MTUHUMIWA WA UGAIDI ARUSHA AFARIKI MIKONONI MWA POLISI


Hatimaye Abdulkarimu Thabiti Hasia aliyekuwa akituhumiwa kwa ugaidi, amefariki katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru alipokuwa amelazwa kwa miezi sita akiwa mikononi wa polisi.
 
Taarifa ya kifo cha Hasia aliyekuwa mmoja wa maimamu wa Msikiti wa Geti la Mbao Mbauda, ilitolewa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Arusha wakati kesi ya mtuhumiwa huyo na wenzake saba ilipotajwa.
 
Hasia aliyekuwa ni mshtakiwa wa pili katika kesi ya kushambulia baa maarufu ya Arusha Naighty Park, alikuwa akikabiliwa na makosa 16 ya ugaidi, amefariki bila kufikishwa mahakamani hata siku moja.
 
Ilielezwa mahakamani hapo jana, mbele ya Hakimu Hawa Mguruta kuwa mtuhumiwa huyo alifariki Desemba mosi, akiwa amelazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
 

Hata hivyo, wakati taarifa hiyo ikitolewa, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Augostino Komba alieleza kutokuwa na taarifa hiyo, hivyo mahakama iliagiza kubadilishwa hati ya mashtaka.

Baadhi ya ndugu wa marehemu walieleza kwamba tangu alipokamatwa na kupata kipigo katika mahojiano na polisi, Hisia alikuwa amelazwa hadi kifo chake.
 
Kifo cha mtuhumiwa huyo kimekuja wakati kuna malalamiko ya watuhumiwa wengine kupigwa na kujeruhiwa na polisi katika mahojiano na bado wapo gerezani.
 
Septemba 4 mwaka huu, mtuhumiwa huyo alisomewa mashtaka 16 ya ugaidi akiwa amelazwa hospitalini baada ya kupata fahamu.
 
Kabla ya kusomewa mashtaka hayo, marehemu alikuwa ameshalazwa hospitalini hapo kwa takriban miezi minne na awali ilishindikana kusomewa mashtaka kutokana na kutokuwa na fahamu.
 
Kesi ya watuhumiwa wengine wa ugaidi inatarajiwa kutajwa tena Desemba 19 kutokana na kutokamilika kwa upelelezi na watuhumiwa hao walirejeshwa rumande.

0 comments:

POLISI NA RAIA WATWANGANA BAADA YA KUFUMANIANA

WAKAZI wawili wilayani hapa, wamelazwa katika hospitali ya Wilaya ya Kahama Mkoa wa Shinyanga baada ya kujeruhiwa katika mapigano kati yao na askari Polisi, baada ya kumshika ugoni mmoja wa askari katika hoteli moja maarufu mjini hapa.
Tukio hilo lilitokea juzi usiku baada ya mmoja wa vijana hao, kumkuta askari akijivinjari na mkewe, ndipo alipomshirikisha ndugu yake na kuibuka mapigano makali ya kurushiana makonde yaliyosababisha baadhi yao kujeruhiana vibaya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Justus Kamugisha, alisema tukio hilo limetokea baada ya askari, Sajenti Edward kufumaniwa akiwa na mke wa mmoja wa vijana hao aliyejulikana kwa jina la Paschal Matonange (26).
Kamugisha, alisema baada ya kufumaniwa akiwa na mwanamke huyo chumbani, vijana hao walianza kumshushia kipigo huku wakimpiga picha akiwa uchi, hali iliyosababisha vurugu kwenye hoteli hiyo iliyopo nje kidogo na mji wa Kahama.
Kamanda huyo, alisema baada ya vurugu hizo wasamalia wema walijaa eneo hilo na baadhi yao kupiga simu kituo cha polisi ambako askari walifika kujaribu kutuliza vurugu hizo bila mafanikio.
Alisema katika kutuliza ghasia hizo, yalizuka mapigano makubwa kati ya vijana hao na askari polisi, hali iliyosababisha kujeruhiwa kwa baadhi ya askari na vijana hao ambao wamelazwa katika hospitali ya Halmashauri ya Mji.
Aidha, waliolazwa ni pamoja Marco Matonange (27), na mdogo wake Paschal Matonange ambaye ndie mme wa mwanamke huyo aliyefumaniwa akiwa na askari.
Hata hivyo, Kamugisha alisema jeshi lake litamchukulia hatua za kinidhamu askari aliyefumaniwa na mke wa mtu, ambaye pia yumo kwenye kikosi maalumu cha kufanya uchunguzi wa makosa ya jinai, kwa kuwa kufanya hivyo ni utovu wa nidhamu.
“Kimsingi sisi kama polisi hatuhusiki na masuala ya ugoni na askari kwenda pale kwenye tukio hawakwenda kwa ajili ya kufumania, bali walikwenda kwa ajili ya kutuliza ghasia lakini ilikuwa ni kazi kuwakamata hao vijana, mpaka sasa pamoja na wao kujeruhiwa pia baadhi ya askari wamejeruhiwa,” alisema Kamugisha.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya, alisema suala hilo  kwa kutumia nafasi yake ya uenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, analifanyia kazi kwa mujibu wa taratibu na sheria za nchi.
“Ni kweli tukio hilo ninalo, vyombo vyangu vya usalama vinalifanyia kazi ikiwemo uchunguzi ili kujua hasa chanzo chake kilichosababisha kuwepo kwa mapigano hayo,” alisema Mpesya ingawa mmoja wa majeruhi hao alidai mkuu huyo ndie aliyewakoa wakati wakipata kipigo kituo cha polisi baada ya kupiga simu kwa mkuu wa polisi Wilaya (OCD).
Akizungumzia tukio hilo katika Hospitali ya Mji wa Kahama, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja, aliyefika kuwapa pole majeruhi, alisema jeshi la polisi linatakiwa kufanya kazi kwa misingi ya sheria.
Mgeja, alimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi, (IGP), Ernest Mangu, kuhakikisha anafanya uchambuzi wa askari wake wasiokuwa na nidhamu ambao hutekeleza majukumu yao kwa vitisho, hali inayosababisha wananchi kukosa imani nao.
Mganga mkuu wa Hospitali ya Mji wa Kahama, Deogratius Nyaga, alisema hali za majeruhi hao zinaendelea vizuri.

0 comments:

LILE SAKATA LA MWANAFUNZI ALIYEFANYA MTIHANI MARA MBILI NA KUONYESHWA MAJIBU AFUTIWA MATOKEO‏ YAKE YOOTE RASMI

BABA YAKE AMBAYE NI MRATIBU ELIMU KATA AVULIWA   WADHIFA

MWALIMU MKUU ALIYESHIRIKIANA NAYE APEWA ONYO KALI

BAADA ya Mtandao huu kuibua tuhuma na mwanafunzi Monica Masunga kufanya mtihani wa darasa mara mbili katika shule tofauti mbili zilizo kata moja mwanafunzi huyo sasa amefutiwa matokea ya mtihani wa darasa la saba mwaka huu 2014.

Uchunguzi wa Mtandao huu ulibaini kuwa mwanafunzi Monica Sayi Masunga (15) ambaye baba yake ni Mratibu Elimu kata katika kata ya Kakubilo 
alimaliza darasa la saba mwaka jana katika shule ya msingi Kakubilo ambapo bada ya matokea kutoka hakuwa amefaulu mtihani huo .

Matokeo ya Monica katika mtihani wa mwaka jana yalionesha Somo Kiswahili alipata alama C,Kiingereza D, Maarifa alama C, Hisabati D, na Sayansi alipata alama D hivyo wastani wake kwa masomo yote ukiwa alama D ambao haukumwezesha kufaulu.

Uchunguzi zaidi ulibaini kuwa mwanafunzi huyo aliingizwa kinyemela na kusajiriwa kuwa mtahiniwa wa mtihani wa darasa la saba mwaka huu 2014 akifanya mtihani huo katika shule ya msingi Kawawa ambako alisajiriwa kwa jina la Monika silya Masunga akitofautishwa kidogo na jina la mwaka jana alilofanyia mtihani.

Mwanafunzi huyo alionekana shule ya msingi Kawawa siku ya mtihani ambako muda wote kabla ya mtihani alikuwa nyumbani bila kusoma hali iliyowafanya hata wanafunzi wa shule hiyo kushangaa kuwa na mtahiniwa mwenzaoambaye hawakuwahi kumuona katika shule hiyo ,walimu kwa maelekezo ya Mratibu huyo walionywa kutomtilia shaka.

Ofisi ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Geita baada ya chapisho la habari hii ulilazimika kutuma ujumbe wa maafisaelimu wawili Stephene Mase Afisaelimu taaluma na Heri Bihemo Afisaelimu ya Watu wazima ambao walifika shule ya msingi Kakubilo alikofanyia mtihani mwaka janana kisha shule ya msingi Kawawa alikofanya mtihani mwaka huu.

Walibaini viashiria vya kuwepo udanganyifu na ukiukwaji mkubwa maadili kutokana na kukuta mwanafunzi huyo kuonekana kufanya mtihani mara mbili kinyume kabisa na sheria ya elimu ya mwaka 1978.

Baada ya kufikisha tarifa hiyo Afisaelimu wa wilaya Deus Seif alilazimika kuunda tume kutoka Ofisi ya ukaguzi wa shule kwa ajili ya kwenda kufanya uchunguzi wa kina kisha kutoa majibu ya uchunguzi wa kwa Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya .

Uchunguzi wa tume hiyo ulibaini kuwa mwanafunzi huyo ni kweli alifanya mtihani mara mbili katika shule mbili tofauti kwa maagizo ya Mratibu Elimu Kata Masunga akiwa baba wa mwanafunzi huyo kwa kubadilisha taarifa ili ionekane Monica alianzia darasa la kwanza s/m Kawawa .

Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashauri ya wilaya ya Geita Ally Kidwaka alisema amepokea taarifa ya uchunguzi huo kwa masikitiko makubwa kutokana na jinsi elimu inavyochezewa tena na watu waliopewa dhamana ya kuongeza sekta hiyo muhimu kwa ustawi wa taifa letu.

Alisema tume ilipomhoji mwalimu mkuu aliyekuwa shule ya msingi Kawawa Chobabona Michael ambaye kwa sasa alihamishiwa shule ya msingi Njingami ambaye ndiye alimsajiri mwanafunzi huyo kinyemela ili aweze kufanya tena mtihani mwaka huu alikiri mbele ya tume kufanya udanganyifu huo.

Aidha Mkurugenzi huyo alisema hata mratibu huyo wa elimu naye alikiri mbele ya tume kutoa maelekezo kwa mwalimu mkuu wa shle ya Kawawa kuhakikisha mtoto wake Monica anasajiriwa kufanya mtihani akikiri kukiuka taratibu za kielimu ambako alimwelekeza Afisaelimu wa wilaya kuchukua hatua kali.

Alipofuatwa na Mtandao huu kuelezea jinsi alivyopokea matokea ya uchunguzi huo Afisaelimu Deus Seif alilimwagia sifa Mtandao huu kwa kuifumbua macho wilaya hiyo juu ya hujuma zinazofanywa za kuzalisha wasomi feki na kufanya wasiostahili kufaulu mitihani.

Alisema maamuzi yaliyochukuliwa dhidi ya Mratibu elimu kata huyo ni kwamba amevuliwa wadhifa wake huku mwalimu Chobabona aliyekubali kukiuka sheria ya Elimu amepewa barua ya onyo kali ,akisema pia kuwa mwanafunzi huyo ambaye alikuwa amefaulu matokea yake yamefutwa.

Matokeo ya mwanafunzi Monica ambaye pia alikiri kuoneshwa majibu ya mtihani katika mtihani wa mwaka huu Kiswahili ana alama B, Eglish D,Maarifa C, Hisabati D na Sayansi ana alama C Wastani wake wa jumla ni alama C.

Monica alianza darasa la kwanza katika shule ya msingi Buligi mwaka 2007 kabla ya kuhamia shule ya msingi Kakubilo mwaka 2011 akiwa darasa la tano ambako aliandikishwa kwa namba 4548 ambapo mwak jana alikwa miongoni mwawanafunzi 78 wa shule ya msingi kakubilo waliofanya mtihani akitumia namba ya mtihani PS 2404051/062.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kakubilo Magessa Mashabala alisema Monica alikuwa mwanafunzi wake tokea 2011alipohamia hapo akitokea shule ya msingi Buligi alikoanzia darasa la kwanza ambako kabla ya kupandishwa cheo baba yake alikuwa mwalimu mkuu wa shule hiyo ya Buligi.

Aliposajiriwa kinyemela shule ya msingi Kawawa Monica alipewa namba za usajiri 530 na kuonekana kuwa alianzia hapo darasa la kwanza hadi darasa la saba namba yake ya mtihani mwaka huu ikiwa ni PS 2404064/O83.

Kitabu cha mahudhurio ya kila siku ya wanafunzi cha shule ya msingi Kawawa kilionesha Monica amehudhuria siku zote shuleni bila kukosa hata siku moja huku ikionesha wazi kuwa kilitkitabu kipya cha mahudhurio na kumwingiza Monica kisha kuweka alama ya vema kuonesha hakuwahi ukosa shule hata siku moja.

Mbaya zaidi mwanafunzi huyo kwa maelekezo ya baba yake yake aliaidiwa kufanya mtihani ambap alikiri kupewa majibu ambayo ndiyo yalimsaidia kufaulu mtihani wa mwaka huu.

Alipozungumza na Mtandao huu Monica alikiri kupewa majibu ambapo alisema yeye baada ya kufeli mtihani mwaka jana akijijua uwezo wake kiakili kuwa mdogo alimuomba baba yake kumtafutia cherahani ili mapeleke akijifunze ushonaji.

Alisema baba yake alimwambia asubiri ataenda kufanya tena mtihani na kwamba angesaidiwa japo alisema alimsihi baba yake kuwa yeye hawezi kabisa kuyamudu masomo ya sekondari.

"Ilipofika mwezi wa saba mwaka huu baba aliniambia niende nikipime sare ya shule na nijiandae kufanya mtihani katika shule ya msingi Kawawa ilipobaki siku ya mtihani nilikuta tayari nimeandaliwa dawati langu nikaingia chumba cha mtihani ambapo niliuwa naletewa majibu " alisema Monica .

0 comments:

ZITTO: NINA SHARTI MOJA TU KURUDI CHADEMA

DAR ES SALAAM. HARUFU YA KUISHA KWA MGOGORO BAINA YA ZITTO KABWE NA CHAMA CHAKE CHA CHADEMA INANUKIA, LAKINI MBUNGE HUYO WA KIGOMA KASKAZINI ANATAKA KUWAPO NA MAZUNGUMZO KUBAINI TATIZO ILI ATAKAYEBAINIKA KUWA ALIFANYA MAKOSA AWE TAYARI KUOMBA RADHI HADHARANI.

Zitto alikiri bungeni kuwa amekuwa “akimiss” harakati zilizokuwa zikifanywa na vyama vya upinzani wakati wa Bunge Maalumu la Katiba, harakati zilizozaa Umoja wa Katiba ya Wananchi na kufurahia kuhudhuria kwa mara ya kwanza vikao vya umoja huo.
Zitto, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), alipata fursa ya kuingia vikao vya Ukawa wakati wapinzani walipoungana tena kupambana dhidi ya wizi wa fedha kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow, sakata ambalo liliwekwa bayana na kamati yake baada ya Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila kulifikisha bungeni, lakini hakudokeza lolote kuhusu Chadema.
Hata hivyo, mapema wiki hii, Zitto, ambaye Novemba mwaka jana alivuliwa nyadhifa zote kwenye chama hicho kwa tuhuma za kukihujumu, lakini akafanikiwa kulinda uanachama wake baada ya kufungua kesi mahakamani na kufanikiwa kupata amri ya kuzuia asijadiliwe.
Baada ya kuongoza PAC kuchunguza wa tuhuma za Escrow na kufanikiwa kulishawishi Bunge kufikia maazimio manane ya kuwashughulikia kisheria wahusika kwenye uchotwaji huo wa fedha, kumekuwapo na wito kutoka kwa baadhi ya wafuasi wa Chadema kutaka pande hizo mbili zimalizane.
“Kabla ya jambo lolote kufanyika, ili kukata kiu ya Watanzania wanaotaka kuona tunaondoa tofauti zetu, ni lazima kusema ukweli na kila upande kuwa tayari kuomba radhi hadharani pindi ikibainika ulifanya makosa,” alisema Zitto alipotakiwa kuzungumzia harakati hizo za kumrejesha Chadema.
“Ukweli wangu ndani ya Chadema ni nini? Lakini mimi ninaona sina kosa ndani ya Chadema. Ninachotaka mimi nielezwe ukweli bila chembe ya shaka makosa yangu mimi ni nini,” alisema na kuongeza:
“Nitakuwa tayari kuomba radhi hadharani kama ikibainika nilifanya makosa na kama ikibainika chama kilifanya makosa, nacho kiwe tayari kuomba radhi hadharani na ukweli uwe mbele katika maridhiano.
“Kama hakutakuwa na ukweli itakuwa vigumu kupata mwafaka. Mimi sina tatizo. Nirudie nilivyosema bungeni kuwa nina-miss sana (ninapenda sana kuwamo kwenye) harakati za mageuzi kipindi hiki za kuiondoa CCM madarakani.”
Katika mkutano na waandishi wa habari mara baada ya kuvuliwa nyadhifa zote, Zitto alisema: “Natambua kuwa wapo ambao wangependa kutumia nafasi zao kudhoofisha mapambano ya siasa za demokrasia nchini mwetu. Napenda wanachama wa Chadema na wapenda demokrasia watambue kuwa, mimi bado ni mwanachama mwaminifu wa chama hiki.
“Kinachoendelea ndani ya chama chetu ni mapambano ya kukuza demokrasia. Ni mapambano baina ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina; waumini wa uwajibikaji dhidi ya wabadhirifu; na wapenda siasa safi dhidi ya watukuzao siasa majitaka.”
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ambaye binafsi aliguswa na mzozo huo, hakuwa tayari kuzungumzia kumaliza matatizo baina ya chama na Zitto.
“No comment (sina maoni) kwa hilo. Siwezi kuzungumzia suala hili katika media (vyombo vya habari),” alisema Mbowe
Hoja ya kutaka Zitto arejeshwe Chadema imekuwa ikisambaa katika mitandao ya kijamii na kwa baadhi ya wanasiasa baada ya kuonekana kuwa karibu na viongozi wa chama chake wakati Kamati ya PAC ilipoibua ufisadi wa Sh306 bilioni kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow wiki iliyopita.
Wakati akihitimisha mjadala wa sakata la Escrow, mbali na kueleza bayana kuwa alifurahia kuhudhuria vikao vya Ukawa kwa mara ya kwanza, Zitto alikwenda mbali na kumpongeza “kwa namna ya pekee” Mbowe kwa jinsi walivyoshirikiana katika sakata hilo.
Zitto alisema hilo lilikuwa ni jambo la kitaifa ndiyo maana wabunge wote wa upinzani bila kujali vyama vyao waliungana.
Alisema mara baada ya sakata hilo kumalizika watu mbalimbali wamekuwa wakizungumzia kufanyika kwa maridhiano ili awe sehemu ya Ukawa na kwamba haoni tatizo.
“Katika hili, kipekee namshukuru kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani kwa kuniunga mkono katika sakata hili,” alisema Zitto.
Kuhusu taarifa za kujiunga kwake na chama kipya cha ACT-Tanzania alisema: “Hizo ni taarifa ambazo hazina ukweli wowote.”
Kuhusu kesi aliyofungua mahakamani dhidi ya Chadema, Zitto alisema:
“Nilifungua kesi kwa sababu ya kulinda uanachama wangu, lakini mazungumzo yakifanyika na kujua kosa langu ni nini, nitaifuta kesi hiyo na kuanza upya harakati.”
Zitto.
Kuhusu taarifa za kujiunga kwake na chama kipya cha ACT-Tanzania alisema, “Hizo ni taarifa ambazo hazina ukweli wowote.”

Kuhusu kesi aliyofungua mahakamani dhidi ya Chadema, Zitto alisema: “Nilifungua kesi kwa sababu ya kulinda uanachama wangu, lakini mazungumzo yakifanyika na kujua kosa langu ni nini, nitaifuta kesi hiyo na kuanza harakati.”
MWANANCHI

0 comments:

"NAJISIKIA RAHA KUKAA UCHI NIWAPO NA MPENZI WANGU"....JOKATE ASEMA


Modo ambaye pia anafanya muziki na ujasiriamali, Jokate Mwegelo amefunguka  kuwa, awapo chumbani na mpenzi wake huwa anasikia raha kutovaa chochote.

Akizungumzia maisha yake ya kimapenzi na mwanadada paparazi, Jokate alisema haoni aibu kusema akiwa faragha na mpenzi wake hapendelei kuvaa kitu kwani ni eneo la kujiachia.
 

“Kwa kweli nikiwa chumbani na mpenzi wangu sipendi kuvaa kitu kabisa,” alisema Jokate kwa kifupi.

0 comments:

RAIA WA PAKISTAN AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 60 JELA KWA KOSA LA KUSAFIRISHA TWIGA WANNE HAI KWENDA QATAR.

Moshi/Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Kilimanjaro, jana imemhukumu raia wa Pakistan Ahmed Kamran kifungo cha miaka 60 jela baada ya kumtia hatiani kwa makosa manne ikiwamo kusafirisha twiga wanne hai kwenda Qatar.
Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Simon Kobelo, ambaye pia aliamuru kutaifishwa kwa mali zote za mtuhumiwa huyo zilizopo katika ardhi ya Tanzania.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana baada ya kutolewa hukumu hiyo, Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa alisema kilichofanyika ni kutaka kuonyesha haki imetendeka, huku Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maliasili, Ardhi na Mazingira, James Lembeli akisema kuwa kumsaka mtuhumiwa huyo ni sawa na mchezo wa kuigiza.
Hata hivyo, tayari Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol) juzi limewataka Watanzania kusaidia katika kumsaka Kamrani, huku likitangaza kuanzisha operesheni iliyoipa jina la Infra Terra ikilenga kuwanasa watuhumiwa uharamia zaidi ya 139 katika nchi 36 duniani.
Mchungaji Msigwa alisema kuwa kilichofanyika ni kiini macho kwa kutaka kuonyesha kuwa haki imetendeka. Alisema haiwezekani Ahmed apatikane na kosa pekee yake wakati mchakato wa kusafirisha wanyama unaonyesha watu wengi wakiwamo viongozi walishiriki kutekeleza biashara hiyo.
“Hata kama wangemfunga miaka 200 haisaidii kitu, hapo mahakama imefanya kazi yake lakini Serikali inafanya kiini macho,” alisema Msigwa.
Msigwa ambaye pia ni Mbunge wa Iringa Mjini, alisema kitendo cha mahakama kuthibitisha kuwa mfanyabiashara huyo alikuwa na vibali halali kinaonyesha kuwa kuna baadhi ya watu walishiriki kumtorosha ili wasitiwe nguvuni.
“Isingewezekana ndege iingie nchini bila wakubwa kujua ilikuja kufanya nini?” alihoji.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli alisema kumsaka mtuhumiwa Kamran Ahmed anaona huo ni mchezo kwa sababu mtuhumiwa huyo raia wa Pakistan alishatoroka awali kisha akapatikana, lakini katika hali ya kushangaza akapewa tena dhamana.
Lembeli alisema hatua ya kuruhusu dhamana ya pili kwa mtuhumiwa huyo inatia shaka kuwa kuna jambo lisilo la kawaida lililomwezesha kutoroka kwake.
“Hivi kwa nini walimpa dhamana wakati alishatoroka mara ya kwanza na huyu mwandishi Temba aliyemdhamini sijui alianzia wapi, najua hamfahamu lakini amejiingiza kwenye matatizo ya kujitakia,” alisema Lembeli.
Kuhusu ndege inayodaiwa kutumika kusafirisha wanyama hao, ambapo mahakama imethibitisha kuwa ilikuwa na vibali vyote halali vya kuingia nchini kwa safari ya kidiplomasia, Lembeli alisema Wizara ya Mambo ya Nje ieleze kwa kina jambo hilo lilitokeaje.
“Mimi katika hilo sitaki kuzungumza sana, ila nafikiri kuna haja ya kujiridhisha kuwa kibali hicho cha kidiplomasia ni cha aina gani, kilitolewaje, kisha majibu tutakayopata ndipo tutajua nini kilitokea,” alisema Lembeli.
Alipotafutwa kwa njia ya simu, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na naibu wake, Mahmoud Mgimwa, simu zao ziliita bila kupokelewa.
Hukumu ya kesi hiyo ilitolewa bila mtuhumiwa wa kwanza (Kamran) kuwapo mahakamani baada ya kutoroka tangu Februari mwaka huu wakati kesi yake ikiwa katika hatua za mwanzo za usikilizwaji.
Katika hukumu hiyo, hakimu Kobelo aliwaona washtakiwa wengine wanne, Hawa Mang’unyuka, Martin Kimath na Michael Mrutu kuwa hawana kesi ya kujibu na kuwaachia huru.
Hakimu Kobelo alisema hakuna ubishi kuwa raia huyo wa Pakistan (Kamran), ndiye aliyekuwa wakala katika biashara hiyo na ambaye ndiye aliyewasafirisha wanyama hao kwa kutumia ndege kubwa ya Jeshi la Qatar. Kobelo alisema ndege hiyo ilikuwa na vibali vyote halali vya kuingia nchini kwa safari ya kidiplomasia kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro(KIA).
Hakimu Kobelo alisisitiza kuwa ndege iliyobeba wanyama hao ilikuwa na hadhi ya kidiplomasia na ilifuata taratibu zote na kuruhusiwa na mamlaka za nchi ikiwamo Wizara ya Mambo ya Nje.Uchambuzi wa ushahidi huo unaonyesha raia huyo wa Pakistan, aliruhusiwa na mamlaka za Tanzania kukamata wanyama kwa kutumia leseni za kampuni mbili zinazomilikiwa na Hawa.
Hata hivyo, mshtakiwa huyo hakuwa na kibali cha kusafirisha wanyama hao kwenda nje ya nchi na kwa kuwa alitoroka, mahakama haikuweza kupata uthibitisho wake kama alikuwa na kibali.
Kutokana na uchambuzi huo, mahakama imemtia hatiani raia huyo wa Pakistani kwa makosa manne ambapo kila kosa amehukumiwa kifungo cha miaka 15 jela.

0 comments:

DK. SLAA AIBUA MAPYA IPTL SOMA HAPA HABARI KAMILI

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilibrod Slaa.
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilibrod Slaa, amesema fedha zilizochotwa katika Akaunti ya Tegeta Escrow ni sh bilion 400 badala sh bilioni 306 kama ilivyokaririwa na vyombo vya habari kutoka bungeni.
Hayo aliyabainisha juzi na Katibu Mkuu huyo katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi wa Serikali  za Mitaa uliofanyika katika mtaa wa Mnazi mmoja Manzese, Tip top jijini Dar es Salaam.
Dk. Slaa alisema kutokana na tuhuma hizo, alifuatilia bunge hatua kwa hatua hadi likaisha kwa maridhiano, akiamini wezi wa fedha hizo watachukuliwa hatua lakini cha kushangaza hadi leo hawajachukuliwa hatua nab ado wanaendelea na kazi.
“Fedha alizochukua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka na Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo ni ukweli uliowazi kuwa Rais Jakaya Kikwete anajua na ndio maana mawaziri hao wamekuwa na jeuri.
“Suala la Escrow ni bichi kuliko mnavyofikiria, lugha ya Mwalimu Nyerere aliposema watu wanaokimbilia Ikulu tuwaogope kama ukoma, Ikulu ni mahali patakatifu mahali pa heshima kumbe wakubwa walijua kuna nini? Atoke Kikwete hadharani kama nasema uongo,” alisema.
Alisema hajawahi kuona Waziri dhaifu kama Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwani kama angekuwa makini, angeweza kuzuia wizi huo usitokee.
“Mfumo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni mbovu kuanzia Kikwete mwenyewe na serikali za mitaa hata wabadilishwe viongozi katika chama hicho bado hakutakuwa na mabadiliko ya kimaendeleo nchini,” alisema Dk. Slaa.
Naye Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe alisema kuwa nguvu ya CHADEMA ya kusimamisha wagombea katika mitaa na vitongoji kwa asilimia 98 katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini imewatia hofu CCM.
Mbowe, alisema  baada ya kubaini mbinu chafu za chama hicho, kuwawekea wagombea wa CHADEMA pingamizi huku wengine wakienguliwa kimizengwe ni dalili ya wazi kwamba chama hicho kinahofu ya kushindwa.
“Presha hiyo inawafanya wawaengue wagombea wetu kwa kuwajengea hoja zisizo na msingi mara utasikia jina limekosewa mara sijui jina la chama liko hivi ili mradi tu wakipunguze nguvu chama chetu.
“Nawaomba wakazi wa Vijibweni ikifika Desemba 14 siku ambayo itakuwa ya uchaguzi, mjitokeze kwa wingi kama mlivyojitokeza leo ili mkawapigie kura wagombea wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA),” alisema Mbowe.
Mbowe, alisema CHADEMA haitaki ushindi wa dezo bali wanataka uchaguzi huru na wa haki ili mshindi atakayepatikana, ashinde kwa haki.
Aidha, CHADEMA imetahadharisha kuwa endapo vurugu za kuwaengua wagombea wake zitaendelea, chama hicho kitakwenda mahakamani kusimamisha uchaguzi huo.
Naye Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, Issaya Mwita, awali akitoa taarifa ya mchakato wa uchaguzi huo alisema katika Kata hiyo ya Vijibweni kuna mitaa sita.
Alisema katika mitaa hiyo, Chama Cha Wananchi (CUF), kimesimamisha wagombea wawili huku CHADEMA kikisimamisha wanne.
(CHANZO: TANZANIA DAIMA)

0 comments:

MABOMU YAFUKULIWA NA WACHIMBA MTARO



Mabomu Nane ya kutupwa kwa mkono yanayodaiwa 

kutengezwa China na Urusi yafukuliwa na wachimbaji wa 

mtaro kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mganga yakiwa 

yamehifadhiwa ardhini karibu na nyumba moja katika kijiji 

cha Mabamba wilayani Kibondo mpakani mwa Tanzania na 

Burundi.

Nini maoni yako kuhusiana na kuzagaa kwa mabomu ya aina hii 


katika makazi ya watu

0 comments:

MMMMHH KUMBE NAYE YUMO:ZARI AFUNGUKA KUHUSU TUHUMA YA ACT VIDEO YAKE CHAFU


#Repost @zarithebosslady Zari>Hii kuhusu Picha Za Mkanda Wa Ngono Kusambazwa.

 Dearest friends, my fans all over the world, relatives and well wishers, as you may be or may not be aware, the print media in Uganda is awash with stories infringing on my fundamental inalienable human rights by attacking my modesty both as a woman and a mother to the utter prejudice of my private life and family. 

The clear motive of such publication is undoubtedly to deter and/or downplay my tireless efforts in my preparations for The Zari All White Party slated for 18/12/14 which to a large extent has rubbed some of my detractors the wrong way. 

I have no doubt in my mind that the pictures that appeared in today's Red Pepper issue were leaked by someone for their own selfish motives. 

Be that as it may, I would like to affirm that what goes on in my private life is absolutely my business that has no reason whatsoever to find it's way in the public realm. Privacy to/for/of a person is not a right granted by anyone, but it's inalienable.

 I am therefore steadfast in my resolve to hold the Zari All White Party for all my fans and friends in Uganda. 

And whilst I explore the option of seeking with a view of taking legal action against the perpetrators/detractors and/or publishers, I want to assure all my family, fans and friends again to disregard such hurtful reports aimed at scoring cheap social points. 

Lastly, I call upon one and all to attend the All White Party as there'll be incredible performances from various artists including Diamond Platinumz, whose attendance is confirmed.

 I'd love to see you there, I'll be there to welcome you all and God willing, we shall have a great time like we always do. Bless you all, Zari. 

0 comments:

MKANDA WA NGONO WA ZARI THE BOSSLADY WAVUJA!


Mkanda wa ngono unamuonesha mfanyabiashara wa Uganda, Zarinah Tlale maarufu kama Zari the Bosslady akifanya mapenzi na mwanaume asiyejulikana umesambaa.


Picha za Zari akivunja amri ya sita kutoka kwenye mkanda huo zimechapishwa kwenye gazeti la udaku la Red Pepper la Uganda.

“For exclusive pictures and a clear description of how Zari moans in bed, Please hurry and Grab Red Pepper copies of Friday and Saturday from the nearest vendor,” umeandika mtandao huo.

Zari ambaye hivi karibuni amekuwa na uhusiano na Diamond Platnumz, amesema mkanda huo umetolewa kwa makusudi ya kumharibia biashara zake.

Kupitia Instagram, Zari amezungumzia kitendo hicho kwa kirefu:

Photo and caption that claim Zari is the nude lady published by Kakensa-Emedia

Dearest friends, my fans all over the world, relatives and well wishers, as you may be or may not be aware, the print media in Uganda is awash with stories infringing on my fundamental inalienable human rights by attacking my modesty both as a woman and a mother to the utter prejudice of my private life and family. The clear motive of such publication is undoubtedly to deter and/or downplay my tireless efforts in my preparations for The Zari All White Party slated for 18/12/14 which to a large extent has rubbed some of my detractors the wrong way.

 I have no doubt in my mind that the pictures that appeared in today’s Red Pepper issue were leaked by someone for their own selfish motives. Be that as it may, I would like to affirm that what goes on in my private life is absolutely my business that has no reason whatsoever to find it’s way in the public realm.

Privacy to/for/of a person is not a right granted by anyone, but it’s inalienable. I am therefore steadfast in my resolve to hold the Zari All White Party for all my fans and friends in Uganda. And whilst I explore the option of seeking with a view of taking legal action against the perpetrators/detractors and/or publishers, I want to assure all my family, fans and friends again to disregard such hurtful reports aimed at scoring cheap social points. Lastly, I call upon one and all to attend the All White Party as there’ll be incredible performances from various artists including Diamond Platinumz, whose attendance is confirmed. I’d love to see you there, I’ll be there to welcome you all and God willing, we shall have a great time like we always do. Bless you all, Zari.

Zari allegedly hooked up with Farouk Sempala in a hotel room in Pretoria, South Africa.


0 comments:

BAADA YA KUSEMA ""HATA ALI SIMUONI"" DIAMOND AZIDI KUMSHUSHIA MADONGO ALI KIBA.... JIONEE ALICHOPOST KWENYE ACCOUNT YAKE FACEBOOK.... WEMA NAE APEWA DOZI YAKE MOJA









HIZI NI MESSAGE AMBAZO ALLY KIBA ANATAKIWA AZISOME...........







WEMA HII INAKUHUSU......................







0 comments: