Woman dies on transatlantic flight from Heathrow to Newark

A female traveller has died aboard a United Airlines flight from London Heathrow to Newark, in New Jersey, USA


The woman, believed to be from Newark, USA, was travelling alone aboard the United Airlines flight from London Heathrow.
She was found unconscious soon after take-off as the plane was mid-air, it is believed.
Despite the efforts of a doctor on the plane, the female traveller – who has not been named – died one hour before Flight 115 touched down in New Jersey.

The woman is believed to have suffered with a pre-existing medical problem, Port Authority spokesman Joe Pentangelo confirmed in an email.
But sources close to the matter have confirmed that the female passenger's condition was not contagious and has not put other passengers on the flight at risk.
A medical examiner arrived with police as the United plane landed at 2:50am GMT last night at Newark Airport, New Jersey, to make the pronouncement.
Preliminary examinations seems to indicate that the female passenger is understood to have "passed away from natural causes", said a Port Authority spokesperson.
Authorities are currently awaiting the results of an autopsy which they hope will uncover the cause of death.
United Airlines spokesperson Mary Ryan said: "United confirms that a passenger passed away on flight UA115 from London Heathrow to New York/Newark on December 1 2014.
"We offer our condolences to the passenger’s family.
"For privacy reasons, it would not be appropriate for us to comment further.
"

0 comments:

Manchester United, Chelsea, Arsenal and Liverpool told to fork out £35m to land Carvalho in January


Sporting Lisbon insist that William Carvalho won’t be leaving the club for the Premier League in January unless his £35m release clause is met.
Arsenal, Manchester United, Liverpool and Chelsea have all been linked with a move for the 22-year-old, who can play in midfield and defence.
All four clubs were interested in Carvalho over the summer, but were put off by Sporting’s refusal to budge on their asking price.
And while the Lisbon club may be prepared to negotiate more next summer, they are keen to keep their core together for the remainder of this season.
Indeed, reports suggest that Carvalho – along with Rui Patricio, Fredy Montero and Islam Slimani – will remain at the Estadio Jose Alvalade unless Sporting’s hand is forced by someone meeting the players’ release clauses.
Such a move may be a boost to United’s chances of beating Arsenal, Liverpool and Chelsea to the Portuguese international, with Sporting leaving the option option for a swap deal involving Nani at season’s end.
Nani has been in electric form since returning to his homeland, however Sporting insist they do not have the financial firepower to make the deal permanent next summer.
However, that could change if United are willing to use the winger as a makeweight in a deal for Carvalho.

0 comments:

Arsenal and Liverpool On Alert After Ligue 1 Target Declares Exit Intentions


Prolific Marseille striker Andre-Pierre Gignac revealed on Tuesday that he plans to leave Ligue 1 at the end of the current season, with Arsenal and Liverpool thought to be monitoring the French star.
The 28-year-old will be out of contract with his current club at the end of the campaign, and appears to be looking for a new challenge.
He is currently the top scorer in the French league, netting 11 times already after just 15 games. His goalscoring exploits have caught the attention of a number of top clubs including Inter Milan, Arsenal, and Liverpool.
It seems they may have to wait to get their man however, with Gignac seemingly happy to see out his contract with Marseille.
“I think I’ll leave at the end of the season,” he said.
“I’d like to know if [coach Marcelo] Bielsa will stay. But I’m looking for a high-level challenge. I’ll examine all proposals carefully.”
His good form has earned him a recall to the French international squad, although his place may be under threat following the early return from injury of Olivier Giroud.


0 comments:

ZITTO KABWE: KASHFA NNE MBAYA ZAIDI YA ESCROW ZINAKUJA.. JIANDAENI


Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto amesema baada ya kukamilisha shughuli ya ufisadi wa Akaunti ya Tegeta Escrow ambayo Sh306 bilioni zilichotwa, kamati yake sasa inaelekeza nguvu katika kashfa nyingine nne.
 
Zitto alisema kamati yake itatumia mwezi huu na Januari kupitia ripoti nne ambazo zina masilahi kwa Taifa, ikiwamo ya utoaji wa vibali vya kuagiza na kuingiza sukari nchini.
 
Alisema ufisadi katika utoaji wa vibali hivyo ni mkubwa kuliko sakata la escrow... “Hili linagusa moja kwa moja maisha ya wananchi, wamiliki wa viwanda na uzalishaji. Tayari tumewaita Bodi ya Sukari tujadiliane kwa kina kuhusu suala hili,” alisema.
 
Mbali na suala la sukari, alizitaja ripoti nyingine kuwa ni ya uchunguzi wa ubinafsishaji wa Benki ya NBC, ripoti maalumu ya Bandari na mikataba ya gesi.
 
“Baada ya kazi ya PAC, tunapumzika, kwani kama unavyojua kazi ilikuwa ngumu, wiki mbili nilikuwa silali. Kwa kuwa tuna ratiba ya wiki mbili. Kwa Desemba na Januari tutaanza kuzifanyia kazi,” alisema Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema).
 
Wiki iliyopita, Bunge lilijadili ripoti ya PAC kuhusu ufisadi katika Akaunti ya Tegeta Escrow na kuhitimishwa kwa kuweka maazimio manane yakiwamo ya kuitaka Serikali iwawajibishe baadhi ya mawaziri na watendaji wengine wakuu huku likitaka pia uchunguzi uendelee kwa wote waliotuhumiwa kupokea fedha hizo kwa njia moja au nyingine.
 
Kauli ya Zitto inakuja wiki moja baada ya wamiliki wa viwanda vya sukari vya Kagera, Mtibwa na Kilombero kutishia kuvifunga kutokana na kuviendesha kwa hasara.
 
Wamiliki hao walisema watafunga viwanda hivyo kutokana na Serikali kushindwa kuzuia uagizwaji wa sukari nchini kinyume cha taratibu.
 
Mkurugenzi wa Viwanda vya Kagera na Mtibwa, Seif Seif alisema uagizaji wa sukari kutoka nje unafanyika kwa ushirikiano wa wafanyabiashara wakubwa na vigogo serikalini kinyume cha makubaliano na hivyo kurudisha nyuma maendeleo ya viwanda.
 
“Tulikubaliana kwamba Serikali iwe inaagiza tani 100,000 kutoka nje lakini sukari inayoingizwa sokoni ni zaidi ya tani hizo. Sukari tunayozalisha katika viwanda vyetu ipo na haina pa kwenda,” alisema Seif na kuongeza:
 
“Leo ukipita katika maduka utakutana na sukari ya kila aina, wafanyabiashara wanaoagiza wanawatumia vigogo serikalini kuingiza sukari wapendavyo, tena bila kulipa kodi,” alisema Seif.
 
Kutokana na hali hiyo, Seif alisema wamelazimika kupunguza wafanyakazi 2,000 na kubakiwa na 5,000 katika Kiwanda cha Kagera, Kilombero imepunguza 3,000 na wamebaki 6,000 huku Mtibwa ikiondoa wafanyakazi 3,000.
 
“Hali ni mbaya, si kama Watanzania wanavyofikiri. Tukifunga kabisa Watanzania wengi watakosa ajira kama ambavyo mnaona wengine wamekosa, hatuwezi kuendelea kufanya biashara ya hasara ambayo Serikali inaihalalisha,” alisema.
 
Mwenyekiti wa Bodi ya Kiwanda cha Sukari Kilombero, Balozi Ami Mpungwe alisema: “Hali ni mbaya, tunaona kuliko kuendelea na hali hii ni bora tusimame kuzalisha sukari.
 

“Serikali kama kweli ina dhamira ya kuvifufua na kuviendeleza viwanda vyetu vya ndani ni lazima kuvilinda na kupiga marufuku uagizwaji holela wa sukari kutoka nje.”

0 comments:

AL SABAB YACHARUKA..... YAUA WATU 36 NCHINI KENYA


Takribani watu 36 wanahofiwa kufariki katika shambulio lililotokea kwenye machimbo ya kokoto karibu na mji wa Mandera kaskazini mwa Kenya. Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya limethibitisha.
 
Wakazi wa eneo hilo wamesema waathirika wote wa tukio hilo ni watu wasio Waislam ambao walikuwa wakifanya kazi katika machimbo hayo yaliyopo Kormey kilomita 15 kutoka mji wa Mandera Kaskazini mwa Kenya.
 
Tukio hili linafuatia tukio la wiki moja iliyopita ambapo watu wapatao 28 waliuawa katika shambulio la basi la abiria huko Mandera.

Kundi la wapiganaji wa Kiislam la Al Shabab limekiri kuhusika na mauaji hayo.


0 comments:

MVUA ILIYONYESHA LEO ASUBUHI JIJINI MWANZA YASABABISHA MAFURIKO


Mvua kubwa iliyonyesha asubuhi ya leo jijini Mwanza, imesababisha mafuriko katika baadhi ya maeneo kama inavyoonekana pichani.
 
Baadhi ya wakazi wa jiji hilo hawana sehemu za kukaa baada ya maji kuingia kwenye nyumba zao na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali.

 

 


0 comments:

DIAMOND PLATNUMZ ASHIRIKI PROJECT YA EBOLA


Nyota wa muziki Diamond Platnumz ambaye mwishoni mwa wiki ameweza kushinda tuzo tatu huko Afrika Kusini, amekuwa ni moja kati ya wasanii wakubwa Afrika walioshiriki katika project ya pamoja inayokwenda kwa jina We are the World Africa.


Kazi hii kubwa imefanyika huko Afrika Kusini ikiwashirikisha pia mastaa kutoka nchi nyingine za Afrika kama vile Banky W, Mafikizolo, Iyanya, Don jazzy na wengineo wengi.
 
Kabla ya kuondoka Tanzania Diamond aliiambia Mpekuzi juu ya ushiriki wake katika project hiyo kubwa, ikiwa pia na lengo la kuongeza uelewa juu ya Gonjwa la Ebola ambalo limekuwa tishio nchi za Afrika Magharibi na Afrika kwa ujumla.

0 comments:

AL SHABAAB YAWAPONZA WAKUU WA USALAMA KUTIMULIWA KAZI KENYA


Rais Uhuru Kenyatta amemwachisha kazi waziri wa usalama Joseph Ole Lenku na kumpendekeza waziri mpya wa usalama Joseph Nkaiseri kuchukua nafasi hio.
 
Wakati huohuo mkuu wa polisi nchini Kenya inspekta generali David Kimaiyo amejiuzulu kutokana na shinikizo dhidi yake afanye hivyo kwa kushindwa kukabiliana na utovu wa usalama nchini.
 
Rais Kenyatta alisema kuwa baada ya mazungumzo na Bwana Kimaiyo alikubali 'kustaafu' mapema kutoka kwa majukumu yake kwa sababu za kibinafsi.
 
Rais alitoa tangazo hilo wakati akihutubia taifa kufuatia shambulizi la hapo jana dhidi ya wachimba migodi 36 waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera Kaskazini ya Kenya.



Rais pia alitangaza kuwa amekubali ombi la Generali wa polisi David Kimaiyo kuachia wadhifa wake.
 
Kimaiyo na Ole Lenku wamekuwa wakikabiliwa na shinikizo za kuachia ngazi kufuatia kukithiri kwa utovu wa usalama nchini.
 
Hatua ya kuwatimua kutoka katika nyadhifa zao wawili hao bila shaka litakuwa jambo la kuridhisha kwa wakenya wengi ambao wamekuwa wakilalamikia utovu wa usalama na kuwataka waondoshwe ofisini.
 
Uteuzi wa Joseph Nkaisery kama waziri mpya wa usalama ni jambo jipya kwani atakuwa mwanasiasa wa kwanza kutoka kwa upinzani kuwa ndani ya serikali.
 

Alipokuwa anahutubia nchi,Rais Kenyatta aliwasihi wabunge kuongeza mda wa vikao vyao vya leo ili kumhoji na kumkagua Nkaisery aliyeteuliwa kuchukua nafasi ya waziri mpya wa usalama na maswala ya ndani ili wamuidhinishe.

0 comments:

IKULU YASEMA ITATEKELEZA MAAZIMIO YA BUNGE KWA NGUVU KUBWA....YASUBIRI TAARIFA RASMI ILI RAIS ACHUKUE UAMUZI


SIKU chache baada ya Bunge kuhitimisha mjadala wa uchotwaji wa zaidi ya Sh bilioni 300 kwenye akaunti ya Tegeta Escrow na kupitisha maazimio nane ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha watendaji na wanasiasa waliohusika, Ikulu imesema itayafanyia kazi maazimio hayo kwa uzito mkubwa.
 
Hayo yalisemwa jana na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alipozungumza na MTANZANIA juu ya hatua iliyofikiwa katika kutekeleza maazimio yaliyofikiwa na Bunge.
 
Balozi Sefue alisema hadi sasa ofisi yake ilikuwa haijayapokea maazimio hayo rasmi kutoka bungeni.
 
MTANZANIA: Baada ya Bunge kufikia maazimio yake, ni hatua gani inafuata kwa upande wa Serikali hadi kuja kuyatekeleza?
Balozi Sefue: Ninavyojua ni kwamba Bunge litaleta rasmi mapendekezo hayo serikalini.
 
MTANZANIA: Ni muda gani utatumika kuyafanyika kazi baada kuwasilishwa rasmi serikalini?
Balozi Sefue: Siwezi kusema ni muda gani.
 
MTANZANIA: Kuna taarifa mabadiliko yatafanyika wakati wowote ndani ya juma hili, kuna ukweli wowote?
Balozi Sefue: Nasema hivi, kwanza hatujayapokea, lakini nikiyaona rais atayatafakari na kuyashughulikia, watu wasihisi kwamba ni leo, kesho au lini.
 
Maana ukiyasoma kwa nilivyoyasikia ni kwamba  wametoa ushauri, kwahiyo aliyeshauriwa ndiye atajua afanye nini na kwa wakati gani.
 
MTANZANIA: Kuna wasiwasi kuwa yawezekana huu ushauri usitekelezwe, hilo unalizungumziaje?
Balozi Sefue: Ndiyo nasema wewe soma vizuri lugha iliyotumika, kwa sasa hivi nasoma kwenye magazeti, lakini itakuja rasmi kiserikali, ikiwa rasmi wakati huo rais naye atayasoma na kujua cha kufanya.
 
Ushauri ni ushauri, lakini ushauri wa Bunge lazima uchukuliwe kwa uzito unaostahili, ndiyo ninachoweza kusema, hauwezi kuchukuliwa ‘lightly’ (kiwepesi), lazima utachukuliwa kwa uzito unaostahili, siwezi kukwambia kwamba rais ataamua vipi, ninachokwambia ni kwamba hawezi kuuchukulia ‘lightly’, ataupa uzito unaostahili.
 
DK. SLAA
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, amelipongeza Bunge kwa hatua iliyofikiwa huku akitilia shaka utekelezaji wa maazimio hayo kutokana na kile alichokiita ‘udhaifu’ wa Serikali katika kutekeleza uamuzi wake.
 
Alisema hofu yake juu ya utekelezaji wa maazimio hayo inatokana na ukweli kwamba mamlaka ya uteuzi imekuwa ikifanya maridhiano na wezi wa mali za umma na kumalizana kienyeji huku wezi wa kuku wakifungwa.
 
“Nimeweka kipimo cha kuangalia mamlaka ya uteuzi itachukua muda gani kutekeleza maazimio haya ya Bunge kwa sababu wajibu wa Bunge ni kusimamia Serikali na si kuhukumu.
 
“Kwa hatua hii, tumetengeneza taswira mbaya kwa kugeuza jinai kwa maridhiano kwa sababu tayari rais alishawahi kusema ana majina ya watu 40 wanaohusika na ujangili wa meno ya tembo, wasafirishaji dawa za kulevya na waliochukua fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
 
“Jambo la kushangaza hadi leo watu hao hajawataja na waliohusika na EPA aliwaomba warudishe fedha walizochukua, yaani watu ambao ni wezi wanapewa muda wa kwenda kujirekebisha, hii ni katiba ya nchi gani?”alihoji Dk. Slaa.
 
Aidha Dk. Slaa alisema taifa halina kumbukumbu na hiyo imethibisha wazi kwamba maazimio ya Bunge huwa hayatekelezwi kutokana na moja ya mapendekezo ya Bunge ya kuitaka Serikali kuutaifisha mtambo wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Solution Limited (IPTL) kwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).
 
NCCR-Mageuzi
Kwa upande wake Chama cha NCCR-Mageuzi kimesema kinaunga mkono maazimio hayo ambapo pia kimehoji uhalali wa kumwacha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
 
Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosena Nyambabe, alisema kuna mawaziri hawajui yanayotendeka katika wizara zao, lakini wamekuwa wakiwajibishwa na kuwajibika kutokana na makosa ya watendaji wao.
 
“Pinda alikuwa na taarifa zote kuhusu Akaunti ya Escrow, lakini hakuwajibishwa, kwanini ameachwa wakati kuna mawaziri hawajahusika, lakini wamewajibika?
 
“Lakini pia upinzani unatakiwa upewe pongezi nyingi katika hili kwa sababu wameonyesha uwezo wa kujenga hoja na wakasikika bila kutoka nje wala kusussia vikao,” alisema Nyambabe.
 
MAAZIMIO YA BUNGE
 
1) Harbinder Singh Seth (Mmiliki wa Kampuni ya Pan African Power, PAP) na wengine
Takukuru (Taasisi ya Kuzuia na Kudhibiti Rushwa) Jeshi la Polisi na Vyombo vingine husika vya Ulinzi na Usalama, vichukue hatua stahiki kwa mujibu wa sheria za nchi, dhidi ya watu wote waliotajwa na Taarifa Maalumu ya Kamati, kuhusika na vitendo vyote vya kijinai kuhusu miamala ya Akaunti ya Escrow, na watu wengine watakaogundulika kufuatia uchunguzi mbalimbali unaoendelea kuhusika katika vitendo vya jinai.
 
2 Mitambo ya IPTL
Bunge linaazimia kwamba, Serikali iangalie uwezekano wa kuichukua mitambo ya kufua umeme wa IPTL na kuimilikisha kwa Tanesco kwa mujibu wa sheria za nchi.
 
3 Mapitio ya Mikataba ya Umeme (Azimio la Kamati teule ya Richmond)
Bunge linaazimia kwamba, Serikali itekeleze Azimio husika la Bunge mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile kabla ya kumalizika kwa Mkutano wa Bunge la Bajeti la Mwaka 2015/2016, Serikali iwasilishe taarifa ya utekelezaji wa mapitio ya mikataba ya umeme.
 
4 Kitengo cha Rushwa kubwa
Bunge linaazimia kwamba; Serikali iandae na kuwasilisha muswada wa marekebisho ya sheria iliyounda Takukuru kwa lengo la kuanzisha taasisi mahususi itakayoshughulikia kupambana na kudhibiti vitendo vya rushwa kubwa, ufisadi na hujuma za uchumi zinazotishia uhai wa taifa kiuchumi, kijamii na kisiasa.
 
5 Majaji
Bunge linaazimia kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aunde Tume ya Kijaji ya Uchunguzi, kuchunguza tuhuma za utovu wa maadili dhidi ya Jaji Aloysius Mujulizi na Jaji Profesa Eudes Ruhangisa wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
 
6 Benki ya Stanbic na Benki nyingine
Bunge linaazimia kwamba, mamlaka husika za kifedha na za kiuchunguzi kuitaja Stanbic Bank Tanzania Ltd na benki nyingine yoyote itakayogundulika kufuatia uchunguzi wa mamlaka za kiuchunguzi, kujihusisha na utakatishaji wa fedha zilizotolewa katika Akaunti ya Escrow kuwa ni taasisi zenye shaka ya utakatishaji wa fedha haramu (Institutions of Money Laundering Concern).
 
7 Mawaziri, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Katibu Mkuu na Bodi ya Tanesco
Bunge linaazimia kwamba, Waziri wa Nishati na Madini, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Tanesco wawajibishwe kwa kuishauri mamlaka ya uteuzi kutengua uteuzi wao.
 
8. William Ngeleja, Victor Mwambalaswa na Andrew Chenge

Bunge linaazimia kwamba, kamati husika za kudumu za Bunge zichukue hatua za haraka na kwa vyovyote vile kabla ya Mkutano wa Kumi na Nane wa Bunge, kuwavua nyadhifa zao kwenye kamati husika za kudumu za Bunge.

Chanzo: Mtanzania

0 comments:

RAIS KIKWETE AMUAPISHA CAG MPYA, PROF MUSA JUMA ASSAD IKULU JIJINI DAR ES SALAAM


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitia sahihi yake kwenye nyaraka baada ya kumuapisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad nyaraka baada ya kumuapisha Ikulu jijini Dar es salaa  Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuangalia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad akiweka sahihi yake kwenye nyaraka baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad na CAG Mstaafu Bw. Ludovick Utouh Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali, Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda, Jaji Mkuu Mhe Mohamed Chande Othman, Spika Anne makinda na Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad na wafanyakazi wa ofisi ya CAG  Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na familia ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad Ikulu jijini Dar es salaam Novemba 02, 2014.
 (PICHA NA IKULU)

0 comments:

HATIMAYE WEMA SEPETU AONYESHA HISIA ZAKE JUU YA PICHA HII KWA KU-COMMENT KWA KUKEBEHI

WEMA GIVES A COMMENT ON ZARI AND DIAMOND'S K!SSING PHOTO


0 comments:

MAJIBU YA AUNT EZEKIEL BAADA YA KUULIZWA KUHUSU DIAMOND NA ZARI PAMOJA NA UJAUZITO.

Aunty

Kwenye U Heard ya leo Decemba 01 2014 Gossip Cop Soudy Brown ameongea na mwigizaji Aunt Ezekiel kuhusu ishu mbili tofauti ambapo ya kwanza ni kuhusu rafiki yake Wema kama amewahi kumwambia chanzo cha kuachana na Diamond.

Ishu ya pili ni Diamond kuonekana na Zari kwenye Tuzo za Channel O Afrika Kusini siku ya Jumamosi, Aunt Ezekiel amesema hajui chochote kuhusiana na masuala hayo na kusema hawezi kuzungumzia masuala ya mtu binafsi.
Soudy Brown akamuuliza swali jingine ambalo linahusiana na namna alivyoonekana kama mjamzito kwenye show ya msanii Mirror siku ya jana Maisha Club ambalo pia Aunty amesema hana ujauzito ila ni gauni alilovaa linamuonyesha hivyo.
Nimekuwekea hapa U Heard, 

0 comments:

Huenda hujayasikia haya ya Idris kutoka #BBA_Hotshots

Big-Brother-Hotshots_opt
Ni washiriki wanane tu waliobakia ndani ya Jumba la Big Brother Afrika Kusini, sasa wiki hii ni kama homa inapanda zaidi kwa kuwa kati ya hao ni mshiriki mmoja tu atakayetoka na ile zawadi ya pesa kiasi cha Dola 300,000/-.
Kampeni zinaendelea katika mitandao kumpigia kura Idris, tumeona watu wengi ikiwemo hata wale walioko nje ya Tz wakitia nguvu kubwa kwenye kampeni hizo.
Idris alionekana mwenye furaha usiku wa Jumapili Novemba 29 na kuna machache ambayo aliyasema baada ya kutajwa kuingia kwenye fainali hizo, haya hapa;
“... I love you Africa, I love you Tanzania… This game ain’t bad you know...”– Idris.
Halafu akaimba kwa kubadilisha mashairi ya Wiz Kid ya kwenye wimbo wa ‘Show the Money'; “… Tanzania gonna dance if I come with money…“– Idris.
Sentesi ya mwisho ilikuwa hii; “… Tanzania once again in the finals…“– Idris.
Comedy_week_day28_bba9

0 comments: