Mke afumaniwa, amgeuzia kibao mme wake Polisi… Unajua kilichomfanya amsaliti?

Black-Couple-in-Bed-PFJamaa mmoja alisababisha kizaazaa baada ya kuvamia chumbani ambako mtu na mkewe walikuwa wamelala.
Fununu zinasema jamaa huyo baada ya tukio hilo alimhoji mkewe kwamba huyo aliyeingia bila hodi chumbani kwao wakiwa wamelala ni nani?
Baada ya jamaa huyo, Calvin Murapata kutoridhishwa na majibu ya mke wake Nomagugu Ncube alimpiga na kumchania nguo, ambapo mwanamke huyo alifungua mashtaka kituo cha Polisi, Zimbabwe.
Mwanamke huyo aliwahi kushinda taji la mitindo katika nchi hiyo, amekiri kuwa na uhusiano na jamaa huyo aliyevamia chumbani humo kutokana na mume wake kuwa busy.
Ncube amefungua mashtaka kudai fidia ya nguo alizochaniwa.

0 comments:

List kamili ya Walioshinda Tuzo za TASWA 2013/2014 iko hapa, yupo aliyechukua Jumla ya Tuzo tatu

gold-star-award-375x250Siku ya jana December 12 kulikuwa na Sherehe za Utoaji wa Tuzo za Wanamichezo Bora Tanzania mwaka 2013/2014, zilizotolewa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) ambazo zilifanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, ambapo Mgeni Rasmi katika Sherehe hizo alikuwa Rais Wa Zanzibar, Dr. Ali Mohamed Shein
Tuzo kubwa ya kwanza iliyotolewa usiku wa jana ni Tuzo ya Heshima ambayo ilitolewa kwa Hayati Sheikh Abeid Aman Karume na kupokelewa na Mama Fatma Karume.
Sheridah Boniface alivunja Rekodi kwenye sherehe hizo baada ya kutoka na jumla ya Tuzo tatu, Tuzo ya Jumla ya Mwanamichezo Bora 2013/ 2014, tuzo ya Mwanamichezo Bora Chipukizi na Tuzo ya Mchezaji Bora wa Soka Wanawake.
Wachezaji wa Azam, Erasto Nyoni na Kipre Cheche baada ya kupokea tuzo zao.
Wachezaji wa Azam, Erasto Nyoni na Kipre Cheche baada ya kupokea tuzo zao.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Gofu Wanawake imechukuliwa na Madina Iddy.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Gofu imechukuliwa na Nuru Mollel.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Gofu Wanawake imechukuliwa na Madina Iddy.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Gofu ya Kulipwa imechukuliwa na Hassan Kadio.
Tuzo ya Mchezaji Bora Mpira wa Kikapu Wanaume imechukuliwa na Lusajo Samweli.
Tuzo ya Mchezaji Bora Mpira wa Kikapu wanawake imechukuliwa na Sajda Ahmed Lyaimaga.
Tuzo ya Mchezaji Bora Mpira wa Wavu Wanaume imechukuliwa na Kelvin Peter Severino.
Tuzo ya Mchezaji Bora Mpira wa Wavu Wanawake imechukuliwa na Teddy Abwao.
Tuzo ya Mchezaji Bora Mpira wa Magongo Wanaume imechukuliwa na Yohana Wilson.
Tuzo ya Mchezaji Bora Mpira wa Magongo Wanawake imechukuliwa na Kidawa Seremala.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Soka Wanaume imechukuliwa na Erasto Nyoni.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Tenisi Walemavu imechukuliwa na Novatus Emmanuel Temba kwa upande wa Wanaume.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Tenisi Walemavu imechukuliwa na Rehema Selemani Saidi kwa upande wa Wanawake.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Olimpiki Maalum imechukuliwa na Blandina Blasi kwa upande wa Wanawake.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Olimpiki Maalum imechukuliwa na Raphael Kalukula kwa upande wa Wanaume.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Nje anayechezea Tanzania imechukuliwa na Kipre Cheche.
Tuzo ya Mchezaji Bora Mtanzania anayechezea nje imechukuliwa na Mbwana Samatta.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mpira wa Mikono Wanaume imechukuliwa na Hemed Saleh.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mpira wa Mikono Wanawake imechukuliwa na Veronica Mapunda.
Tuzo ya Mwendeshaji Bora wa Baiskeli imechukuliwa na Richard Laizer kwa upande wa wanaume.
Tuzo ya Mwendeshaji Bora wa Baiskeli imechukuliwa na Sophia Adson kwa upande wa wanawake.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ngumi za Ridhaa imechukuliwa na Bondia Suleiman Kidunda.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa ngumi za Kulipwa imechukuliwa na Bondia Francis Cheka.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Tenisi Wanaume imechukuliwa na Omary Sulle.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Tenisi Wanawake imechukuliwa na Rehema Athumani.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Kike mchezo wa Judo imechukuliwa na Grace Alfonce Mhanga.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Kiume mchezo wa Judo imechukuliwa na Geofrey Edward Mtawa.
Tuzo ya Mwanariadha Bora wa Kike imechukuliwa na Zakia Mrisho.
Tuzo ya Mwanariadha Bora wa Kiume imechukuliwa na Alfonce Felix.
Tuzo ya Muogeleaji Bora wa Kike imechukuliwa na Catherine Maswa.

0 comments:

Matokeo ya Simba vs Yanga – picha na idadi ya watu waliozimia uwanjani vipo hapa

Screen Shot 2014-12-13 at 7.09.29 PMTimu ya Simba imeibuka na ushindi baada ya kuichapa timu ya Yanga 2-0 huku timu ya Yanga wakiambulia kuondoka na maumivu ya kushindwa kufurukuta kwa bao hata moja.
Wafungaji wa magoli kutoka timu ya Simba ni Awadh Juma na Elias Maguri ambapo mabao yote yamefungwa katika kipindi cha kwanza.
Kwa mara ya pili tena timu ya SIMBA wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa Nani Mtani Jembe baada ya kutwaa ubingwa huo mwaka jana walipoichapa Yanga bao 3 -1.
Kwa upande wa zawadi Simba wamefanikiwa kutwaa milioni 92 huku Yanga wakiondoka milioni 7.
 Wachezaji wa timu ya Simba wakishangilia bao la pili lililofungwa na Elias Maguli katika dakika ya 40 ya kipindi cha kwanza. Mabao yote ya Simba yamefungwa katika kipindi cha kwanza huku bao la kwanza likifungwa na Awadh Juma katika dakika ya 30.
 Mashabiki wa Simba wakishangilia moja ya mabao yaliyofungwa na timu yao.
 Andreu Coutihno, akimiliki mpira katikati ya mabeki wa Simba…
Mchezaji mpya wa Yanga, kutoka nchini Liberia, Kpah Sherman. akisomba kijiji cha mabeki wa Simba…. Hadi mpira unaisha jumla ya mashabiki wasiopungua wanne wa Yanga walikuwa wameshazimia uwanjani. 
Mashabiki wa Simba waliojaza kwenye dimba la uwanja wa taifa – PICHA ZOTE KWA NIABA YA SUFIAN MAFOTO
                                     Umati wa wana jangwani leo taifa

0 comments: