Watatu wafukiwa na kifusi wakichimba madini wilayani Kahama mkoani Shinyanga





Wachimbaji watatu wa madini ya dhahabu ya Kalole kata ya Lunguya wilayani Kahama mkoani Shinyanga  wamefariki dunia baada ya kufukiwa na udongo wakiwa kwenye shimo la dhahabu wakitafuta dhahabu.

Kwa mujibu wa taarifa ya kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha alisema tukio hilo limetokea Januari 7,2015 saa 12 asubuhi katika machimbo madogo ya dhahabu ya Kalole kata ya Lunguya,tarafa ya Msalala wilayani Kahama.

Aliwataja waliofariki kwa kufukiwa kwenye shimo  hilo la dhahabu kuwa ni  Kulwa Magele(20) mkazi wa Shishani wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Ihalu Maheme(23) mkazi wa Idisa wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu na Lameck Frank(22) mkazi wa Nzega mkoani Tabora.

Kamanda Kamugisha alisema vijana hao ambao ni wachimbaji wadogo wa madini waligundulika wakiwa wamekufa ndani ya shimo la kuchimbia dhahabu na inaelezwa kuwa waliingia kwenye shimo hilo ambalo halitumiki kwa nia ya kuchimba dhahabu ndpo likabomoka na kuwafukia na kusababisha  vifo vyao papo hapo.
Wakati huo huo mwanamke aitwaye Sayi Shitunguru(50) mkazi wa  kijiji cha Buruma kata ya Isaka wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ameuawa kwa kupigwa kitu kizito kichwani na watu wasiofahamika akiwa nyumbani kwake.

Kamanda Kamugisha alisema tukio hilo limetokea Januari 7,2015 saa 1 asubuhi ambapo mwanamke huyo akiwa nyumbani kwake alivamiwa na mtu/watu wasiojulikana kasha kumpiga na kitu kizito kichwani na kusababisha kifo chake papo hapo.

Alisema chanzo cha tukio hilo bado hakijajulikana  na jeshi la polisi linaendelea kufanyan uchunguzi ili kubaini chanzo chake.

Hata hiyvyo alisema tayari wanamshikilia mtu mmoja aitwaye  John Jota(33) mkazi wa Kazungu wilayani Kahama kwa mahojiano zaidi huku akiwataka wananchi kushirikiana na polisi ili kusaidia kukamatwa kwa wahusika wa mauaji hayo.

0 comments:

Kuhusu Ajali aliyopata Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi.

Leo January 10 kupitia mitandao na blogs tofauti zimeenea taarifa na picha za ajali ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi. Taarifa nilizopokea mpaka sasa kuhusu ajali hii ni kwamba mhe Mbilinyi amepata ajali akielekea Dar es salaam kwenye kona kali iliyopo eneo la Kitonga, Iringa akiwa na watu wanne kwenye gari moja.
vyombo vya habari vimesema hakuna mtu aliyepoteza maisha waka kupata majeraha yeyote makubwa. Kamanda wa Polisi wa Iringa, Ramadhani Mungi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo leo.
sugu 1 
 sugu 2 
 sugu 3 
 sugu 4 
 sugu 5 
 sugu 6


0 comments:

Ifahamu klabu pekee inayoweza kumsajili Messi kwa sasa… INGIA HAPA

lionel_messi_barcelona

Huku habari kuhusu uhusiano mbaya wa Lionel Messi na klabu yake ukiendelea kutengeneza headlines kwenye vyombo vya habari barani Ulaya tetesi za kuondoka kwake zimezidi kushika kasi huku kila siku ikiibuka story mpya.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na mtaalamu wa biashara kwenye mchezo wa soka ni klabu mbili pekee ambazo kwa sasa zina uwezo wa kumsajili nyota huyu raia wa Argentina kinyume na ilivyoripotiwa kuwa klabu kadhaa ziko kwenye harakati za kumsajili.
Klabu hizi zimetajwa kuwa Manchester United na Real Madrid kutokana na kuwa na msuli wa kifedha pamoja na sababu nyingine ambazo zinaleta ugumu kwa zile klabu ambazo zinaweza kuwa na fedha lakini zikashindwa kufanya usajili kutokana na kubanwa kwenye sehemu tofauti.
Katika hali ya kawaida klabu kama Manchester City, PSG , Chelsea na Bayern Munich zinaweza kumsajili mchezaji yoyote kwa bei yoyote, lakini hali kwa sasa ni tofauti kwani kanuni za kusimamia matumizi ya fedha kwa vilabu ‘Financial Fair Play’ zinafanya matumizi kwa vilabu yafanywe kwa kuzingatia vitu vingi.
Hapa ndio mahali ambako United na Real zinapata faida endapo zitakuwa na dhamira ya kumsajili Messi.
Ili kumnunua Messi klabu inayomtaka itapaswa kulipa ada ya uhamisho ambayo ni paundi milioni 196 na mshahara wake utalazimika kuwa mkubwa kutokana na hadhi ya mchezaji mwenyewe na kwa mantiki hiyo ni United na Madrid pekee ambazo zinatengeneza aina ya fedha ambayo inaweza kutosha kumnunua Messi pasipo kukiuka sheria za Financial Fair Play.
Klabu ambazo zinatangaza hasara ya zaidi ya paundi milioni 23.5 kwa muda wa miaka mitatu zinaadhibiwa na sheria za FFP na tayari Man City na PSG zimekumbana na rungu hilo jambo ambalo linawaondoa kwenye mbio za kumsajili Messi endapo nyota huyo atawekwa sokoni.
Pamoja na ukweli huu bado haitakuwa rahisi kwa Barcelona kukubali kumuona Messi akiondoka hasa ukizingatia kuwa klabu hiyo ina adhabu ya kutofanya usajili kwa muda wa mwaka mzima hali inayowafanya wasiwe kwenye nafasi ya kumuuza mchezaji yoyote muhimu kwani kufanya hivyo itakuwa sawa na kujidhoofisha huku wakiwa hawana nafasi ya kujiimarisha.

0 comments:

TAZAMA PICHA ALIZOPOSTI MCHUMBA WA NAY MTANDAONI INGIA HAPA




Mchumba wa staa wa Bongo Fleva, Emanuel Elibariki 'Nay wa Mitego' , Siwema Edson 'Mama Curtis' amepost leo picha za mahaba akiwa kitandani na mzazi mwenzie huyo kupitia Account yake ya Instagram.

0 comments: