa Serikali za Mitaa, Mariam Yusuf alisema mama huyo wa jirani alipaswa kutoa taarifa kwa mabalozi ama kwa wazazi wa binti huyo kama alikuwa na uhakika na madai yake kabla ya kuchukua ukatili dhidi ya binti huyo.


Read More »

NEW ALART: CCM KUANZA FAGIO LA VIONGOZI WIKI IJAYO

0 comments

Chama cha Mapinduzi (CCM) wiki ijayo kitaanza rasmi vikao vyake kwa ngazi ya Taifa vitakavyo chunguza maadili ya viongozi ikiwa ni maandalizi ya kuwapata wagombea wanaokubalika na wananchi katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alitoa taarifa hiyo jana katika mkutano maalumu wa kuwashukuru Watanzania kwa kukichagua chama hicho katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Desemba 14, mwaka jana. Alisema chama chake kinajipanga kuwa na viongozi wasio wamangimeza na wenye moyo wa kuwatumikia wananchi.
Katibu huyo Mkuu aliwashukuru Watanzania kwa kukipa ushindi chama chake na kubainisha kuwa kitaifa, CCM imeshinda kwa asilimia 81.
Hata hivyo, alisema katika maeneo ambayo imeshindwa kama Wilaya ya Pangani, itafanyika tathmini na watajipanga kuhakikisha Uchaguzi Mkuu ujao wanapa ushindi wa kishindo.Alisema watahakikisha wanashinda katika maeneo yote waliyofanya vibaya.

Read More »

Alichosema Ney Wa Mitego Kuhusu Nikki Mbishi Kuacha Muziki

0 comments
ney
Kupitia exclusive interview na Power Jams, Ney wa Mitego amezungumzia hatua ya Nikki Mbishi ya kuacha muziki nakusema “Ukiona kitu hakikulipi ni bora uachane nacho, mtu anaweza kuangalia kitu na kujua hakimfai na bora afanye mambo mengine
Ney aliendelea kusema ” Sijui kwanini amechelewa, nimefurahi kuona maamuzi mazuri kijana mwenzangu aliyofanya, amejitambua na kuamua kuangalia vitu vingine, niko tayari kumshauri kama bado hajapata cha kufanya” .

Read More »

MAHAKAMA YAIANDIKIA WIZARA KUREJESHA MALI ZA MELI YA MAGUFULI

0 comments
Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli.

Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imeiandikia barua Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kwa ajili ya kurejesha mali ikiwamo meli ya Tawariq 1 na  zaidi ya Sh. bilioni mbili za tani 296.3 za samaki kwa raia wawili wa China.
Watu hao ni Hsu Tai na Zhao Hanquing walikamatwa wakivua samaki katika Ukanda wa Kiuchumi wa Bahari ya Tanzania bila kibali.

Kwa mujibu wa barua hiyo iliyosainiwa na msajili wa Mahakama hiyo ya Desemba 17, 2014, imeitaka Serikali kurejea ahadi, kupitia hati ya kiapo iliyotolewa na Godfrey Nanyaro, Dk. Charles Nyamlundana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.

Kwa mujibu wa barua ya msajili huyo, kiapo kinasema endapo washtakiwa hawatakutwa na hatia mahakamani Serikali italipa gharama za samaki waliokutwa nao wa tani 296.3 za Sh. 2,074,249,000 ndani ya siku 30 tangu kuachiwa na mahakama.

Chanzo cha NIPASHE kinaeleza kwamba mbali na barua hiyo, Mahakama Kuu, imeambatanisha nakala ya amri ya kuuza samaki hao uliotolewa Desemba 11, mwaka 2009 na Jaji Radhia Sheikh, hukumu ya kuwaachia huru ya Mahakama ya Rufani na Hati ya Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) ya kuwafutia mashitaka Agosti 14, mwaka 2014.

Septemba Mosi, mwaka huu, upande wa utetezi uliwasilisha barua ya kudai vielelezo hivyo, mbele ya Msajili wa mahakama hiyo.

Katika barua hiyo utetezi wanaomba kwamba mahakama iwarejeshee vielelezo vilivyotolewa katika Mahakama Kuu katika kesi namba 38 ya mwaka 2009 mbele ya Jaji Radhia Sheikh.

Barua hiyo ilivitaja vielelezo hivyo kuwa ni, meli ya uvuvi Tawariq 1 pamoja na Sh. 2, 074,249,000 za tani 296.3 za samaki walizokutwa nazo raia hao ambavyo vilitolewa Oktoba Mosi, 2009 mbele ya Jaji Sheikh.

Awali, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, iliamuru serikali ya Tanzania kulipa meli ya uvuvi pamoja na samaki waliokamatwa miaka mitano iliyopita vyote vikiwa na thamani ya Dola miliobi 3.2  baada ya kuwaachia washtakiwa wawili raia wa China, waliokuwa wanakabiliwa na kesi hiyo.

Wakili wa utetezi Kapteni Ibrahim Bendera, alisema baada ya mahakama kutoa amri hiyo, meli iliyokamatwa na wateja wake ilikuwa na thamani ya Dola milioni 2.5 na samaki waliokutwa nao washtakiwa hao walikuwa na thamani ya Dola 720,000.

Agosti 22, mwaka huu Hakimu Mkazi Mkuu, Mfawidhi, Isaya Arufani alisoma uamuzi wa kuwaachia huru wachina hao pamoja na mambo mengine mahakama yake iliamuru serikali kulipa mali hizo pamoja na hati zao za kusafiria.

Read More »

HII NDIYO AJALI ILIYOTOKEA KIKATITI JIJINI ARUSHA JANA

0 comments

Mwili wa mwanamke anayedaiwa kuwa mke wa mmiliki wa hoteli na klabu ya AQ baada ya ajali.

Basi la Mrindoko Trans baada ya ajali hiyo.

Gari dogo lililogongana na basi.

Mwanamke aliyepoteza maisha katika ajali hiyo enzi za uhai wake.

AJALI mbaya iliyolihusisha basi la Mrindoko Trans na gari dogo lililokuwa linaendeshwa na mwanamke anayedaiwa kuwa mke wa mmiliki wa Hoteli na Klabu ya AQ iliyopo jirani na stendi ya mabasi jijini Arusha ilitokea jana jioni maeneo ya Kikatiti mkoani Arusha.
Katika ajali hiyo, mwanamke huyo alifariki dunia papo hapo.

Read More »

EWURA YASHUSHA BEI YA MAFUTA NI KUANZIA KESHO JANUARI 7, 2015‏

0 comments
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati, Maji na Mafuta (Ewura), Felix Ngamlagosi (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo, kuhusu mwenendo wa bei za mafuta nchini na katika soko la Dunia. Kulia ni Mkurugenzi wa Petroli, Godwin Samwel.

Mkurugenzi wa Petroli, Godwin Samwel (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
 Ofisa Mawasiliano wa Ewura, Titus Kaguo (kushoto), akizungumza katika mkutano huo.
 Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.
Dotto Mwaibale
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati, Maji na Mafuta (Ewura), imepunguza bei za mafuta kote nchini kuanzia leo kutokana na kudorora kwa uchumi wa bara la ulaya.
 
Hayo yalibainishwa  na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati, Maji na Mafuta (Ewura), Felix Ngamlagosi wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo mchana, kuhusu mwenendo wa bei za mafuta nchini na katika soko la Dunia.
Alisema kuanzia leo bei ya mafuta ya petroli kwa lita moja itauzwa sh.1955 na hiyo inatokana na kushuka kwa jumla ya asilimia 16 sawa na pungufu kwa jumla ya sh.311 kwa lita.
Alisema bei ya petroli katika soko la dunia imeshuka kwa jumla ya aasilimia 25 kuanzia Julai hadi Novemba 2014, sawa na pungufu kwa jumla ya dila 249 kwa tani.
Ngamlagosi alisema mafuta ya dizeli kwa lita moja yatauzwa sh.1846 na kuwa bei hiyo imeshuka kwa asilimia 13 sawa na pungufu kwa jumla ya sh.244 kwa lita na kuwa dizeli kwa soko la dunia imeshuka kwa jumla ya asilimia 28 kuanzia Julai hadi Novemba 2014 sawa na pungufu kwa jumla ya dola 189 kwa tani na kuwa mafuta ya taa yatauzwa sh. sh.1833 kwa lita.
 
Alisema katika kipindi cha robo ya mwisho wa mwaka kuanzia mwezi Septemba hadi Desemba 2014, bei za mafuta ghafi zimekuwa zikishuka kwa kasi ikilinganishwa na kipindi cha hapo nyuma ambapo zimeshuka toka dola 100 kwa pipa hadi kufikia wastani wa dola 60 kwa pipa moja ambayo ni sawa na  karibu asilimia 40.
 
Alisema viwango hivyo vya bei iliyopungua ni katika soko la Dar es Salaam na mikoa mingine bei zao zimepangwa kutokana na kuwepo kwa gharama za usafirishaji.
 
Ngamlagosi alitoa mwito kwa wanunuaji wa mafuta hayo kuhakikisha wanapatiwa lisiti baada ya kununua kwani itasaidia kuwabaini wafanyabiashara wasio waaminifu ambao wataendelea kuuza kwa bei ya zamani.
 
"Natioa mwito wa kuwaomba wanunuaji wa mafuta kuhakikisha wanapewa lisiti kwani itatusaidia kuwabaini wale wanauza kwa bei ya juu, na pia itamsaidia mnunuzi iwapo atauziwa mafuta yaliyochini ya kiwango na ukusanyaji wa kodi ya serikali" alisema Ngamlagosi.
 
Naye Mkurugenzi wa Petroli, Edwin Samwel alisema Ewura imejipanga vizuri kuhakikishha hakuna ujanja ujanja utakaojitokeza wa kudai mafuta yamekwisha au yaliyopo yatauzwa kwa bei yaliyonunuliwa.
 
Alisema mfanyabiashara yeyote atakayekiuka utaratibu huo atachukuliwa sheria pamoja na kufungiwa biashara yake ingawa alisema hali hiyo haitajitokeza.

Read More »

POLISI DAR WAZIMA VURUGU KWA MABOMU YA MACHOZI

0 comments



Polisi jijini Dar es Salaam wamelazimika kufyatua risasi hewani na kupiga mabomu ya machozi kufuatia kuibuka kwa vurugu katika hoteli ya Land Mark ambapo shughuli ya uapishaji wa wenyeviti wa Serikali za Mitaa ulikuwa ukifanyika.
Vurugu hizo, zimeibuliwa na kambi ya upinzani ambayo ilikuwa ikilalamikia kuwa Mwenyekiti mmoja wa Chama tawala CCM aliyeapishwa hakuwa ameshinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, uliofanyika mwaka jana.



Read More »

WAKUBWA TU Picha,Mwanamitindo aliyetoa mbavu mbili ili awe na umbo namba nane.

0 comments

Mwanamitindo na stripper maarufu kutoka Miami ‘Estrelle’ amefanya maamuzi ya mugumu ili kupata muonekano aupendao. Model huyu wa video na matangazo amekubali kutolewa mbavu zake mbili ili apate umbo namba 8.

Mwana mitindo huyu alikwenda Miami kwenye hospitali maarufu inayofanya zoezi hilo ambalo limetajwa kuwa ni hatai sana na kupona kwa mgonjwa inaweza kuchukua mpaka miezi 6 kupona.
nomaa 2

nomaa 1

nomaa 3

nomaa 4
Baada ya zoezi kufanyika alikuwa hivi

Read More »

Polici Wasema “Panya Road” 36 watiwa mbaroni Dar

0 comments
polici
Msemaji wa jeshi la polisi SSP Advera Bulimba

Jeshi la polisi nchini linawashikilia vijana 36 wa kundi maarufu Panya Road wanaodaiwa kufanya vurugu na kupora mali za watu na kusababisha taharuki katika jiji la Dar es salaam huku baadhi ya wananchi wakitoa maoni tofauti kuhusiana na tukio hilo.
Akitoa ufafanuzi wa taharuki hiyo msemaji wa jeshi la polisi SSP ADVERA BULIMBA ambaye mbali na kuwatoa hofu wananchi kuwa hali hiyo haitajitokeza tena amesema jeshi hilo limejipanga vizuri kukabiliana na vikundi vyovyote vinavyotaka kuvuruga amani ya nchi.
Pia amesema kwamba endapo polisi wasingewadhibiti vijana hao mapema tangu wakiwa makaburini baada ya kumzika mwenzao aliyeuawa na wananchi baada ya kuiba hali ingekuwa mbaya zadi.
Kufuatia tukio hilo baadhi ya wananchi wa maeneo ya Magomeni ambako vurugu zilianzia wameelezea namna zilivyoanza hadi kusababisha watu kuanza kukimbia hovyo na wengine kuacha maduka yao wazi na taarifa kusambaa maeneo mengine.
Katika maeneo ya Mwananyamala na Ubungo baadhi ya waliozungumzia sakata hilo wameitaka serikali kuangalia makundi ya vijana na ikiwezekana wapatiwe elimu ya ujasiriamali bure ili waweze kuendesha maisha.
Wananchi wengine wameshauri vijana wasiokuwa na kazi mitaani wapelekwe jeshini wakafundishwe stadi za kazi pamoja na uzalendo ili kuepuka vitendo hivyo.
Taharuki hiyo ilitokea usiku wa tarehe 2 Januari, 2014 chanzo kikiwa ni kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la MOHAMED AYUB kuuawa na wananchi tarehe mosi mwaka huu katika maeneo ya Tandale kwa Mtogole kwa tuhuma za wizi ambapo tarehe 2 maziko yalifanyika na taarifa zilizolifikia jeshi la polisi zilidai kuwa baada ya maziko vijana wenzake walijipanga kufanya fujo ili kulipiza kisasi.

Read More »

David Moyes Azungumzia Ushindi dhidi Ya Barcelona Na Jina Alilopewa Baada.

0 comments
moyes
David Moyes ambaye kwa sasa ni kocha wa klabu ya Real Sociedad amesema “Kushinda dhidi ya Barcelona ni jambo ambalo aliwaza kwa muda mrefu bila kujua atalifanikisha vipi na hatakama itawezekana
Kwenye mechi yake ya kwanza dhidi ya Barcelona, Moyes ambaye alikuwa manager wa Manchester United alifanikiwa kushinda kwa bao moja bila.
Moyes alisema “Ushindi huu umemkumbusha wakati alivyokuwa manager wa Everton, wakati anashinda dhidi ya timu kubwa kama Arsenal, Liverpool na Man United ” yMoes alifukuzwa man utd baada ya miezi kumi kwenye nafasi ya Sir Alex Ferguson.
Mtangazaji maarufu wa soka kutoka Span amembatiza David Moyes jina la ‘Braveheart‘.

Read More »

Mwanasheria Mkuu Mpya wa Serikali Mhe.George Masaju amewaomba Watanzania wajenge imani na serikali yao

0 comments
sheria
Mwanasheria Mkuu Mpya wa Serikali Mhe. George Masaju amewaomba Watanzania wajenge imani na serikali yao huku akiahidi kushughulikia kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.
Mheshimiwa Masaju amesema hayo leo muda mfupi baada ya kuapishwa na Rais Tanzania Jakaya Kikwete kushika wadhifa huo uliokuwa ukishikiliwa na Jaji Frederick Werema ambaye alijiuzulu kutokana na kashfa ya ufisadi wa Escrow.
Kwa mujibu wa Masaju, maeneo ambayo atayaangalia ni pamoja na suala na kilio cha muda mrefu cha wanachi na wabunge la kutaka uwazi katika mikataba mbalimbali ambayo serikali imekuwa akiisaini kwa niaba ya wananchi.

Read More »

KWA NINI BEI YA MAFUTA KWA WALAJI HAISHUKI KWA KASI? SOMA HAPA

0 comments

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe.
 
Kuanzia Mwezi Julai mwaka 2014 mpaka Desemba, bei ya mafuta ghafi imekuwa ikishuka kutoka $110 kwa pipa mpaka $56 kwa pipa. Mporomoko huu wa bei wa zaidi ya 40% haujaleta unafuu kwa mtumiaji wa kawaida wa mafuta ikiwemo wenye daladala na kupelekea nauli za usafiri wa umma kupungua.
Leo bado bei ya mafuta kwenye vituo vya mafuta ni tshs 2029 kwa Petroli na 1909 kwa dizeli, bei ambayo ni karibia ile ile kwa miezi michache iliyopita.
EWURA, inasemekana, wamesema kuwa bei za hapa nchini hushuka baada ya miezi 2 kwa sababu waagizaji huagiza kwa ujumla mafuta mengi zaidi na hivyo kutofaidika na punguzo la bei.
Hata hivyo bei zimeanza kushuka toka mwezi Julai na hatujashuhudia unafuu wowote kwa wananchi. Ingekuwa bei ya mafuta imepanda tungeona bei zimepanda mara moja na sababu za kununua ' bulky' huwa hazitolewi.
Ni kweli kwamba Tanzania hununua mafuta yaliyosafishwa na hivyo bei inayoshuka sio hiyo. Lakini hao wasafishaji hununua mafuta ghafi yenye bei ndogo hivi sasa kwa hiyo ni dhahiri lazima bei za pampu zipungue.
Vile vile ni kweli kwamba thamani ya shilingi ya Tanzania imeporomoka hivyo wananchi hawawezi kuona unafuu wa bei ya mafuta kwa sababu hununuliwa kwa fedha za kigeni na kuuzwa kwa Sarafu yetu. Hata hivyo kasi ya kushuka kwa bei ya mafuta ni 40% wakati shilingi imeshuka kwa chini ya 10%.
Katika hali ya kawaida na kwa kutumia mfumo wa kukokotoa bei wa EWURA, angalau bei ya mafuta ingeshuka kwa kati ya 15% and 25%.
Ni dhahiri mamlaka za nchi na hasa EWURA wanapaswa kueleza kwa umma ni Kwanini bei za mafuta hazishuki kulingana na bei ya bidhaa hiyo katika soko la Dunia.
Wananchi wana haki ya kujua na kama hakuna Maelezo basi bei hizo zishuke na wananchi wafaidike na punguzo hilo.
Zitto Kabwe, Mb


Read More »

Soma Hapa Mwigizaji Wastara Azungumzia Mahusiano Yake Na Bondi.

0 comments
WASTARANABONDI2
Kwenye friday nite live ya eatv, mwigizaji Wastara amezungumzia mahusiano yake na mwigizaji maarufu wa filamu Tanzania “Bondi” nakusema  “Nikiwa karibu na mwanaume yeyote sasa watu huzusha maneno ila mimi na Bondi tunafanya kazi pamoja tu, ni manager wangu na husimamia kazi zangu, siwezi kufanya kila kitu mwenyewe
Wastara yuko mbioni kuanza kufanya filamu mpya na kuanzia Januari 5 2014, atakuwa kambini.

Read More »

JOKATE: SIPENDI ‘SINI’ ZA KUTOMASWA! SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments
Mwanamitindo ambaye pia ni msanii wa filamu Bongo, Jokate Mwegelo.
Stori: Laurent Samatta
MWANAMITINDO ambaye pia ni msanii wa filamu Bongo, Jokate Mwegelo amesema kuwa hapendi kuigiza sini za mapenzi hasa zile anazotakiwa kushikwashikwa na mwanaume hasa asiyemjua.
Jokate alifunguka hayo wakati paparazi wetu alipotaka kujua namna ambavyo wazazi na mpenzi wake wanavyolipokea suala la yeye kuigiza sini za kushikwashikwa na wanaume tofauti katika filamu ndipo alipofunguka kuwa suala hilo limekuwa likipigwa vita na wazazi wake lakini analazimika kufanya kwa sababu ndiyo kazi aliyoichagua.
Jokate Mwegelo akipozi.
“Wazazi wangu wanachukia sana jambo hili na huwa wanasema bora niache filamu, hata mimi mwenyewe huwa sipendi ila huwa navumilia kwa kuwa ni kazi, sina jinsi,” alisema Jokate.

Read More »

Avril,Collabo Na Ommy Dimpoz Inakuja Soon.

0 comments

avril 3
Nikimuona ndio single ya mwisho kutoka kwa Avril iliyotoka 2014 na kufanya vizuri kwenye radio na tv nje na ndani ya Kenya. Kupitia instagram yake Avril ametufahamisha kuwa kazi mpya aliyofanya na Ommy Dimpoz inakuja Soon.
avril 1 avril 2

Read More »

NDOA YA LULU YABUMA:ADAI ANAETAKA KUMUOA AWE NA SIFA HIZI...SOMA SIRI HIYO HAPA IKO HAPA

0 comments

Mwigizaji wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’. 

BAADA ya kuwa na malengo ya kuolewa mwaka 2014, mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameibuka na kusema imeshindikana lakini hajilaumu wala hamlaumu mtu yeyote kwa kutotimiza suala hilo kwani anaamini Mungu ndiye anayewezesha kila kitu.
Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Lulu alisema mwaka 2014 alikuwa na malengo mengi likiwemo suala la ndoa lakini kwa kuwa Mungu ndiye muweza, atapanga upya suala hilo na anaamini litakuja kutimia.
“Ndoa ni mipango ya Mungu, huwezi kulazimisha hata siku moja, sisi wanadamu huwa tuna mipango yetu lakini ili ifanikiwe lazima kuwe na baraka za Mungu,” alisema Lulu.

Akizidi kupiga stori na paparazi wetu, Lulu alisema kwa mwaka huu na mwakani hawezi kuweka malengo ya ndoa kwani bado kuna mambo yake hajayaweka sawa hivyo suala la kuolewa ataliweka hadharani baada ya miaka miwili ijayo.
‘Lulu’ akipozi.

“Sina mpango hata kidogo kwa mwaka huu wala mwakani labda baada ya hii miaka kupita ndiyo ninaweza kupanga tena suala la ndoa,” alisema Lulu.

Alipotakiwa kumtaja mpenzi aliyenaye kwa sasa, Lulu aligoma kufunguka lakini akakubali kuanika siri za mwanaume anayetaka kuwa mumewe.
“Kwanza nahitaji mwanaume atakayenielewa kwa kila kitu, pia awe na mapenzi ya kweli na atakayeniangalia kama Lulu na siyo kama Elizabeth pekee. Anapaswa kutambua na kusapoti kazi zangu za sanaa,” alisema Lulu.
Kuhusu mikakati yake ya sanaa mwaka huu, Lulu alisema ana mpango wa kuendelea na masomo huku akiwa pia na ‘project’ kubwa mbili ambazo anatarajia kuzifanya.
“Nina project kubwa mbili mwaka huu, muda utakapofika kila mmoja atazijua maana nitaziweka wazi,” alisema Lulu.

Read More »

BAADA YA NIKKI MBISHI KUTANGAZA KUACHA MUZIKI, HAYA NDIO MANENO YA CHID BENZ

0 comments

.
.
Baada ya msanii wa Hip Hop Nikki Mbishi aka Baba Malcom kutangaza kuwa ameacha kufanya kazi ya muziki sasa Chid Benz amekanusha taarifa hizo na kusema kuwa ameshafanya mazungumzo na msanii huyo  na kumtaka asichukue uamuzi huo mapema kwani hata yeye amepitia katika changamoto hizo.
Chid Benz alichukua nafasi hiyo kuwataarifu mashabiki wa muziki kupitia ukurasa wa facebook na kuandika ‘Nakanusha habari za Nikki mbishi kuacha mziki,nimeongea nae kama kaka na kumgusia mengi,najua amenielewa na nimemwambia asikubali wale wanaomkubali waanze kukubali wengine.mimi nimekumbana na vingi na watu weengi waliaminishwa kama nimeshushwa kimziki,jimefanyiwa mengi ambayo kwa muda ule nsingeweza kuelezea kila mtu nini kinaendelea,so if kikitokea kibaya kinatangazwa mpk kwenye taarifa za habari mbona mziki hauchezwi?ningekua sina nguvu hio nisingesumbua watu kuniweka front page..but bado nipo na nimekomaa.na naishi na naona wanaopewa kipaumbele na najua bado mimi ni mimi.Iron
.

Read More »

ALICHOKIANDIKA TUNDU LISU KABLA YA WALE VIJANA WATATU KUTOKA GEITA KUKAMATWA NA POLISI

0 comments


  

Kuna vijana watatu kutoka mkoani Geita,
wanakuja kwa mguu kuja kuonana na rais
Kikwete ikulu, ili kueleza kero zao kuhusu nchi
yao, je? watakaribishwa ikulu? au wataitwa
wahuni na wavuta bangi? nakumbuka rais
amewahi kuwakaribisha watu wengi ikulu kama
Ray c, Diamond, mzee yusufu, n.k, ambao ni
waimbaji majukwaani, wala sio watetezi wa
wanyonge, wengine ni wala madawa ya kulevya
tu, mh. Rais wanakuja hao vijana watatu kutoka
Geita nakushauri uwapokee, otherwise
utaonekana una upendeleo kwa kuwakaribisha
watu unaowataka wakati ikulu sio mali yako. 

Read More »

BREAKING NEWS: MMILIKI WA VIP ENGINERING RUGEMALIRA AMEFUNGUA KESI MAHAKAMA KUU AKIIDAI SERIKALI BILION SH. 398

0 comments


Mmiliki wa VIP Enginering, aliyekuwa anamiliki hisa IPTL Ndugu Rugemalira amefungua kesi mahakama kuu akiidai serikali jumla ya Sh. 398 bilion zilizokuwemo/zinazotakiwa kuwemo katika Escrow Account ya Tegete na zilizolipwa kwa kampuni ya PAP na kuleta mjafala mkubwa bungeni.

Katika madai yake, mwenye hisa hatambui malipo yote yaliyolipwa na serikali kwa kampuni ya PAP kwani kampuni hiyo haikuwa na nyaraka halali kutoka kwa msajili wa makampuni BRELA, Taxe Clearance Certificate kutoka TRA, kuandikishwa Tanzania Investment Center na wala mmliki wake kuwa na vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini kutoka idara ya Uamiaji.

Katika hoja yake mdai anasema kuwa ni jukumu la serikali kuwahakiki wawekezaji wa nje ili kuwalinda wawekezaji wa ndani pindi tu wanapoingia ubia na wawekezaji wa nje.

Ameendelea kudai kuwa, kwa uzembe huo wa serika kwa kutotimiza uhakiki wake wa kigeni ulisabibisha kampuni yake ya VIP Engineering kuingia ubia na Kampuni Feki na kumsababishia hasara ya sh. Bilion 56 kwani alizimika kuvunja ubia wao na kumfungulia mashitaka mbia mwenza PAP baada ya kugundua ubabahishaji wa uhalali wa kampuni hiyo. Hivyo ameitaka tena serikali kulipa gharama zote alizotumia kuendesha kesi sh.36.8 bilion.

Aidha amedai kuwa aliwafahamisha serikali kutolipa malipo yoyote yaliyokuwemo kwenye account ya Escrow na endapo serikal ingeona kuna haja ya kufanya hivyo basi ilipe kwa VIP au IPTL account ambayo yeye alikuwa signatory.

Katika uwasilishaji wake mahakamani hapo anadai kutofahamu au kutambua kulipwa kwa PAP. Hivyo serikali inatakiwa kulipa tena madai yote kwa VIP au IPTL. Amewapa serikali siku 14 tu toka 1 Januari,2015 kuwa wamelipa malipo yote.

Katika madai hayo, ili kuyadhitisha ameambatinisha :
1. Report ya Mkaguzi mkuu wa hesabu za serika inayodhibitisha baadhi ya pesa kulipwa kwa PAP
2. Mkaguzi mkuu kudhibitisha kuwa mlipwaji hajawahi kusajiliwa kama mlipa kodi wala kupewa Taxe clearance certificate.
3. Report ya mdhibi mkuu wa Rushwa kuthibitisha kuwa kampuni iliyolipwa haikusajiliwa BRELLA na wala haikuwa na sifa au uhalali kufanya kazi yoyote ya ugavi dhidi ya Shirika lolote la Uma.
3. Report ya Bunge kama muhimili mwingine wa nchi kupitia kamati yake ya hesabu za serikali na mashirika ya uma kutodhibitisha/kudhibitisha juu uhalali wa PAP, mmiliki wa kampuni ya PAP na utendaji wake wa kazi.
4. Mapendekezo ya kamati ya bunge kwa serikali dhid ya PAP, mali zake na mmiliki wake.
5. Mapendekezo ya bunge kwa serikali yanayodhibitisha kuwa PAP haikuwa halali.
6. Mapendezo ya bunge kwa serikali juu ya watendaji wote walioshilikiana kwa pamoja ya kuilipa kampuni isiyo halali.
7. Baadhi ya magazeti likiwemo gazeti la serikal kudhibitisha mkuu wa nchi kupokea na kuridhia mapendezo hayo.
8. Magazeti pamoja na la serikali kudhibitisha serikali kwa kuwaadhibu watendaji wote waluofanya udhembe wa kulipa kampuni isiyo halali.
9. Mkanda wa video ya Rais wa nchi katika hotuba yake kukili watendaji wake kuilipa kampuni isiyo halali na kawasimamisha kazi kwa uzembe huo.
10. Barua ya Mwanasheria mkuu wa serikali kwa Rais ya kuomba kujiuzuru kwa kufanya uzembe huo wa kulipa kampuni isiyo halali.
11. Barua ya Rais kwa Mwanasheria mkuu kukubali kujiuzuru kwake kwa kutoa ushahuri wa kulipa kampuni isiyo halali.
Kesi hiyo uenda ikaamsha tena hisia za wananchi juu ya malipo ya Escrow account. Ni mtihani mwingine kwa serikali kwani Bunge na wanachi hawako tayari kuona pesa kama hiyo ikilipwa tena.

Read More »

KIONGOZI WA CHADEMA ASIMAMISHWA KAZI..MWINGINE APEWA ONYO KALI

0 comments

Naibu Katibu Mkuu  CHADEMA  Zanzibar,  Salum  Mwalimu akiutubia mkutano wa hazara  mjini  Nansio Wilaya ya  Ukerewe, Mwanza lengo kushukulu wananchi kwa kukipatia ushindi katika uchaguzi wa Serikali  za  mitaa uliopita. Wilaya  hiyo Chadema imepata  viti 47 vya Serikali za vijiji huku ccm  ikipata 27 na CUF viwili.
Ukerewe. Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu amemsimamisha kazi mjumbe wa kamati ya utendaji ya chama hicho Wilaya ya Ukerewe, Wilbrod Machemli kwa kushindwa kutimiza wajibu wake, ikiwa ni pamoja na kutotangaza ujio wa kiongozi huyo.
Rungu hilo pia limemkuta katibu wa Chadema wilaya hiyo, Libelatus Mlebele ambaye amepewa onyo kali.
Akizungumzia hatua hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Nansio jana, Mwalimu ambaye ameanza ziara mkoani hapa juzi kwa lengo la kuwashukuru wananchi baada ya kukichagua chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, alisema hakuridhishwa na maandalizi yaliyofanywa na viongozi hao.
Kutokana na hali hiyo, Mwalimu alimwagiza Mwenyekiti wa wilaya wa chama hicho, Jacobo Munyaga kwa gharama zake amwandalie mkutano mwingine kabla ya mwisho wa mwezi ujao.
Mwalimu pia alitilia shaka matumizi ya fedha yaliyotajwa kutumika kutangaza uwepo wa mkutano wake.
Alisema Chadema hakipo tayari kulinda viongozi wazembe na wasiowajibika na kuwaonya wajumbe wa kamati tendaji hasa katibu ambaye bado yupo katika uangalizi wa miezi sita kwa maelezo kuwa anaweza kuondolewa kazini.
Kabla ya kuchukua uamuzi huo, Mwalimu aliwaita mbele wakazi wanne wa kata za Kakerege, Nansio, Nakatungulu na Kagera ambao walikiri kutosikia matangazo ya ujio wake.
Hatua hiyo aliichukua baada ya kuwasili katika Uwanja wa Mongera wa mjini Nansio saa 9:30 alasiri huku kukiwa na idadi ndogo ya watu ikilinganishwa na ziara zake za nyuma.
Mbali na hilo, pia Mwalimu ametumia mkutano huo kukemea matumizi mabaya ya fedha za serikali yanayofanywa na viongozi waandamizi wakati huduma za kijamii zikizidi kuwa mbaya.
Alisema ziara za mara kwa mara za nje ya nchi zisizo za lazima zinazofanywa na Rais Jakaya Kikwete pamoja na viongozi wengine hazina tija kwa taifa.
Naye mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, Joseph Mkundi akizungumza katika mkutano huo, alisema katika katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wao wamepata mafanikio makubwa.
Alisema mbali na kusimamia vyema matumizi ya fedha za serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, pia halmashauri hiyo imekamilisha mipango ya kununua greda moja la kutengeneza barabara lenye thamani ya Sh400 milioni hivi karibuni chama hiko kimeluwa kikipigania kukishinikiza serikali kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi.
Hata hivyo, alisema mbali ya halmashauri hiyo kupata hati safi ya matumizi ya fedha za umma pia hivi karibuni huko jijini Nairobi Kenya, Halmashauri hiyo ilipata tuzo ya kukidhi vigezo vya sheria ya ununuzi ya umma kati ya wilaya 166 za nchi nzima.


chanzo: gazeti la mwananchi

Read More »

ATANGAZA KUUZA FIGO KWA SH90 MILION SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments

Mkazi wa Morogoro, Andrew Germanis Chimulimuli ametangaza kuingiza sokoni figo yake ambayo amesema anaiuza Sh90 milioni ili kukabiliana na ugumu wa maisha.
Chimulimuli aliyefunga safari kutoka Ifakara, Morogoro hadi jijini Dar es Salaam ili kufanya biashara hiyo alisema ameamua kutoa kiungo chake hicho muhimu kutokana na ugumu wa maisha unaomkabili.
“Nimeamua kujitolea nafsi yangu ili niisaidie familia yangu, kwa sababu mimi si kitu kama sina fedha, ndiyo maana nimejitolea kutoa figo yangu nipate fedha,” alisema Chimulimuli.
Chimulimuli alisema anataka kuiuza figo hiyo kwa gharama ya Sh90 milioni ingawa alikubali kufanya mazungumzo ya kupunguza bei pindi atakapopatikana mteja.
Takwimu za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii zinaeleza kuwa kuna wagonjwa 470,000 nchini ambao figo zao zimeshindwa kufanya kazi kabisa na wanahitaji upandikizaji.
Ingawa uamuzi wa Chimulimuli unaweza kuwa msaada kwa Watanzania wenye mahitaji, lakini kimaadili ya afya na kisheria, jambo hilo linakatazwa kufanywa kiholela hadi pale linapofuata taratibu.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Figo Tanzania, Jaji Frederick Werema aliwahi kuliambia gazeti hili kwamba anashangazwa na hatua za baadhi ya watu kuchukua uamuzi wa kuuza figo kwa ajili ya kujipatia fedha.
“Kutoa figo ni kosa la jinai, lakini siyo hivyo tu, kutoa figo ni lazima ufuate taratibu za kisheria na za kitabibu,” alisema Jaji Werema miezi kadhaa iliyopita.
Biashara ya figo
Aprili mwaka jana, gazeti hili lilifanya uchunguzi na kubaini kuwa wapo Watanzania wanaouza figo zao kiholela kwa ajili ya kujipatia fedha.
Gazeti hili liliwasiliana na vijana kadhaa ambao kwa nyakati tofauti walikubali kuwa wanauza figo zao na baadhi wakieleza kuwa tayari walishauza kwa gharama za kati ya Sh50 milioni hadi Sh80 milioni.


Chimulimuli alisema kutokana na ugumu wa maisha, kipato chake kimekuwa kigumu sana na hakiwezi kukidhi mahitaji ya familia.
“Mtu akikuona kwa nje anaweza kukuona kama upo sawa na una maisha mazuri lakini ukweli ni kuwa nina maisha magumu sana,” alisema. Kuhusu hatima yake kiafya, alisema yeye ni msafiri na hawezi kuishi milele na hivyo bora auze figo yake iwe msaada kwa wengine wenye mahitaji.
“Ni bora nifanye kitu cha halali kinachoigharimu afya yangu mwenyewe badala ya kuiba au kufanya uhalifu mwingine,” alisema Chimulimuli.
Uchangiaji wa figo
Daktari bingwa wa figo katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Linda Ezekiel alisema uchangiaji wa figo ni mchakato mrefu na si suala la fedha tu.
Dk Ezekiel alisema mchakato wa kuchangia figo ni mrefu kwani mchangiaji hutakiwa kuwa na kundi la damu linalofanana na mgonjwa.
Alisema vipimo vya afya hufanyika ambapo maradhi yanayoweza kuambukiza kama homa ya ini, magonjwa ya zinaa na Virusi vya Ukimwi, navyo huangaliwa kwa umakini mkubwa.
“Ni lazima tuhakikishe mtu ameridhia kabisa kufanya hivyo na katika hali hiyo ni lazima tumfanyie mtu ushauri wa kisaikolojia na afahamu hatua za utoaji huo sambamba na madhara anayoweza kuyapata,” alisema.
Kuhusu changamoto ya maradhi hayo Dk Ezekiel alisema kusafisha figo ‘dialysis’ ni gharama kubwa ambapo kwa tiba moja mgonjwa hutakiwa kulipa Sh300,000 na tiba hiyo hufanywa angalau mara tatu kwa wiki.
Hata hivyo Dk Ezekiel alisema kwa anayechangia figo na kubaki na moja hawezi kupata madhara kiafya kwani figo moja ina uwezo mkubwa wa kufanya kazi zake.

Read More »

SAKATA LA ESCROW: KAFULILA AJIPANGA KUPELEKA HOJA BINAFSI KUMNG'OA PINDA SOMA HAPA

0 comments

SASA kuna kila dalili kuwa mwangwi wa kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow iliyotikisa mkutano wa 16 na 17 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, utaendelea kusikika kwa namna ya kuishinikiza Serikali kuwajibika zaidi.
 
Dalili hizi zimeonyeshwa waziwazi na baadhi ya wabunge hususani waliokuwa vinara wa kupambana na kashfa hiyo ambao hawajaridhishwa na hatua zilizochukuliwa na Rais Jakaya Kikwete dhidi ya watendaji wa Serikali na viongozi wa kisiasa walioguswa na ripoti ya uchunguzi wa kashfa hiyo.
 
Mmoja wa wabunge walio katika mkakati huo ambao kimsingi unalenga kumng’oa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ni David Kafulila wa Kigoma Kusini.
 
Kafulila katika mahojiano yake na waandishi wa habari alisema hatua zilizochukuliwa na Rais Kikwete kushughulikia maazimio nane ya Bunge haziridhishi na kuongeza kuwa kabla ya kuketi kwa mkutano wa 18 wa Bunge anapaswa kuwa amemfukuza kazi Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
 
Alisema Waziri Muhongo ni muhusika muhimu katika kashfa hiyo, kwa sababu alidiriki kusimama bungeni na kulidanganya taifa kuwa fedha zilizokuwa zimehifadhiwa katika Akaunti ya Tegeta Escrow hazikuwa za umma hadi uchunguzi wa vyombo vya dola ulipothibitisha pasipo shaka kuwa ni za umma.
 
“Hatufanyi haya kwa lengo la kumkomoa mtu, hapana kabisa. Sisi tuna dhamira ya dhati ya kutetea maslahi ya taifa kwa hiyo hatuko tayari kumuona Rais akiendelea kumuacha kiporo Waziri Muhongo.
 
“Rais anaonekana kusuasua kuchukua uamuzi dhidi ya Waziri Muhongo, sasa kama itatokea akashindwa kutengua uteuzi wake hadi Bunge lijalo tutawasilisha hoja binafsi ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu tukiwa na kusudio la kumng’oa kwenye wadhifa wake, hiyo ndiyo njia pekee ya kumwondoa Waziri Muhongo,” alisema Kafulila.
 
Alipoulizwa iwapo mkakati huo wa kumng’oa Waziri Mkuu Pinda unaungwa mkono pia na wabunge wa CCM, alisema hawezi kuzungumzia msimamo wa wanasiasa wengine hata hivyo, ujasiri waliouonyesha baadhi ya wabunge wa chama hicho wakati wa mjadala uliopitisha maazimio ya Bunge unaondoa shaka ya kupata uungwaji mkono wa kutosha.
 
Mbali na Kafulila, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge wa Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe, alipoulizwa msimamo wake kuhusu jambo hilo, akiandika kwa maandishi kupitia barua pepe alisema anaamini Serikali itatekeleza maazimio yote ya Bunge.
 
Ingawa tayari Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue amekwishamsimamisha kazi Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, kupisha uchunguzi dhidi yake kwa kashfa ya Escrow, bado yapo mashinikizo yanayotaka hatua zaidi zichukuliwa kwa mujibu wa maazimio nane ya Bunge.
 
Mbali na Katibu Mkuu Sefue, Jaji Mkuu Othaman Chande bado yuko kimya kuhusu majaji wa Mahakama Kuu walioguswa katika kashfa hiyo.
 
Awali viongozi wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kwa nyakati tofauti walikaririwa na vyombo vya habari wakitoa matamshi yenye mwelekeo wa kulishinikiza Bunge kuiwajibisha Serikali iwapo Rais Kikwete hatatekeleza maazimio yote nane ya Bunge.
 
Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba, ndiye aliyekaririwa kwanza akieleza kuwa endapo Rais Kikwete atashindwa kumwajibisha Prof. Muhongo, wabunge walio ndani ya Ukawa watawasilisha hoja na kushawishi wengine kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu sambamba na kuitisha maandamano nchi nzima.


Wakati shinikizo hili likizidi kushika kasi, Rais Kikwete katika hotuba yake ya kufunga mwaka aliendelea kusisitiza msimamo wake wa kumuweka kiporo Prof. Muhongo kwa maelezo kuwa uchunguzi dhidi yake haujakamilika.

Read More »