Man U yamsajili kipa wa Barcelona

Victor Valdes akisaini kuichezea Man U.

MANCHESTER, England  
KLABU ya Manchester United imethibitisha kumsajili kipa wa zamani wa Barcelona, Victor Valdes kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu.
Valdes mwenye umri wa miaka 32, alikuwa akifanya mazoezi na klabu hiyo tangu Oktoba, mwaka jana baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu akisumbuliwa na maumivu ya goti.
Valdes ameeleza kuwa amefurahishwa na usajili huo na yupo tayari kufanya kazi na kipa chaguo la kwanza la timu hiyo, David de Gea ambaye ni raia mwenzake wa Hispania.

0 comments:

Yanga yamtema Kaseja rasmi, yamdai 400m


Kipa wa Yanga Juma Kaseja.

YANGA imetangaza rasmi kuachana na kipa Juma Kaseja lakini Championi Ijumaa linafahamu ukweli kuwa klabu hiyo imepanga kumfungulia mashitaka ya kumtaka alipe shilingi milioni 400, kutokana na kuvunja mkataba.
Akitangaza kwa waandishi wa habari jana, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Jerry Muro alisema kuwa Kaseja ndiye aliyevunja mkataba na klabu hiyo kutokana na kutoonekana mazoezini kwa zaidi ya saa 48, hivyo kuvunja kipengele katika mkataba wake.
“Yanga inatangaza rasmi kuwa haitakuwa na kipa Juma Kaseja kwa sababu amevunja mkataba na klabu yetu na tunamtakia kila la kheri katika maisha yake mapya  huko aendako,” alisema Muro
Kuhusu madai kuwa Kaseja anaidai Yanga, Muro alifafanua: “Kaseja alisaini mkataba na klabu Novemba 8, 2013, siku hiyohiyo akalipwa shilingi milioni 20, makubaliano ilikuwa alipwe shilingi milioni 40 ndani ya kipindi cha mkataba wake wa miaka miwili na hakukuwa na muda maalum uliopangwa.
“Januari 15, 2014 klabu ikamlipa fedha zake zilizosalia shilingi milioni 20, lakini Novemba 11, 2014, akaleta barua ya malalamiko kadhaa kwetu akidai hapati nafasi ya kucheza jambo ambalo siyo kweli na alilalamika kuhusu masuala ya bima.
“Desemba 15, 2014, Klabu ya Yanga ilimjibu barua hiyo na kumfafanulia kile alichohitaji, lakini yote kwa yote hakuna ambacho anatudai wala tunachomdai.”Baada ya hapo gazeti hili lilipata taarifa za ndani juu ya mpango huo wa Yanga kumshitaki Kaseja kwa kukiuka masharti ya mkataba, lakini alipoulizwa Muro alisema hajui chochote kuhusua suala hilo.

0 comments:

DAH INASIKITISHA SANA : MWANAFUNZI WA DARASA LA TATU ABAKWA NA WATU MPAKA KUFARIKI DUNIA KISHA KUMUWEKA KWENYE SINKI LA KUOGEA-MBEYA



MWANAFUNZI wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Rwanda Nzovwe jijini Mbeya , Elika Mkubwa (8), amefariki dunia baada ya kubakwa na watu wasiojulukana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, alisema baada ya watu hao kufanya unyama huo, waliuweka mwili wa mtoto huyo katika sinki la kuogea kwenye nyumba moja ambayo haijakamilika ujenzi wake. Pamoja na hayo, alisema upelelezi bado unaendelea ili kuwabaini waliohusika na tukio hilo.
Akizungumza eneo la tukio, kiongozi wa Mtaa wa Ilomba, Ezekiel Mwakalandwa, alisema taarifa za mauaji hayo alizipata jana asubuhi kupitia kwa majirani zake.
Akizungumza eneo la tukio na paparazi huru, kiongozi wa Mtaa wa Ilomba, Ezekiel Mwakalandwa, alisema taarifa za mauaji hayo alizipata jana asubuhi kupitia kwa majirani zake.
"Nilipota taarifa hiyo, niliongozana na majirani tukiwa na ndugu wa marehemu na kushuhudia mwili wa mtoto huyo ukiwa umelazwa kwenye sinki la kuogea huku sehemu zake za siri zikiwa zimeharibiwa vibaya"
Mama mlezi wa mtoto huyo, Sala Mwandobo, alisema mtoto huyo alitoweka nyumbani kwake January 7 mwaka huu baada ya kuaga anakwenda kufua nguo za shule eneo la chemchem ya maji lililopo mbali kidogo na nyumbani kwake.

0 comments:

Mume hanifikishi kisawasawa, Akimaliza yeye mimi nabaki bado na hamu INGIA HAPA KUSOMA HABARI KAMILI


Mimi ni msichana wa miaka 27 nimeolewa miaka minne iliyopita na nina watoto wawili wote wa kike. Mwanzoni mwa mahusiano yetu na mume wangu (wakati tukiwa wachumba) na hata kama mwaka mmoja na nusu hivi kwenye ndoa yetu, baba watoto alikuwa ananiweza kweli....yaani nikikutana nae...aaah, allahmdullillah, nilikuwa naiona anga kwa uhalisia kabisa....na akiwa amechoka sana, basi hata mbili nitapata na kweli nilikuwa najisikia nime.....! Na kwa wiki nilikuwa napata kama siku nne hivi, yale mapigo ya sawa sawa.

Sasa kwa kipindi kama cha mwaka mmoja hivi...da, baba watoto kwa kweli ana underperform kabisa....wakati mwingine inapita wiki nzima, sionji na mimi mwanamke huwa nahitaji...nikimwambia anasema nimechoka sana kazini. Kwa heshima niliyo nayo kwa mume wangu, huwa namwambia sawa, lakini moyoni huwa nabaki na maswali mengi kuliko majibu. Huwa nahisi moja kati ya mambno haya:

1. Huenda mume wangu ameanza mambo ya nyumba ndogo, so akitoka kazini huenda anamalizia huko huko then akirudi nyumbani anakuwa hoi

2. Labda umbile langu limemchosha, coz kabla hatujaoana nilikuwa na bambataa ya wastani na kiuno chembamba, lakini now sio utani, nyonga imebaki vile vile lakini makalio yameongezeka mara-dufu, so huwa hafikii pale "Dar es Salaam" kisawasawa 

Haya yoye ni mawazo yangu ambayo ninayo moyoni. Sasa sijajua kama nimuulize au na mimi nianze kupiga show za nje kwani wanaonitongoza nikiwapanga kuanzia Dar, basi watafika hadi Morogoro......tatizo nampenda baba watoto na nimempa muda wa kama miezi 6 hivi, kama hatobadilika, basi nita-confirm namba moja ya hapo juu....So na mimi nitaanzia  kutafuta wa kurusha nae roho.

0 comments:

Viongozi wa Siasa Wamcharukia Rais Kikwete…..Wamtaka Afanye Maamuzi juu ya Waziri wa Nishati na Madini.


Viongozi wa vyama vya siasa nchini wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kutekeleza ahadi yake aliyoahidi wakati wa mkutano na wazee wa Dar es Salaam ya kufanya maamuzi ya kumwajibisha waziri wa nishati na madini ambaye alimweka kiporo na kudai kuwa atatoa maamuzi ndani ya siku mbili lakini hadi leo amekaa kimya.
 
Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF Prof Iibrahim Lipumba amesema suala la viongozi wakiwemo mawaziri kuwajibika halikuanza leo hasa anaposhindwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kuisababishia serikali hasara au kushusha heshima ya taifa hivyo ni vyema uwajibikaji ukawa ni kwa kila mtumishi wa umma bila kubagua ili kuleta tija kwa taifa.
 
slaa
Dk. Slaa
Kwa upande wake mjumbe wa halmashauri kuu taifa ya chama cha mapinduzi CCM Bw Najim Msenga amesema niimani ya chama chake kuwa rais atafanya maamuzi sahihi kwa maslahi ya taifa kama alivyoahidi na kwamba suala hilo haliwezi kuathiri uhai wa CCM kwani bado iko imara baada ya baadhi ya watuhumiwa kuchukuliwa hatua.
 
Akizungumzia suala hilo katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Dk Willbroad Silaa amesema hata hao waliojiuzulu na kuenguliwa uteuzi wao maadam uchunguzi ulifanywa na vyombo sahihi hadi kufikia hatua ya kupelekwa bungeni na kujadiliwa na wao kutoa maazimio watuhumiwa wote hadi sasa walipaswa wawe wamefikishwa mahakamani.
 
Katika mkutano wake na wazee wa Dar es Salaam uliofanyika ukumbi wa Diamond Jublee desemba 22 mwaka jana Rais Kikwete alitengua uteuzi wa aliyekuwa waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mh Anna Tibaijuka na kutangaza kumweka kiporo waziri wa nishati na madini Prof Muhongo

0 comments:

WANNE WAFA AJALINI IRINGA SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

Muonekano wa lori lenye namba za usajili T122 ALW baada ya kugongana na basi la Fanuel Express  yenye namba za usajili T919 DCD katika Kijiji cha Ibetelo eneo la Nyororo, wilayani Mufindi mkoani Iringa.
 
Basi la Fanuel Express  yenye namba za usajili T919 DCD baada ya ajali hiyo.
ZAIDI ya watu 4 wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya basi la abiria kutoka Mbeya kwenda Dodoma kugongana na lori katika Kijiji cha Ibetelo eneo la Nyororo wilayani Mufindi mkoani Iringa.
Kamanda wa Polisi Mkoani Iringa, Ramadhani Mungi amesema kuwa ajali hiyo imetokea saa 4.45 asubuhi na kuhusisha basi mali ya Kampuni ya Fanuel Express  yenye namba za usajili T919 DCD kugongana uso kwa uso na lori lenye namba za usajili T122 ALW mali ya Kampuni ya Transisco lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda nchi jirani.
Amesema watu wawili waliokuwa ndani ya basi wamefariki papo hapo na wote waliokuwa ndani ya lori wanahofiwa kufa, ambapo hadi kufikia  saa 7 mchana, watu wawili ndani ya lori walikuwa wamethibitika kufariki dunia na kufanya waliokufa kuwa wanne.

Zoezi la kuondoa miili iliyokuwa ndani ya lori linaendelea ambapo amesema kuwa huenda idadi hiyo ya waliokufa ikaongezeka.
Akielezea mazingira ya ajali hiyo, Kamanda Mungi amesema kuwa basi hilo lilikuwa likijaribu kulipita basi lililokuwa mbele yake katika eneo ambapo palikuwa na lori lingine lililoharibika, wakati huo huo lori lililohusika katika ajali hiyo lilikuwa likikwepa lori lililoharibika pamoja na basi hilo, ndipo magari hayo yalipogongana uso kwa uso katika jitihada za kukwepana.

Majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika Hospitali ya Mafinga, Iringa.

0 comments:

Picha,Diamond Alivyokutana na Peter wa P Square na Fally Ipupa Nigeria. SOMA HAPA

Unafuatilia habari za burudani Tanzania, basi utakumbuka swali waliloulizwa P Square walivyokuja Tanzania kuhusu kumfahamu Diamond. Jibu lao lilitengeneza drama kwa mashabiki wa Platnumz.
Diamond kwa sasa yupo Nigeria kwaajili ya tuzo za Glo-CAf. Amekutana na mastaa tofauti na miongoni mwao ni Peter wa P Square na Fally Ipupa.
diamond square
diamond pupa 2 diamond pupa 3 diamond pupa 4 diamond pupa 5 diamond pupa 6 diamond pupa

0 comments: