Picha za show ya DIAMOND (@diamondplatnumz) aliyoifanya BUJUMBURA ziko hapa

1

2 
 3 10546587_908259752530229_441171772_n 
 10853148_396132520552360_98340790_n 10864705_405236846303028_78045836_n 
 10865169_594902770609770_1224541353_n 
 10899340_792983947439779_1058578797_n

0 comments:

Nimeamua Kutoka Kimapenzi na Binti wa Kazi ( Hausigeli) , Sina Jinsi… INGIA HAPA


Nina mke na watoto 3 wote tunafanya kazi. Tulipozaa mtoto wa pili wife alianza kupunguza umuhimu wa tendo la ndoa sijua ni kwa kuzoea au kuchoka.

Tumewekana vikao vyetu binafsi ili kila mmoja abainishe ni vichocheo gani vinakosekana ili tuviongeze kuboresha mchezo. Wote siyo walevi na tuko karibu kifamilia. 

  
Ukifuatilia labda mke wangu ana mtu sipewi taarifa zozote mbaya. Sasa tatizo ni kitu gani sijui. Ukimwuliza naye anakwambia mume wangu nivumilie nitajitahidi ila baada ya mwezi anarudi kule kule. 
  
Usipochombeza anaweza kupitiliza hata mwezi bila kukumbushia .

Hali hii imenisumbua kwa muda sana .Ili kuepuka kugombana na kuepuka kwenda nje kupata UKIMWI basi nikaamua nimweleze binti ambaye anatusaidia kazi nyumbani na akaonyesha kunisikitikia kwani mi si mtu wa baa useme ningetafuta huko na pia naogopa UKIMWI. 

  
Binti akasema anaweza kunisaidia lakini kwa masharti kwamba ataendelea kuniheshimu mimi pamoja na wife ili chochote kisishtukiwe.

Kwa mtazamo wangu hata kama mtaniona mjinga ni kwamba huyu binti anatumika kuokoa jahazi la sivyo ningekwenda huko na huko kutafuta viruka njia ambao wangeniweka mahali pabaya zaidi. 

  
Tumeanza mahusiano vizuri na tunaendelea kiasi kwamba hata wife asipokuwa tayari mwezi mzima sipati shida na hii imenisaidia kuepuka ugomvi uliokuwa unatokana na tendo la ndoa kutokuwa zuri. 
  
Je wadau katika hali kama hii ambayo mke anakuwa namna hii kwa ninachokifanya nimekosea au niko sawa??
  
Kama unafikiri nimekosea nipe ushauri kuhusu njia mbadala na jiweke kwenye hali yangu  kabla  hujazungumza chochote.

0 comments:

UPDATES: NDEGE YA AIRASIA QZ8501 ILIYOPOTEA NA WATU 162 SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

 

Kikosi cha wanamaji nchini Indonesia kikisali kabla ya kuanza zoezi la kuitafuta Ndege ya AirAsia QZ8501 katika bandari ya Pangkal Pinang kwenye kisiwa cha Sumatra.

 
 Kikosi cha wanamaji kikiwa kazini kuitafuta ndege iliyopotea.

 
  
Ndugu wa watu waliokuwa kwenye ndege iliyopotea wakifarijiana huku wengine wakilia kwa uchungu.

ZOEZI la kuitafuta Ndege ya AirAsia QZ8501 iliyopotea ikiwa na watu 162 ikitokea Indonesia kwenda Singapore jana limeendelea leo asubuhi.
Taarifa zilizopatikana kutoka eneo la utafutaji ndege hiyo zinadai kwamba mabaki ya AirAsia QZ8501 yameonekana baharini na kuna uwezekano ndege hiyo ipo chini ya bahari.
Saa 11:36 asubuhi, Ndege ya AirAsia QZ8501 iliondoka Indonesia.
Saa 12:12 asubuhi rubani aliomba kuipandisha ndege mpaka futi 38,000 kutokana na hali mbaya ya hewa.
Saa 12:16 asubuhi AirAsia ilikuwa bado inaonekana kwenye rada.
Saa 12:18 asubuhi AirAsia QZ8501 ikapoteza mawasiliano na rada na mpaka sasa bado haijapatikana.


0 comments:

Mashindano ya Miss Tanzania Yasimamishwa kwa Miaka Miwili

taji
Shindano la Miss Tanzania limesimamishwa kwa muda wa misimu miwili ili kutoa fursa kwa waandaaji wa shindano hilo kurekebisha baadhi ya kasoro ambazo zimekuwa zikilalamikiwa mara kwa mara.
 
Akizungumza na Mpekuzi Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa Godfrey Mngereza amesema kuwa serikali kupitia baraza hilo imefikia umamuzi huo kutokana na malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa wadau mbalimbali na wapenzi wa shindano hilo.
 
Amesema imefika wakati sasa waandaji warekebishe masuala kadhaa ili kuondoa malalamiko na manung’uniko miongoni mwa wadau ili kulipa heshima shindano hilo, pia liweze kuheshimika na kila mtu.
 
Mngereza ameongeza kuwa, serikali kupitia wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imelipa dhamana baraza hilo kisheria kushughulikia masuala yote yanahusu sanaa na Utamaduni hivyo baraza hilo lina mamlaka ya kuingilia kati endapo litajiridhisha kuwa kuna masuala hayaendi sawasawa.
 
Kuhusu masuala wanayotakiwa kuyarekebisha, Mngereza amesema kuna mambo mengi hayako sawa katika mchakato mzima kuanzia katika ngazi ya vitongoji, na baraza limekuwa likipata malalamiko karibu kila mwaka lakini kwa mwaka huu malalamiko yamekuwa mengi zaidi.
 
Mngereza amesema “Kama imefikia wakati hadi mshindi wa shindano mwenyewe analazimika kuvua taji lake kwa shinikizo, ina maana kuna tatizo, kwahiyo tumewapa muda ili wakaangalie upya mchakato mzima na wafanye marekebisho” 
 
Kuhusiana na sakata la umri wa aliyeshinda shindano hilo kwa mwaka 2014 Sitti Mtemvu, Mngereza amesema kuwa suala la kuthibitisha umri wa mrembo huyo linafanyiwa kazi na Mamlaka husika ambayo ni RITA, na kwamba BASATA haihusiki nalo kabisa.
taji
 
Amemalizia kwa kusema kuwa mrembo  Lilian Kamazima aliyetwaa taji hilo baada ya kuvuliwa na Sitti Mtemvu ataendelea kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya dunia kwa mwaka 2015 kama ilivyopangwa, lakini hakutakuwa na mashindano mengine kwa kipindi cha miaka miwili ndani ya Tanzania kuanzia ngazi ya vitongoji.

0 comments:

MAUWAJI: KIJANA MMOJA APIGWA RISASI YA SHINGO AKIWA CLUB MAISHA, INGIA HAPA KWA HABARI KAMILI.

 
 
Kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja, leo usiku amepigwa risasi ya shingo na watu wasiojulikana wakati akiingia Club Maisha ilioko Oyster Bay jijini Dar es salaam.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa tano(5) usiku ambapo kijana huyu akiwa na rafiki zake wanne(4) wakiwa ndio wanashuka kwenye gari yao waliokuja nayo, walijikuta wamevamiwa na watu wawili wasiojulikana na yeye kupigwa risasi ya shingo kisha watu hao kutokomea kusikojulikana. 

Shuhuda wa tukio hilo alisema aliwaona watu wawili walioshuka kwenye gari ndogo nyeusi ilifunga breki kwa kasi kwani walionekana walikuwa mwendo kasi sana, kisha kuwavamia watu waliokuwa wanashuka kwenye gari ilikuwa imepaki muda mfupi baada ya kufika eneo hilo. 

shuhuda huyo aliendelea kwa kusema alisikia sauti ndogo ya kitu kilicholia "pyuuu!!!" bila ya kuelewa ni nini na kisha kufuatiwa na kelele nyingi za watu hao waliokuwa wamevamiwa.

Waliotenda tukio hilo walitoweka mara moja eneo la tukio baada ya watu kujaa eneo ambalo kijana huyo alipigwa risasi alikuwa ameanguka chini.

Polisi walifika eneo la tukio na kukuta kijana huyo ameanguka chini na damu nyingi zikiwa zimemtoka sehemu za shingoni na kifuani huku akiwa amewekewa nguo shingoni ili damu isiendelee kutoka ambapo ilisemekana ilikuwa ikitoka nyingi sana, walimpakia kwenye gari yao kumuwahisha katika hospitali ya jirani ya mwananyamala, lakini kijana huyo alifia njiani akikimbizwa kuelekea hospitali
Tukio hili linaonekana nila kulipiza kisasi ingawa taarifa kamili bado hazijajulina, endelea kufatilia blog yetu kujua mwendelezo wa tukio hili la kusikitisha.

0 comments:

aliyekuwa Waziri wa Kilimo zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad AJIUNGA RASMI NA CHAMA CHA WANANCHI (C.U.F) leo

Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, akimpongeza Mhe. Mansour Yussuf Himid baada ya kuamua kujiunga na chama hicho na kumkabidhi rasmi kadi ya CUF katika viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja

Aliyekuwa Mwakilishi wa jimbo la Kiembesamaki Mhe. Mansour Yussuf Himid,amejiunga rasmi na chama cha wananchi CUF.

Mhe. Mansour ambaye amewahi kuitumikia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushika nyadhifa mbali mbali ikiwemo ya Waziri wa Kilimo, amechukua uamuzi huo leo kwenye mkutano wa hadhara wa CUF uliofanyika viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja.
Mwanachama mpya wa CUF Mansour Yussuf Himid akizungumza na wanachama wenzake , baada ya kujiunga na chama hicho katika viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja

Baada ya kukabidhiwa kadi ya CUF na Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad, Mhe. Mansour amesema ameamua kujiunga na CUF baada ya kubaini na kuridhika kuwa chama hicho kimebeba matumaini mapya ya wazanzibari.

Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, akihutubia mkutano wa hadhara wa chama hicho katika viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja

Mhe. Mansour ambaye tayari alishateuliwa na chama hicho kuwa mshauri wa mikakati wa Katibu Mkuu wa CUF, amechukua kadi hiyo akiwa miongoni mwa wanachama wapya 108 waliojiunga na CUF kwenye mkutano huo.

Mapema akizungumza kwenye mkutano huo, Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, amempongeza Mhe. Mansour kwa kuamua kujiunga na chama hicho hadharani, na kukiita kitendo hicho kuwa ni cha kijasiri.

Akizungumzia mafanikio ya chama hicho, Maalim Seif amesema kimepata mafanikio makubwa katika mwaka unaomalizika wa 2014, na kutangaza maazimia mapya ya chama hicho kwa mwaka 2015.

Wanachama wa CUF wakionyesha kuunga mkono uamuzi wa Mansour Yussuf Himid kujiunga rasmi na chama hicho kwenye viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja. 

Ametaja mafanikio yaliyopatikana kuwa ni pamoja na kuendelea kukubalika kwa chama hicho katika pembe zote za Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Kuhusu maazimio ya Chama hicho kwa mwaka 2015, Maalim Seif amesema kimejipanga kuhakikisha kuwa kinashinda kwa asilimia kubwa katika uchaguzi mkuu ujao na kuweza kuongoza serikali ya umoja wa kitaifa.

Hata hivyo amewataka wanachama wasibetweke kutokana na mafanikio yaliyopatikana, bali waongeze nguvu kuhakikisha kuwa malengo ya chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao yanafikiwa.

Ameongeza kuwa CUF pia kimejipanga kuimarisha uchumi na kujenga Zanzibar mpya itakayokuwa ya matumaini kwa Wazanzibari wote.

Katika hatua nyengine, Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amesema katika uchaguzi mkuu ujao hatowazuia vijana kutetea haki yao iwapo watadhulumiwa.

“Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 nilifanya kazi kubwa ya kuwazuia vijana wasifanye vurugu pale hoteli ya Bwawani. Mwanzo niliwatuma wasaidizi wangu waende kuwaondosha lakini hakuna aliyesikia hadi nilipokwenda mwenyewe, tena waliondoka kwa shingo upande kabisa. Kwa hivyo uchaguzi mkuu ujao sina namna yoyote ya kuwazuia vijana kutetea haki yao”, alifafanua Maalim Seif.

Kabla ya mkutano huo Maalim Seif alifanya ziara ya kukagua uhai wa chama hicho katika vijiji vya Michamvi, Bwejuu, Jambiani na Paje ambako aliweka mawe ya msingi kwenye matawi ya chama hicho, pamoja na kupandisha bendera kwenye barza ya DAY OUT ya Paje.

0 comments:

aliyekuwa Waziri wa Kilimo zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad AJIUNGA RASMI NA CHAMA CHA WANANCHI (C.U.F) leo

Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, akimpongeza Mhe. Mansour Yussuf Himid baada ya kuamua kujiunga na chama hicho na kumkabidhi rasmi kadi ya CUF katika viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja

Aliyekuwa Mwakilishi wa jimbo la Kiembesamaki Mhe. Mansour Yussuf Himid,amejiunga rasmi na chama cha wananchi CUF.

Mhe. Mansour ambaye amewahi kuitumikia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushika nyadhifa mbali mbali ikiwemo ya Waziri wa Kilimo, amechukua uamuzi huo leo kwenye mkutano wa hadhara wa CUF uliofanyika viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja.
Mwanachama mpya wa CUF Mansour Yussuf Himid akizungumza na wanachama wenzake , baada ya kujiunga na chama hicho katika viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja

Baada ya kukabidhiwa kadi ya CUF na Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad, Mhe. Mansour amesema ameamua kujiunga na CUF baada ya kubaini na kuridhika kuwa chama hicho kimebeba matumaini mapya ya wazanzibari.

Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, akihutubia mkutano wa hadhara wa chama hicho katika viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja

Mhe. Mansour ambaye tayari alishateuliwa na chama hicho kuwa mshauri wa mikakati wa Katibu Mkuu wa CUF, amechukua kadi hiyo akiwa miongoni mwa wanachama wapya 108 waliojiunga na CUF kwenye mkutano huo.

Mapema akizungumza kwenye mkutano huo, Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, amempongeza Mhe. Mansour kwa kuamua kujiunga na chama hicho hadharani, na kukiita kitendo hicho kuwa ni cha kijasiri.

Akizungumzia mafanikio ya chama hicho, Maalim Seif amesema kimepata mafanikio makubwa katika mwaka unaomalizika wa 2014, na kutangaza maazimia mapya ya chama hicho kwa mwaka 2015.

Wanachama wa CUF wakionyesha kuunga mkono uamuzi wa Mansour Yussuf Himid kujiunga rasmi na chama hicho kwenye viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja. 

Ametaja mafanikio yaliyopatikana kuwa ni pamoja na kuendelea kukubalika kwa chama hicho katika pembe zote za Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Kuhusu maazimio ya Chama hicho kwa mwaka 2015, Maalim Seif amesema kimejipanga kuhakikisha kuwa kinashinda kwa asilimia kubwa katika uchaguzi mkuu ujao na kuweza kuongoza serikali ya umoja wa kitaifa.

Hata hivyo amewataka wanachama wasibetweke kutokana na mafanikio yaliyopatikana, bali waongeze nguvu kuhakikisha kuwa malengo ya chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao yanafikiwa.

Ameongeza kuwa CUF pia kimejipanga kuimarisha uchumi na kujenga Zanzibar mpya itakayokuwa ya matumaini kwa Wazanzibari wote.

Katika hatua nyengine, Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amesema katika uchaguzi mkuu ujao hatowazuia vijana kutetea haki yao iwapo watadhulumiwa.

“Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 nilifanya kazi kubwa ya kuwazuia vijana wasifanye vurugu pale hoteli ya Bwawani. Mwanzo niliwatuma wasaidizi wangu waende kuwaondosha lakini hakuna aliyesikia hadi nilipokwenda mwenyewe, tena waliondoka kwa shingo upande kabisa. Kwa hivyo uchaguzi mkuu ujao sina namna yoyote ya kuwazuia vijana kutetea haki yao”, alifafanua Maalim Seif.

Kabla ya mkutano huo Maalim Seif alifanya ziara ya kukagua uhai wa chama hicho katika vijiji vya Michamvi, Bwejuu, Jambiani na Paje ambako aliweka mawe ya msingi kwenye matawi ya chama hicho, pamoja na kupandisha bendera kwenye barza ya DAY OUT ya Paje.

0 comments:

Nyalandu atangaza rasmi kugombea Urais kupitia CCM 2015 HABARI KAMILI IPO HAPA


WAZIRI wa maliasili na utalii na mbunge wa jimbo la Singida kaskazini(CCM) ,Lazaro Samwel Nyalandu, ambaye ametangaza rasmi kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.


WAZIRI wa maliasili na utalii na mbunge wa jimbo la Singida kaskazini(CCM) ,Lazaro Samwel Nyalandu,ametangaza rasmi nia ya kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.
Nyalandu ametangaza nia hiyo leo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Ilongero Jimbo la Singida kaskazini.
Alisema baada ya kutafakari kwa muda mrefu na kujikagua kwa kina,ameona anao uwezo wa kutosha wa kuweza kupokea kijiti kutoka kwa rais anayemaliza muda wake mwakani kwa mujibu wa katiba.
“Kujikagua huko ni pamoja na kutafakari jinsi alivyoweza kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM katika vipindi vitatu (miaka 15) akiwa mbunge wa jimbo la Singida kaskazini.Katika kipindi hicho cha ubunge,nimeweza kutumia zaidi ya shilingi bilioni mbili katika kufanikisha kuchangia miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali zikiwemo za afya,maji na barabara”,alisema Nyalandu.
Alisema wakati ukifika,Watanzania kutoka sehemu mbalimbali za nchi wakiongozwa na wakazi wengi wa kutoka jimbo la Singida kaskazini,kwenda Dodoma kuchukua fomu za kuwania urais.
“Watanzania waliokwisha onyesha nia ya kuwania urais mwakani,nawaomba sote tuonyeshe kazi tulizozifanya katika kuwahudumia Watanzania,ili waweze kutupima vizuri waweze kujijengea mazingira mazuri ya kuchangua rais atakayewafaa kwa kuwaletea maendeleo endelevu”,alisema.
Nyalandu alisema kuwa anakishukuru Chama Cha Mapinduzi,kwa maandalizi yake mazuri ya kuhakikisha chama kinapata mwanaCCM safi,mwadilifu na mchapa kazi atakayepeperusha bendera ya chama katika kinyang’anyiro cha kuwania urais mwakani.

chanzo: gazeti la mwananchi

0 comments:

PHOTO’S: Hivi ndivyo alivyopokelewa DIAMOND (@diamondplatnumz) na kundi lake Nchini BURUNDI..

1
2 

3 

4 

5

6

7
 1515782_813759588680773_361530474_n
 10843796_1600128320221330_1387340386_n 10848256_1562372814004909_1103692674_n 10864869_1532023193734930_727265778_n 10864970_1592259054322814_1268864582_n
10890552_323662227824937_934916415_n 10891006_431393020343188_1378749524_n

0 comments:

MAJANGA MWISHONI MWA MWAKA 2014: NDEGE YA AIRASIA QZ8501 YAPOTEA IKIWA NA WATU 162

Ndege ya AirAsia, QZ8501iliyopoteza mawasiliano ikiwa na watu 162 ikitokea Indonesia kwenda Singapore.
Ndugu, jamaa na marafiki wa abiria waliokuwa kwenye ndege ya AirAsia QZ8501 wakiwa na majonzi wakati wakisubiri taarifa kuhusu ndugu zao katika Uwanja wa Ndege wa Surabaya, Indonesia.
NDEGE ya AirAsia, QZ8501 iliyokuwa na watu 162 ikitokea Indonesia kwenda Singapore imepoteza mawasiliano leo asubuhi.
Kati ya watu hao 162, abiria walikuwa 155, marubani 2 na wafanyakazi wa ndege hiyo 5. Watu 157 ni raia wa Indonesia, 3 raia wa Korea Kusini, 1 kutoka Malaysia na 1 raia wa Singapore.
Imeelezwa kuwa kabla ya ndege hiyo kupoteza mawasiliano, rubani aliomba kubadili uelekeo wa kawaida kutokana na hali mbaya ya hewa.
Ndege hiyo ilifanyiwa matengenezo kwa mara ya mwisho Novemba 16, 2014 kama ilivyokuwa imepangwa.
Rubani wa ndege hiyo ana uzoefu wa saa 6,100 angani huku msaidizi wake akiwa na uzoefu wa saa 2,275.
Miongoni mwa abiria 155 waliokuwa kwenye ndege hiyo, 138 ni watu wazima, 16 watoto na 1 mama mjamzito.

QZ8501 imetoka Indonesia saa 11: 27 alfajiri na ilitarajiwa kuwasili Singapore saa 2:37 asubuhi.

0 comments:

FULL TIME: TOTTENHAM HOTSPUR 0-0 MANCHESTER UNITED

 

Robin van Persie wa Manchester United akijaribu kufunga bao lililookolewa na kipa Hugo Lloris wa Spurs.

 
Patashika wakati wa mtanange wa leo.
 
Mchezaji wa Tottenham, Nacer Chadi (kulia) akiruka juu kuwania mpira na Antonio Valencia wa Manchester United.
TIMU za Tottenham Hotspur na Manchester United zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu katika mechi yao ya Ligi Kuu England iliyomalizika kwenye Uwanja wa White Hart Lane hivi punde.
VIKOSI VYA LEO
Tottenham: Lloris, Chiriches, Fazio, Vertonghen, Davies, Mason, Stambouli; Chadli, Eriksen, Townsend, Kane
Waliokuwa benchi: Vorm, Dier, Walker, Lamela, Dembele, Paulinho, Soldado

Manchester United: De Gea, Jones, McNair, Evans, Valencia, Carrick, Rooney, Mata, Young, Van Persie, Falcao
Waliokuwa benchi: Lindegaard, Rafael, Smalling, Shaw, Fletcher, A.Pereira, Wilson


0 comments:

BREAKING NEWS: MWISHONI MWA MWAKA 2014: NDEGE YA AIRASIA QZ8501 YAPOTEA IKIWA NA WATU 162 INGIA HAPA KWA HABARI KAMILI








 

NDEGE ya AirAsia, QZ8501 iliyokuwa na watu 162 ikitokea Indonesia kwenda Singapore imepoteza mawasiliano leo asubuhi.
Kati ya watu hao 162, abiria walikuwa 155, marubani 2 na wafanyakazi wa ndege hiyo 5. Watu 157 ni raia wa Indonesia, 3 raia wa Korea Kusini, 1 kutoka Malaysia na 1 raia wa Singapore.
Imeelezwa kuwa kabla ya ndege hiyo kupoteza mawasiliano, rubani aliomba kubadili uelekeo wa kawaida kutokana na hali mbaya ya hewa.
Ndege hiyo ilifanyiwa matengenezo kwa mara ya mwisho Novemba 16, 2014 kama ilivyokuwa imepangwa.
Rubani wa ndege hiyo ana uzoefu wa saa 6,100 angani huku msaidizi wake akiwa na uzoefu wa saa 2,275.
Miongoni mwa abiria 155 waliokuwa kwenye ndege hiyo, 138 ni watu wazima, 16 watoto na 1 mama mjamzito.

QZ8501 imetoka Indonesia saa 11: 27 alfajiri na ilitarajiwa kuwasili Singapore saa 2:37 asubuhi.

0 comments:

Tuzo Walizoshinda @VanessaMdee Na @diamondplatnumz Zilizofanyika Nigeria.

vanessa mdee tuzo
Mtangazaji/Msanii Vanessa Mdee na  Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ wamewakilisha vizuri Tanzania kwa kushinda tuzo zingine kubwa Nigeria za AFRIMA.
Vanessa ameshinda tuzo ya Best Female Artist in East Africa [Msanii bora wa kike Afrika Mashariki ] huku Diamond akishinda Tuzo Ya Best Male Artist in East Africa [ Msanii bora wa kiume Africa Mashariki] . Tuzo ya Diamond ilipokelewa na Peter Msechu ambaye pia alikuwa kwenye kuwania tuzo hizo.
vanessa mdee tuzo 3
peter 2 peter 3
Hongera kwao na Peter Msechu kwa kuwakilisha vizuri.

0 comments: