KWA NINI BEI YA MAFUTA KWA WALAJI HAISHUKI KWA KASI? SOMA HAPA


Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe.
 
Kuanzia Mwezi Julai mwaka 2014 mpaka Desemba, bei ya mafuta ghafi imekuwa ikishuka kutoka $110 kwa pipa mpaka $56 kwa pipa. Mporomoko huu wa bei wa zaidi ya 40% haujaleta unafuu kwa mtumiaji wa kawaida wa mafuta ikiwemo wenye daladala na kupelekea nauli za usafiri wa umma kupungua.
Leo bado bei ya mafuta kwenye vituo vya mafuta ni tshs 2029 kwa Petroli na 1909 kwa dizeli, bei ambayo ni karibia ile ile kwa miezi michache iliyopita.
EWURA, inasemekana, wamesema kuwa bei za hapa nchini hushuka baada ya miezi 2 kwa sababu waagizaji huagiza kwa ujumla mafuta mengi zaidi na hivyo kutofaidika na punguzo la bei.
Hata hivyo bei zimeanza kushuka toka mwezi Julai na hatujashuhudia unafuu wowote kwa wananchi. Ingekuwa bei ya mafuta imepanda tungeona bei zimepanda mara moja na sababu za kununua ' bulky' huwa hazitolewi.
Ni kweli kwamba Tanzania hununua mafuta yaliyosafishwa na hivyo bei inayoshuka sio hiyo. Lakini hao wasafishaji hununua mafuta ghafi yenye bei ndogo hivi sasa kwa hiyo ni dhahiri lazima bei za pampu zipungue.
Vile vile ni kweli kwamba thamani ya shilingi ya Tanzania imeporomoka hivyo wananchi hawawezi kuona unafuu wa bei ya mafuta kwa sababu hununuliwa kwa fedha za kigeni na kuuzwa kwa Sarafu yetu. Hata hivyo kasi ya kushuka kwa bei ya mafuta ni 40% wakati shilingi imeshuka kwa chini ya 10%.
Katika hali ya kawaida na kwa kutumia mfumo wa kukokotoa bei wa EWURA, angalau bei ya mafuta ingeshuka kwa kati ya 15% and 25%.
Ni dhahiri mamlaka za nchi na hasa EWURA wanapaswa kueleza kwa umma ni Kwanini bei za mafuta hazishuki kulingana na bei ya bidhaa hiyo katika soko la Dunia.
Wananchi wana haki ya kujua na kama hakuna Maelezo basi bei hizo zishuke na wananchi wafaidike na punguzo hilo.
Zitto Kabwe, Mb


0 comments:

Soma Hapa Mwigizaji Wastara Azungumzia Mahusiano Yake Na Bondi.

WASTARANABONDI2
Kwenye friday nite live ya eatv, mwigizaji Wastara amezungumzia mahusiano yake na mwigizaji maarufu wa filamu Tanzania “Bondi” nakusema  “Nikiwa karibu na mwanaume yeyote sasa watu huzusha maneno ila mimi na Bondi tunafanya kazi pamoja tu, ni manager wangu na husimamia kazi zangu, siwezi kufanya kila kitu mwenyewe
Wastara yuko mbioni kuanza kufanya filamu mpya na kuanzia Januari 5 2014, atakuwa kambini.

0 comments:

JOKATE: SIPENDI ‘SINI’ ZA KUTOMASWA! SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

Mwanamitindo ambaye pia ni msanii wa filamu Bongo, Jokate Mwegelo.
Stori: Laurent Samatta
MWANAMITINDO ambaye pia ni msanii wa filamu Bongo, Jokate Mwegelo amesema kuwa hapendi kuigiza sini za mapenzi hasa zile anazotakiwa kushikwashikwa na mwanaume hasa asiyemjua.
Jokate alifunguka hayo wakati paparazi wetu alipotaka kujua namna ambavyo wazazi na mpenzi wake wanavyolipokea suala la yeye kuigiza sini za kushikwashikwa na wanaume tofauti katika filamu ndipo alipofunguka kuwa suala hilo limekuwa likipigwa vita na wazazi wake lakini analazimika kufanya kwa sababu ndiyo kazi aliyoichagua.
Jokate Mwegelo akipozi.
“Wazazi wangu wanachukia sana jambo hili na huwa wanasema bora niache filamu, hata mimi mwenyewe huwa sipendi ila huwa navumilia kwa kuwa ni kazi, sina jinsi,” alisema Jokate.

0 comments:

Avril,Collabo Na Ommy Dimpoz Inakuja Soon.


avril 3
Nikimuona ndio single ya mwisho kutoka kwa Avril iliyotoka 2014 na kufanya vizuri kwenye radio na tv nje na ndani ya Kenya. Kupitia instagram yake Avril ametufahamisha kuwa kazi mpya aliyofanya na Ommy Dimpoz inakuja Soon.
avril 1 avril 2

0 comments: