SIASA: Aliyetemwa ukuu wa wilaya ya Igunga ageukia ubunge

Aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Igunga, Elibariki Kingu. 
Siku moja baada ya uteuzi wake kutenguliwa na Rais Jakaya Kikwete, aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Igunga, Elibariki Kingu amesema sasa anageukia ubunge katika Jimbo la Singida Magharibi.
Kingu alisema siku nyingi alikuwa na shauku ya kugombea ubunge katika jimbo hilo, kwamba kuondolewa katika wadhifa huo kutampa nafasi ya kujipanga na kuhakikisha anashinda jimbo hilo linaloongozwa na Mohamed Hamisi Missanga (CCM).
“Unajua kwa muda sasa akili yangu ilijikita zaidi katika ubunge ili niweze kuwasaidia wananchi kwa ukaribu zaidi. Wananchi wa Jimbo la Singida Magharibi wamekaa muda mrefu bila kupata mtu wa kutatua matatizo yanayowakabili,” alisema.    
Alifafanua kuwa Februari 28, mwaka huu atafanya mkutano mkubwa wa hadhara katika jimbo hilo, ataitumia siku hiyo kutangaza rasmi nia yake ya kugombea ubunge.
“Nitakachokifanya sasa ni kuwa karibu zaidi na wananchi na kuhakikisha matatizo yanayowakabili ninayajua kiundani ili niweze kuyatatua kwa urahisi,” alisema.
Aliongeza, “Namshukuru Rais Kikwete kwani aliniamini na kazi aliyonipa niliifanya kwa uaminifu na uzalendo wa hali ya juu, kufanikiwa kuleta mabadiliko katika sekta ya kilimo, afya, mifugo, uvuvi na maendeleo kwa vijana,” alisema Kingu (pichani).
 “Rais ameamua nipumzike na ninamshukuru kwa uzalendo wake mkubwa naamini bado ana imani kubwa  na mimi.”
Akitoa ushauri wa wakuu wapya wa wilaya alisema, “Wanatakiwa kuhakikisha wanamsaidia kazi Rais Kikwete na kutekeleza ilani.”
Wakati Kingu akieleza hayo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen ambaye ameteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Musoma.
Alisema:  “Sina maneno mengi kwa sasa nitasema kauli tatu; Asante kwa pongezi yako, namshukuru Mwenyezi Mungu, namshukuru sana Rais Kikwete kwa kuniteuwa kushika wadhifa huu.”
Kwa upande wake Martha Umbulla aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, alipotafutwa siku nzima ya jana alisema kuwa yupo katika kikao na kuahidi kuzungumzia uteuzi huo baada ya kumalizika kwa kikao, jambo ambalo hakulitekeleza.

Wilaya ya Kiteto ni moja kati ya wilaya zilizokithiri migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, iliyosababisha watu zaidi ya 10 kuuawa na wengine kujeruhiwa.
Akizungumzia uteuzi huo Naibu Katibu Mkuu wa Chadema- Bara, John Mnyika alisema unadhihirisha kuwa  nchi ina mifumo legelege ya kupima wanaopendekezwa kuteuliwa kabla ya uteuzi.
“Uteuzi huu unapaswa kuibua mjadala wa haja ya kufuta wadhifa wa ukuu wa wilaya. Watanzania wanatakiwa kuikataa Katiba Inayopendekezwa kwa sababu imependekeza vyeo vya wakuu wa wilaya ambavyo vipo kwa ajili ya kufanya hujuma na kuiba kura katika chaguzi,” alisema.
Hata hivyo, mkurugenzi wa masomo ya shahada ya kwanza kutoka Chuo cha Usimamaizi wa Fedha (IFM), Dk Shaban Ngole alisema kuwa mabadiliko yaliyofanywa kwa wakuu wa wilaya yanalenga kukiimarisha chama tawala baada ya tathmini ya matokeo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
“Ndiyo maana unaweza ukaona kuwa wapo baadhi ya watu ambao wanazua maswali katika jamii, mfano, uteuzi wa Paul Makonda hauna kitu kingine zaidi ya kuongeza ushawishi wa chama katika Wilaya ya Kinondoni. Chama kimeona kuwa anaweza kuhimili mikikimikiki ya hapa mjini,” alisema Dk Ngole.
Alifafanua kuwa Makonda anaeleweka kuwa ni kada wa CCM ambaye hajifichi kutokana na utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya chama hicho, hivyo kuteuliwa kwake hakuwezi kuwa na maana nyingine.
Licha ya kukiimarisha chama, Dk Ngole alisema kuwa Serikali ina dhamira ya kuongeza ufanisi katika utendaji wake. Hilo limeisukuma kufanya mabadiliko ya msingi ili kujiongezea nafasi ya ushawishi miongoni mwa wananchi.

0 comments:

MZEE MAJUTO NA WASANII WENZAKE WAMTEMBELEA MAMA ALIYEPOKONYWA MTOTO ALBINO NA KISHA KUUWAWA KIKATILI




0 comments:

KUTEULIWA KWA Makonda NA Zelothe KUWA WAKUU WA WILAYA NI MKAKATI WA CCM kutengeneza mazingira ya kuchakachua kura za maoni

nape
SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kuteua wakuu wa wilaya wapya 27 na wengine 19 kuondolewa, wadau mbalimbali wamejitokeza wakidai huo ni mkakati wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) kutengeneza mazingira ya kuchakachua kura za maoni ili kiweze kushinda kwa urahisi.
Wadau hao pia wamedai katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu, chama hicho kimekuwa na utaratibu wa kuteua viongozi hao waweze kutengeneza mikakati ya ushindi katika maeneo yao.
Hata hivyo, akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, aliwashangaa wapinzani kwa kupinga uteuzi huo huku akisisitiza kuwa lingekuwa jambo la ajabu kama wanasiasa hao wangeupongeza.
“Ningeshangaa kama wanasiasa wangesifia uteuzi huo…kwa sababu ndiyo uwezo wao wa kufikiri uliopoishia, ninaomba Watanzania kuwasamehe bure,” alisema Nape kwa kifupi.
Wakizungumzia uteuzi huo mpya, baadhi ya wanasiasa akiwamo Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, walisema hawaoni umuhimu wa nafasi hizo wakidai uteuzi huo umelenga kuandaa timu ya uchakachuaji wa kura katika uchaguzi mkuu na kura ya maoni ili kupitisha Katiba Inayopendekezwa.
Walidai uteuzi huo ni maandalizi ya CCM kuelekea uchaguzi mkuu kwa sababu nafasi hizo hazina umuhimu kwa taifa na kwamba hatua hiyo inaongeza mzigo wa gharama kwa wananchi.
WASOMI
Baadhi ya wasomi kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini waliuita uteuzi huo kuwa ni wa siasa na umelenga kuhakikisha Katiba mpya inapita.
“Uteuzi huo ni wa siasa zaidi kuhakikisha CCM inashinda kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani,” alisema Profesa Gaudence Mpangala wa Chuo Kikuu cha Ruaha Iringa.
Profesa Mpangala pia alitoa tahadhari kwa mteule wa Kinondoni ambaye pia aliwahi kuwa mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Paul Makonda, akisema kiongozi huyo ameteuliwa kimkakati ili kuhakikisha anasimamia upitishwaji wa Katiba mpya katika eneo lake.
“Uteuzi wa Paul Makonda umekuja kimkakati, lengo ni kuhakikisha Katiba Inayopendekezwa inapita kwenye kura za maoni si vinginevyo.
“Ndiyo maana Rais Kikwete amefanya mabadiliko hayo kwa sababu anajua kuwa kinachofuata ni uchaguzi mkuu, lazima aangalie watu watakaoweza kutetea maslahi ya chama chake,” alisema.
Alisema kutokana na hali hiyo, idadi kubwa ya waliochaguliwa wanafanya kazi kwa kufuata matakwa ya viongozi wao jambo ambalo linaweza kuwasaidia kupata ushindi.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Hajji Semboja, alisema nafasi ya ukuu wa wilaya ni ya siasa zaidi kwa vile haiangalii sifa ya mtu anayeteuliwa kushika nafasi hiyo.
“Hizi nafasi za U-DC na RC ni za wanasiasa zaidi ndiyo maana wanachaguliwa bila kuangalia sifa ya mtu… hali ambayo imesababisha kuwapo malalamiko mengi kutoka kwa wananchi.
“Yaani kila nilipopita nasikia Makonda, Makonda…, nikajiuliza ni mtu wa aina gani? Kumbe wanamtuhumu kwenye tukio la Jaji Joseph Warioba, nikajiuliza kwanini aliteuliwa…ila nikapata jibu kwa sababu nafasi zenyewe zimetoka kisiasa zaidi,” alisema Profesa Semboja.
Alisema ili kupata viongozi bora, Serikali inapaswa kuwapa elimu ya uongozi ili wakichaguliwa waweze kujua wajibu kwa wananchi na jinsi ya kujiheshimu.
WANAHARAKATI
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk. Helen Kijo-Bisimba, alisema hakuna kificho, pangua pangua na uteuzi huo wa ma-DC wapya una sababu maalumu.
Alisema ni wazi wakuu hao wa wilaya wamechaguliwa kwa ajili ya kwenda kushughulikia uchaguzi mkuu ujao utakaofanyia Oktoba, mwaka huu.
Sioni sababu hasa iliyomfanya rais apangue wakuu wa wilaya katika kipindi hiki ambacho tumebakiza miezi minane tufanye Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani,” alisema Dk. Bisimba.
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la SIKIKA, Irene Kiria, alisema hatua hiyo ni gharama ambayo inahitaji fedha wakati katika huduma nyingine za jamii Serikali imekuwa ikisema haina fedha.
“Gharama zinakuja kwa kuwa ma-DC hao watahitaji kuhamishwa kwa wale waliohamishiwa vituo vipya na wale wapya pia wana mahitaji yao zaidi.
“Kupangua wakuu hao ni kupoteza fedha za umma bure wakati kuna sekta zinazohitaji fedha kwa ajili ya mahitaji muhimu.
“Hili suala la wakuu wa wilaya tumeshalizungumza mara nyingi, hata kwenye rasimu ya pili ya Katiba iliyosimamiwa na Jaji Joseph Warioba ilitaka watu hao wasiwepo, lakini tunandelea kuona fedha zinatumika kwa ajili yao bila sababu ya msingi,” alisema.
MNYIKA
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), alisema kuhamishwa vituo kwa wakuu wengi wa wilaya miezi michache kabla ya kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa ni mkakati wa wakuu hao ambao ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwenda kupiga kampeni za ndiyo kwa Katiba haramu.
“Wakuu wote ni wajumbe wa kamati za siasa za CCM, hivyo huu ni mkakati kwenda kupiga kampeni za ndiyo kwa Katiba haramu iliyopitishwa kiharamia katika Bunge Maalumu na baadaye kuhujumu upinzani kuelekea uchaguzi mkuu kuliko ufanisi wa utendaji wa Serikali,” alisema Mnyika.
Akizungumzia uteuzi wa aliyewahi kuwa Kamanda wa Polisi katika mikoa kadhaa, Zelothe Steven, alisema utachochea wakuu wengine wa polisi kuhujumu upinzani.

“Uteuzi wa Zelothe utaendelea kuchochea wakuu wengine wa polisi kuhujumu upinzani katika kipindi cha utumishi wao kwa kujipendekeza kwa rais ambaye pia ni amiri jeshi mkuu ili wakistaafu utumishi wao waendelee kupata fadhila kupitia nafasi kama za ukuu wa wilaya,” alisema Mnyika.

0 comments:

Precision air yafirisika...sasa kuuza ndege zake

Precision_Air_ATR_42-600_(5H-PWH)_at_Toulouse-Blagnac_Airport_(LFBO)
SHIRIKA la Ndege la Precision linatarajia kuuza baadhi ya ndege zake na kubakiza ndege sita kupunguza mzigo wa madeni yanayoikabili Kampuni hiyo kwa sasa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo, Michael Shirima alisema Dar es Salaam jana kuwa hatua hiyo imefikiwa kutokana na uchakavu wa ndege hizo na hali ya uchumi wa kampuni.


“Kampuni iko katika mazungumzo na mwekezaji ili kukamilisha makubaliano ya kununua ndege zenye madeni na kisha kuzikodisha kwa kampuni nyingine… makubaliano haya yanatarajiwa kufikiwa mwishoni mwa robo ya kwanza ya mwaka huu,” alisema Shirima.


Alisema pamoja na kufikia hatua hiyo kampuni haijakata tamaa kwa kuweka jitihada ya kutafuta mtaji mkubwa kupitia kwa wanahisa wa sasa au wawekezaji wasio wanahisa.


Awali akiitoa taarifa katika mkutano mkuu wa mwaka wa Tatu wa wanahisa, Shirima alisema mazingira ya biashara yalikuwa na ushindani huku kukiwa na hofu juu ya usalama duniani kote.


Pia alisema thamani ya fedha za kigeni hususan Dola ya Marekani imeendelea kukua ikilinganisha na shilingi ya Tanzania hivyo kusababisha akiba hafifu ya fedha za kigeni na hasara kwa biashara ambazo matumizi yake mengi yanategemea fedha hizo.

0 comments:

Picha: Huddah Monroe achefua tena, atupia picha akiwa uc*i kitandani! WAKUBWA TU

10982337_501544039986956_8689538412124604069_nHuddah Monroe ameshajikubali kuwa ni ‘good girl gone bad’ na ndio maana haoni tatizo kuweka picha akiwa kitandani kama alivyozaliwa.


Mrembo huyo wa Kenya amepost picha kwenye akaunti yake ya Facebook akiwa kitandani huku akiwa amejifunika na shuka sehemu ndogo tu ya mwili wake kuficha sehemu ny*ti.
Mashabiki wake hawakusita kumchana.

“Dnt you fear God?oh I like your beauty and en everything mash Allah but this idea of being naked subhanallah stop it.You are a good girl hudda you can change if you want,” aliandika Shankaroon A. Mohammed.

“Wajameni u mean ur whoring for real?? Oh my… please stop proving ppl right n be decent now that uv achieved what u wanted… n be quiet, if not for anything else then respect your clientèle. This is wrong,” ameandika Brenskie La’femme.

WAKUBWA TU...BOFYA PICHA HAPA CHINI AKIWA AMEPANUA MAPAJA

0 comments:

Mwanamke Amuua Mwanamke Mwenzake kwa Kummwagia Mafuta ya taa na Kumchoma Moto baada ya Kumfumania na Mumewe


Mkazi wa kijiji cha Ibosa, kata ya Nyakato, Bukoba Vijijini, Amelia Richard (50) anatuhumiwa kumuua mwanamke mwenzake kwa kummwagia mafuta ya taa na kumchoma moto baada ya kumfumania na mumewe.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera,  Henry Mwaibambe  alitaja tukio hilo ni  la Februari 15, mwaka huu saa 3 usiku katika kijiji cha Ibosa kata ya Nyakata Bukoba vijijini.
  Alimtaja aliyeuawa ni  Pelagia Martin (46) aliyeunguzwa mwili mzima. Kamanda alisema mwanamke huyo alicheleweshwa kufikishwa Hospitali ya Mkoa hadi kesho yake; Februari 16 baada ya wanafamilia kuomba wayamalize bila kwenda Polisi.
  Makubaliano ya wanafamilia hao yalitokana na kile kilichoonekana kwamba  Amelia alimfumania Pelagia akiwa na mumewe,  Richard Bulebo (57) ndani ya nyumba yao.
  Kwa mujibu wa Kamanda, Februari 16 walipoona hali ya majeruhi inazidi kuwa mbaya, ndipo walifika katika Kituo cha Polisi mjini Kati wakiomba msaada.
  Polisi walimpeleka majeruhi huyo Hospitali ya Mkoa lakini alifariki kabla ya kupatiwa matibabu. Polisi inamshikilia Amelia na Bulebo kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo.


0 comments:

KIKONGWE ALIYEPIGWA MAWE KWA MADAI YA USHIRIKINA HALI MBAYA

 KIKONGWE Hilda Johnfan Pili (79) aliyepigwa mawe kutokana na imani za kishirikina katika Kijiji cha Kilagano, Peramiho mkoani Ruvuma hivi karibuni, bado hali yake ni mbaya kutokana na majeraha makubwa aliyoyapata.

Kikongwe akiwa hoi baada ya kupigwa mawe kutokana na imani za kishirikina.Kikongwe huyo na Maurus Zenda (46) anayedaiwa kuwa ni mwanaye kiukoo, kwa pamoja walijeruhiwa vibaya baada ya kupigwa na baadhi ya ndugu zake kwa kuhisiwa kuhusika katika upotevu wa mtoto Adamu Mselewa (4).
Kwa mujibu wa mmoja wa wanafamilia wa ukoo huo, hali ya bibi huyo bado ni mbaya na wanajitahidi kwa hali na mali kuokoa maisha yake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma alikolazwa.
“Bado hali ni mbaya, bibi bado analalamika maumivu, tunaendelea na matibabu huku tukisubiri madaktari watatueleza nini kuhusu maendeleo yake, ikishindikana hapa tutamhamisha hospitali, afadhali kidogo Maurus,” alisema mwanafamilia huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake.

Mtoto wa kikongwe huyo.Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Mihayo Msekhela, waliwakamata watuhumiwa 10 kutokana na tukio hilo, ambao ni Ambros Mselewa (24) ambaye ni baba mzazi wa mtoto aliyepotea, Maria Zenda (45), Lameck Zenda (22), Pautas Komba (24), Fredy Mende (24), Gerord Ngonyani (27), Odilo Mwingira (21), Shadrack Ngonyani (22), Hilda Zenda(36) ambao wote ni wakazi wa Kijiji cha Muunganozomba.
Msikhela alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa moja asubuhi baada ya baba mzazi wa mtoto huyo, Ambros Mselewa akiwa pamoja na watu wengine walipoanza kuwashambulia watu hao wakimtaka kijana wao aliyepotea kimauzauza tangu Februari 3, mwaka hu

0 comments:

DIAMOND ATOA SABABU ZA KUSHINDWA KUHUDHURIA MSIBA WA BABA YAKE DULY SYKES

mond

 

0 comments: