Watatu wafukiwa na kifusi wakichimba madini wilayani Kahama mkoani Shinyanga

0 comments




Wachimbaji watatu wa madini ya dhahabu ya Kalole kata ya Lunguya wilayani Kahama mkoani Shinyanga  wamefariki dunia baada ya kufukiwa na udongo wakiwa kwenye shimo la dhahabu wakitafuta dhahabu.

Kwa mujibu wa taarifa ya kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha alisema tukio hilo limetokea Januari 7,2015 saa 12 asubuhi katika machimbo madogo ya dhahabu ya Kalole kata ya Lunguya,tarafa ya Msalala wilayani Kahama.

Aliwataja waliofariki kwa kufukiwa kwenye shimo  hilo la dhahabu kuwa ni  Kulwa Magele(20) mkazi wa Shishani wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Ihalu Maheme(23) mkazi wa Idisa wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu na Lameck Frank(22) mkazi wa Nzega mkoani Tabora.

Kamanda Kamugisha alisema vijana hao ambao ni wachimbaji wadogo wa madini waligundulika wakiwa wamekufa ndani ya shimo la kuchimbia dhahabu na inaelezwa kuwa waliingia kwenye shimo hilo ambalo halitumiki kwa nia ya kuchimba dhahabu ndpo likabomoka na kuwafukia na kusababisha  vifo vyao papo hapo.
Wakati huo huo mwanamke aitwaye Sayi Shitunguru(50) mkazi wa  kijiji cha Buruma kata ya Isaka wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ameuawa kwa kupigwa kitu kizito kichwani na watu wasiofahamika akiwa nyumbani kwake.

Kamanda Kamugisha alisema tukio hilo limetokea Januari 7,2015 saa 1 asubuhi ambapo mwanamke huyo akiwa nyumbani kwake alivamiwa na mtu/watu wasiojulikana kasha kumpiga na kitu kizito kichwani na kusababisha kifo chake papo hapo.

Alisema chanzo cha tukio hilo bado hakijajulikana  na jeshi la polisi linaendelea kufanyan uchunguzi ili kubaini chanzo chake.

Hata hiyvyo alisema tayari wanamshikilia mtu mmoja aitwaye  John Jota(33) mkazi wa Kazungu wilayani Kahama kwa mahojiano zaidi huku akiwataka wananchi kushirikiana na polisi ili kusaidia kukamatwa kwa wahusika wa mauaji hayo.

Read More »

Kuhusu Ajali aliyopata Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi.

0 comments
Leo January 10 kupitia mitandao na blogs tofauti zimeenea taarifa na picha za ajali ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi. Taarifa nilizopokea mpaka sasa kuhusu ajali hii ni kwamba mhe Mbilinyi amepata ajali akielekea Dar es salaam kwenye kona kali iliyopo eneo la Kitonga, Iringa akiwa na watu wanne kwenye gari moja.
vyombo vya habari vimesema hakuna mtu aliyepoteza maisha waka kupata majeraha yeyote makubwa. Kamanda wa Polisi wa Iringa, Ramadhani Mungi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo leo.
sugu 1 
 sugu 2 
 sugu 3 
 sugu 4 
 sugu 5 
 sugu 6


Read More »

Ifahamu klabu pekee inayoweza kumsajili Messi kwa sasa… INGIA HAPA

0 comments
lionel_messi_barcelona

Huku habari kuhusu uhusiano mbaya wa Lionel Messi na klabu yake ukiendelea kutengeneza headlines kwenye vyombo vya habari barani Ulaya tetesi za kuondoka kwake zimezidi kushika kasi huku kila siku ikiibuka story mpya.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na mtaalamu wa biashara kwenye mchezo wa soka ni klabu mbili pekee ambazo kwa sasa zina uwezo wa kumsajili nyota huyu raia wa Argentina kinyume na ilivyoripotiwa kuwa klabu kadhaa ziko kwenye harakati za kumsajili.
Klabu hizi zimetajwa kuwa Manchester United na Real Madrid kutokana na kuwa na msuli wa kifedha pamoja na sababu nyingine ambazo zinaleta ugumu kwa zile klabu ambazo zinaweza kuwa na fedha lakini zikashindwa kufanya usajili kutokana na kubanwa kwenye sehemu tofauti.
Katika hali ya kawaida klabu kama Manchester City, PSG , Chelsea na Bayern Munich zinaweza kumsajili mchezaji yoyote kwa bei yoyote, lakini hali kwa sasa ni tofauti kwani kanuni za kusimamia matumizi ya fedha kwa vilabu ‘Financial Fair Play’ zinafanya matumizi kwa vilabu yafanywe kwa kuzingatia vitu vingi.
Hapa ndio mahali ambako United na Real zinapata faida endapo zitakuwa na dhamira ya kumsajili Messi.
Ili kumnunua Messi klabu inayomtaka itapaswa kulipa ada ya uhamisho ambayo ni paundi milioni 196 na mshahara wake utalazimika kuwa mkubwa kutokana na hadhi ya mchezaji mwenyewe na kwa mantiki hiyo ni United na Madrid pekee ambazo zinatengeneza aina ya fedha ambayo inaweza kutosha kumnunua Messi pasipo kukiuka sheria za Financial Fair Play.
Klabu ambazo zinatangaza hasara ya zaidi ya paundi milioni 23.5 kwa muda wa miaka mitatu zinaadhibiwa na sheria za FFP na tayari Man City na PSG zimekumbana na rungu hilo jambo ambalo linawaondoa kwenye mbio za kumsajili Messi endapo nyota huyo atawekwa sokoni.
Pamoja na ukweli huu bado haitakuwa rahisi kwa Barcelona kukubali kumuona Messi akiondoka hasa ukizingatia kuwa klabu hiyo ina adhabu ya kutofanya usajili kwa muda wa mwaka mzima hali inayowafanya wasiwe kwenye nafasi ya kumuuza mchezaji yoyote muhimu kwani kufanya hivyo itakuwa sawa na kujidhoofisha huku wakiwa hawana nafasi ya kujiimarisha.

Read More »

TAZAMA PICHA ALIZOPOSTI MCHUMBA WA NAY MTANDAONI INGIA HAPA

0 comments




Mchumba wa staa wa Bongo Fleva, Emanuel Elibariki 'Nay wa Mitego' , Siwema Edson 'Mama Curtis' amepost leo picha za mahaba akiwa kitandani na mzazi mwenzie huyo kupitia Account yake ya Instagram.

Read More »

Man U yamsajili kipa wa Barcelona

0 comments

Victor Valdes akisaini kuichezea Man U.

MANCHESTER, England  
KLABU ya Manchester United imethibitisha kumsajili kipa wa zamani wa Barcelona, Victor Valdes kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu.
Valdes mwenye umri wa miaka 32, alikuwa akifanya mazoezi na klabu hiyo tangu Oktoba, mwaka jana baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu akisumbuliwa na maumivu ya goti.
Valdes ameeleza kuwa amefurahishwa na usajili huo na yupo tayari kufanya kazi na kipa chaguo la kwanza la timu hiyo, David de Gea ambaye ni raia mwenzake wa Hispania.

Read More »

Yanga yamtema Kaseja rasmi, yamdai 400m

0 comments


Kipa wa Yanga Juma Kaseja.

YANGA imetangaza rasmi kuachana na kipa Juma Kaseja lakini Championi Ijumaa linafahamu ukweli kuwa klabu hiyo imepanga kumfungulia mashitaka ya kumtaka alipe shilingi milioni 400, kutokana na kuvunja mkataba.
Akitangaza kwa waandishi wa habari jana, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Jerry Muro alisema kuwa Kaseja ndiye aliyevunja mkataba na klabu hiyo kutokana na kutoonekana mazoezini kwa zaidi ya saa 48, hivyo kuvunja kipengele katika mkataba wake.
“Yanga inatangaza rasmi kuwa haitakuwa na kipa Juma Kaseja kwa sababu amevunja mkataba na klabu yetu na tunamtakia kila la kheri katika maisha yake mapya  huko aendako,” alisema Muro
Kuhusu madai kuwa Kaseja anaidai Yanga, Muro alifafanua: “Kaseja alisaini mkataba na klabu Novemba 8, 2013, siku hiyohiyo akalipwa shilingi milioni 20, makubaliano ilikuwa alipwe shilingi milioni 40 ndani ya kipindi cha mkataba wake wa miaka miwili na hakukuwa na muda maalum uliopangwa.
“Januari 15, 2014 klabu ikamlipa fedha zake zilizosalia shilingi milioni 20, lakini Novemba 11, 2014, akaleta barua ya malalamiko kadhaa kwetu akidai hapati nafasi ya kucheza jambo ambalo siyo kweli na alilalamika kuhusu masuala ya bima.
“Desemba 15, 2014, Klabu ya Yanga ilimjibu barua hiyo na kumfafanulia kile alichohitaji, lakini yote kwa yote hakuna ambacho anatudai wala tunachomdai.”Baada ya hapo gazeti hili lilipata taarifa za ndani juu ya mpango huo wa Yanga kumshitaki Kaseja kwa kukiuka masharti ya mkataba, lakini alipoulizwa Muro alisema hajui chochote kuhusua suala hilo.

Read More »

DAH INASIKITISHA SANA : MWANAFUNZI WA DARASA LA TATU ABAKWA NA WATU MPAKA KUFARIKI DUNIA KISHA KUMUWEKA KWENYE SINKI LA KUOGEA-MBEYA

0 comments


MWANAFUNZI wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Rwanda Nzovwe jijini Mbeya , Elika Mkubwa (8), amefariki dunia baada ya kubakwa na watu wasiojulukana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, alisema baada ya watu hao kufanya unyama huo, waliuweka mwili wa mtoto huyo katika sinki la kuogea kwenye nyumba moja ambayo haijakamilika ujenzi wake. Pamoja na hayo, alisema upelelezi bado unaendelea ili kuwabaini waliohusika na tukio hilo.
Akizungumza eneo la tukio, kiongozi wa Mtaa wa Ilomba, Ezekiel Mwakalandwa, alisema taarifa za mauaji hayo alizipata jana asubuhi kupitia kwa majirani zake.
Akizungumza eneo la tukio na paparazi huru, kiongozi wa Mtaa wa Ilomba, Ezekiel Mwakalandwa, alisema taarifa za mauaji hayo alizipata jana asubuhi kupitia kwa majirani zake.
"Nilipota taarifa hiyo, niliongozana na majirani tukiwa na ndugu wa marehemu na kushuhudia mwili wa mtoto huyo ukiwa umelazwa kwenye sinki la kuogea huku sehemu zake za siri zikiwa zimeharibiwa vibaya"
Mama mlezi wa mtoto huyo, Sala Mwandobo, alisema mtoto huyo alitoweka nyumbani kwake January 7 mwaka huu baada ya kuaga anakwenda kufua nguo za shule eneo la chemchem ya maji lililopo mbali kidogo na nyumbani kwake.

Read More »

Mume hanifikishi kisawasawa, Akimaliza yeye mimi nabaki bado na hamu INGIA HAPA KUSOMA HABARI KAMILI

0 comments


Mimi ni msichana wa miaka 27 nimeolewa miaka minne iliyopita na nina watoto wawili wote wa kike. Mwanzoni mwa mahusiano yetu na mume wangu (wakati tukiwa wachumba) na hata kama mwaka mmoja na nusu hivi kwenye ndoa yetu, baba watoto alikuwa ananiweza kweli....yaani nikikutana nae...aaah, allahmdullillah, nilikuwa naiona anga kwa uhalisia kabisa....na akiwa amechoka sana, basi hata mbili nitapata na kweli nilikuwa najisikia nime.....! Na kwa wiki nilikuwa napata kama siku nne hivi, yale mapigo ya sawa sawa.

Sasa kwa kipindi kama cha mwaka mmoja hivi...da, baba watoto kwa kweli ana underperform kabisa....wakati mwingine inapita wiki nzima, sionji na mimi mwanamke huwa nahitaji...nikimwambia anasema nimechoka sana kazini. Kwa heshima niliyo nayo kwa mume wangu, huwa namwambia sawa, lakini moyoni huwa nabaki na maswali mengi kuliko majibu. Huwa nahisi moja kati ya mambno haya:

1. Huenda mume wangu ameanza mambo ya nyumba ndogo, so akitoka kazini huenda anamalizia huko huko then akirudi nyumbani anakuwa hoi

2. Labda umbile langu limemchosha, coz kabla hatujaoana nilikuwa na bambataa ya wastani na kiuno chembamba, lakini now sio utani, nyonga imebaki vile vile lakini makalio yameongezeka mara-dufu, so huwa hafikii pale "Dar es Salaam" kisawasawa 

Haya yoye ni mawazo yangu ambayo ninayo moyoni. Sasa sijajua kama nimuulize au na mimi nianze kupiga show za nje kwani wanaonitongoza nikiwapanga kuanzia Dar, basi watafika hadi Morogoro......tatizo nampenda baba watoto na nimempa muda wa kama miezi 6 hivi, kama hatobadilika, basi nita-confirm namba moja ya hapo juu....So na mimi nitaanzia  kutafuta wa kurusha nae roho.

Read More »

Viongozi wa Siasa Wamcharukia Rais Kikwete…..Wamtaka Afanye Maamuzi juu ya Waziri wa Nishati na Madini.

0 comments

Viongozi wa vyama vya siasa nchini wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kutekeleza ahadi yake aliyoahidi wakati wa mkutano na wazee wa Dar es Salaam ya kufanya maamuzi ya kumwajibisha waziri wa nishati na madini ambaye alimweka kiporo na kudai kuwa atatoa maamuzi ndani ya siku mbili lakini hadi leo amekaa kimya.
 
Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF Prof Iibrahim Lipumba amesema suala la viongozi wakiwemo mawaziri kuwajibika halikuanza leo hasa anaposhindwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kuisababishia serikali hasara au kushusha heshima ya taifa hivyo ni vyema uwajibikaji ukawa ni kwa kila mtumishi wa umma bila kubagua ili kuleta tija kwa taifa.
 
slaa
Dk. Slaa
Kwa upande wake mjumbe wa halmashauri kuu taifa ya chama cha mapinduzi CCM Bw Najim Msenga amesema niimani ya chama chake kuwa rais atafanya maamuzi sahihi kwa maslahi ya taifa kama alivyoahidi na kwamba suala hilo haliwezi kuathiri uhai wa CCM kwani bado iko imara baada ya baadhi ya watuhumiwa kuchukuliwa hatua.
 
Akizungumzia suala hilo katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Dk Willbroad Silaa amesema hata hao waliojiuzulu na kuenguliwa uteuzi wao maadam uchunguzi ulifanywa na vyombo sahihi hadi kufikia hatua ya kupelekwa bungeni na kujadiliwa na wao kutoa maazimio watuhumiwa wote hadi sasa walipaswa wawe wamefikishwa mahakamani.
 
Katika mkutano wake na wazee wa Dar es Salaam uliofanyika ukumbi wa Diamond Jublee desemba 22 mwaka jana Rais Kikwete alitengua uteuzi wa aliyekuwa waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mh Anna Tibaijuka na kutangaza kumweka kiporo waziri wa nishati na madini Prof Muhongo

Read More »

WANNE WAFA AJALINI IRINGA SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments
Muonekano wa lori lenye namba za usajili T122 ALW baada ya kugongana na basi la Fanuel Express  yenye namba za usajili T919 DCD katika Kijiji cha Ibetelo eneo la Nyororo, wilayani Mufindi mkoani Iringa.
 
Basi la Fanuel Express  yenye namba za usajili T919 DCD baada ya ajali hiyo.
ZAIDI ya watu 4 wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya basi la abiria kutoka Mbeya kwenda Dodoma kugongana na lori katika Kijiji cha Ibetelo eneo la Nyororo wilayani Mufindi mkoani Iringa.
Kamanda wa Polisi Mkoani Iringa, Ramadhani Mungi amesema kuwa ajali hiyo imetokea saa 4.45 asubuhi na kuhusisha basi mali ya Kampuni ya Fanuel Express  yenye namba za usajili T919 DCD kugongana uso kwa uso na lori lenye namba za usajili T122 ALW mali ya Kampuni ya Transisco lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda nchi jirani.
Amesema watu wawili waliokuwa ndani ya basi wamefariki papo hapo na wote waliokuwa ndani ya lori wanahofiwa kufa, ambapo hadi kufikia  saa 7 mchana, watu wawili ndani ya lori walikuwa wamethibitika kufariki dunia na kufanya waliokufa kuwa wanne.

Zoezi la kuondoa miili iliyokuwa ndani ya lori linaendelea ambapo amesema kuwa huenda idadi hiyo ya waliokufa ikaongezeka.
Akielezea mazingira ya ajali hiyo, Kamanda Mungi amesema kuwa basi hilo lilikuwa likijaribu kulipita basi lililokuwa mbele yake katika eneo ambapo palikuwa na lori lingine lililoharibika, wakati huo huo lori lililohusika katika ajali hiyo lilikuwa likikwepa lori lililoharibika pamoja na basi hilo, ndipo magari hayo yalipogongana uso kwa uso katika jitihada za kukwepana.

Majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika Hospitali ya Mafinga, Iringa.

Read More »

Picha,Diamond Alivyokutana na Peter wa P Square na Fally Ipupa Nigeria. SOMA HAPA

0 comments
Unafuatilia habari za burudani Tanzania, basi utakumbuka swali waliloulizwa P Square walivyokuja Tanzania kuhusu kumfahamu Diamond. Jibu lao lilitengeneza drama kwa mashabiki wa Platnumz.
Diamond kwa sasa yupo Nigeria kwaajili ya tuzo za Glo-CAf. Amekutana na mastaa tofauti na miongoni mwao ni Peter wa P Square na Fally Ipupa.
diamond square
diamond pupa 2 diamond pupa 3 diamond pupa 4 diamond pupa 5 diamond pupa 6 diamond pupa

Read More »

WEMA, AUNT KICHEKO KABURINI KWA NGWEA INGIA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments
Mastaa wa Bongo, Wema Sepetu na shostito wake, Aunt Ezekiel wakiangusha kicheko katika kaburi la marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’.

INAWEZEKANA ilikuwa utani? Au ‘waliamka’ nazo?! Kweli binadamu anaweza kuvunjika mbavu (kicheko) juu ya kaburi la mpendwa wake? Mh!
Lakini imetokea! Wakati dunia ikisherehekea ujio wa mwaka mpya wa 2015, mastaa wa Bongo, Wema Sepetu na shostito wake, Aunt Ezekiel walionesha jambo tofauti kufuatia kutinga kwenye kaburi la aliyekuwa nyota wa Bongo Fleva, marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ na kutumia muda mwingi kucheka na kutuma meseji kwa simu wakiwa juu ya kaburi hilo.
ENEO LA TUKIO
Tukio hilo lililonaswa zimazima na kamera za paparazi, lilijiri Januari Mosi, mwaka huu kwenye kaburi la Ngwea lililopo katika Makaburi ya Kihonda mjini Morogoro.
ILIVYOKUWA
Aunt ndiye aliyeanza kutia timu kwenye makaburi hayo na kukaa. Baadhi ya ‘kruu’ ya Wema, akiwemo Petit Man nayo ilifika na kuungana na Aunt.Baada ya dakika tatu, Mama la Mama, Wema aliwasili akiwa ndani ya nguo isiyokuwa ya mtoko, akakaa upande wa pili wa kaburi. Yeye na Aunt walikaa kwa kupeana ubavu.
CHA AJABU SASA
Awali ilidaiwa kuwa, kruu hiyo ilipanga kuwa baada ya kufika kwenye kaburi hilo wangefanya dua fupi kwa ajili ya kumwombea marehemu apumzike kwa amani huko aliko.Lakini cha ajabu, kabla ya ibada hiyo, Wema, Aunt na wafuasi wao walikuwa wakipiga stori za hapa na pale na katika hali ya kushangaza zaidi, ilifika mahali wakaanza kucheka kile kicheko cha kuvunjika mbavu bila shuhuda wa tukio hili kujua nini hasa kilichokuwa kikiwachekesha!
Baadhi ya wapita njia waliokuwa wakikatiza karibu na makaburi hayo, nao walipigwa na butwaa kuwaona watu hao, walioamini ni ndugu wa marehemu, wakiangua vicheko kama hawana akili nzuri. kwa nukta kadhaa walisimama na kushangaa kabla ya kuendelea na ‘hamsini zao’.-
WEMA ATUMIA SIMU KUFICHA USO
Ni dhahiri kuwa, Wema alijishtukia kuwa kitendo cha kucheka juu ya kaburi hakikuwa na ujazo wa kiungwana hivyo haraka sana aliweka simu sehemu ya midomoni na kumfanya asionekane kwenye kamera kwamba alikuwa akicheka. Miwani ya jua aliyovaa pia ilimsaidia.
Wakati Wema akionesha ubinadamu huo, ‘mwenzangu na mimi’, Aunt yeye alijimalizia kiu yake ya kicheko mpaka pale alipoamua mwenyewe kuacha na si kwa kuogopa kamera wala malaika waliolizunguka kaburi lile (kama wapo) la mmoja wa marapa bora kabisa kuwahi kutokea Tanzania.
WEMA AJIELEZA
Baada ya wote kuacha kucheka na kila mmoja kuchukua nafasi ya ubinadamu, paparazi wetu alimuuliza Wema ni kwa nini walionesha kuwa na furaha juu ya kaburi la staa huyo.Wema: “Tumepita hapa ili kumuombea ndugu na rafiki yetu Mangweha hivyo hatuna lengo lingine zaidi ya hilo.“Ishu ya kupiga stori na kucheka, tusingeweza kuacha kuongea eti kisa tupo kaburini, maana kila kitu lazima kijadiliwe hata kukaa hapa tumekaa kwa sababu tunafarijika kuona kaburi la mwenzetu.”
Albert Mangweha ‘Ngwea’ enzi za uhai wake.
KWA NINI WALIFANYA ZIARA KABURINI KWA NGWEA?
Awali, mastaa hao na wapambe wao walikuwa na shoo ya kuukaribisha Mwaka Mpya iliyofanyika Desemba 31, 2014 ndani ya Ukumbi wa  Matei Lounge mjini Dodoma.Wakiwa wanarudi Dar, walipiga kituo mjini Morogoro ambapo miongoni mwa mambo waliyokuwa nayo kwenye ratiba ni kulitembelea kaburi la Ngwea na kuangusha dua fupi.
Hata hivyo, baada ya yote hayo, kundi hilo la Wema na watu wake hatimaye walifanya dua fupi ya kumuombea malazi mema Albert Mangweha.
KUMBUKUMBU MUHIMU
Mangweha alikuwa msanii wa Bongo Fleva. Akiwa na miaka 31 alifariki dunia, Mei 28, 2013 nchini Afrika Kusini. Chanzo cha kifo chake inadaiwa ni matumizi yaliyopitiliza  ya madawa ya kulevya. Alizikwa Morogoro, Tanzania, Juni 6, 2013.

Read More »

MSANII WA KIZAZI KIPYA MATONYA BAADA YA KULEWA KAVULIWA NGUO

0 comments

Picha hizi zimezagaa kwenye Mitandao tofauti tofauti ya kijamii ambazo zimeleta utata na kudai kuwa msani Maarafu wa kizazi kipya Matonya baada ya kulewa vijana wa kihuni walimvua nguo na kumfanya kitendo kibaya.... Mtandao huu unajaribu kumtafuta msanii huyu ili kutoa ufafanuzi wa picha hizi ila kwa bahati mbaya hatukufanikiwa kumpata

vijana wa kihuni wakifanya kazi yao

Read More »

10 wajeruhiwa ajali ya Noah wakitoka Maulid

0 comments
Mmoja wa majeruhi, Mwanahawa Ramadhani, akiwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Muheza kupatiwa matibabu baada ya kuvunjika mkono kutokana na ajali ya gari wakitokea Bagamoyo mkoani Pwani kusherehekea Maulid. 
Watu 10 wamejeruhiwa baada ya gari dogo aina ya Noah kupinduka katika kijiji cha Kitumbi Wilaya ya  Handeni mkoani Tanga.

Ajali hiyoilitokea juzi gari hilo likiwa limebeba abiria wanawake watupu waliokuwa wakitoka Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kusherehekea sikukuu ya Maulid kuelekea kijiji cha Kwakibuyu kata ya Songa wilayani Muheza.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga,  Frasser Kashai, abiria waliopata ajali hiyo walikuwa wakitoka katika Msikiti wa Songa kwa Kibuyu wilayani Muheza.

"Walikodi magari mawili yote aina ya Noah moja liliwabeba wanaume na lingine wanawake kwa ajili ya kuwapeleka Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kusherehekea Maulid," alifafanua Kamanda Kashai.

Alifafanua kuwa baada ya Maulid kumalizika, waligeuza siku iliyofuata kurejea Muheza.

Alisema kuwa gari iliyokuwa imewabeba wanawake, ilitangulia mbele na kufuatiwa ya wanaume.

Hata hivyo, Kamanda Kashai alisema walipofika maeneo ya kijiji cha Kitumbi, gari lililokuwa limewabeba wanawake, lilipinduka na kusababisha majeruhi hao.

Alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni baada ya dereva kutaka kulipita gari lingine ambapo lilitokea gari lingine mbele yake na alipojaribu kulikwepa, likapinduka

Baadhi ya majeruhi walivunjika mikono katika ajali hiyo.

Sheikh Mkuu wa kata ya Songa, Twaha Saidi, alimueleza Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu, aliyekwenda kuwajulia hali majeruhi hao katika Hospitali Teule Muheza kuwa majeruhi wote walioumia ni waumini wa dini ya Kiisilamu na walikuwa wanatoka katika Maulid wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

Na katika hatua nyingine, majeruhi sita wa ajali ya ajali ya basi dogo aina ya Hiace wakati wakitokea kijiji cha Misozwe kuelekea mjini Muheza mjini, wamelazwa Hospitali Teule Muheza, wametoa kilio kwa Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu,  wakidai  kwamba tangu wapate ajali hiyo zaidi ya wiki moja sasa, hawajapatiwa huduma yoyote ya matibabu.

Kutokana na kilio cha majeruhi hao, Mgalu amewaagiza viongozi wa hospitali hiyo kuwashughulikia haraka majeruhi hao ikiwamo na kuwapiga picha za X-ray.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya, ameahidi kwamba atafika hospitali hapo kila siku kusikiliza kero za majeruhi hao.

Read More »

BREAKING NEWS: Askari wa jeshi la polisi ajiua kwa kujipiga risasi ya Mdomoni Mkoani Mbeya

0 comments

Askari wa jeshi lapolisi, Sajenti Patrick Kondwa amejiua kwa kujipiga risasi akiwa katika ofisi yake kwenye ghala lakuhifadhia silaha katika kituo cha polisi cha wilaya ya mbozi mkoani mbeya.
Akizungumza na Paparazi wetu kwanjia ya simu, kamanda wa polisi mkoawambeya amekiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa chanzo cha kifo hicho bado hakijafahamika na kwamba jeshi lapolisi linaendelea na uchunguzi wa tukiohilo.
 
Sajenti Patrick mwenye umri wamiaka 54 ,akiwa katika ofisi yake kwenye chumba cha kuhifadhia silaha katika kituo cha polisi cha wilaya ya mbozi amejipiga risasi mdomoni ambayo imetokea kisogoni na kuondoka na uhai wake, tukio ambalo limetokea majira ya saa tisa usiku na kuthibitishwa na kaimu mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo, ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya ileje, Rosemary Staki Senyamule.
 
Baadhi ya waombolezaji ambao wamezungumza na Mwandishi wetu wamesema kuwa wamepokea msiba huo kwa masikitikomakubwa hasa kwa kuzingatia kuwa Sajenti Patrick alikuwani askari mwadilifu na anayeipenda kazi yake.

Read More »

Ata baada ya kupewa ushauri,Wasanii wa Rnb bado wanapiga picha vifua wazi,huyu mwingine. WAKUBWA TU

0 comments
Msanii wa Rnb uliyemsikia kwenye hit zake kama 2 On na Pretend “Tinashe” ameng’arisha jarida la V kwa picha zake akiwa kifua wazi kwenye toleo la mwaka 2015.
Tinashe amezungumzia kufananishwa na Jhene Aiko na kusema ‘ kama kila msanii anatengeneza kazi bora basi wote tuna nafasi yetu kwenye muziki ila tusichanganye mashabiki ‘.
Tinashe-x-V-Magazine 
 Tinashe-x-V-Magazine-2 Tinashe-x-V-Magazine-Music-Issue-700x954

Read More »

Unaambiwa huko DMV imedondoka Theluji (Snow) balaaa

0 comments

B6rCt6nIYAICE3Q


Kama vile matangazo ya hali ya hewa yalivyo tolewa mwazoni mwa wiki hii na National Weather Service, katika maeneo mbali mbali ya hapa DMV kwamba hali ya hewa itazidi kuwa baridi na kutegemea kuanguka theluji ya inches mbili hadi tatu katika maeneo mbali mbali hapa DMV

Read More »

Hii sasa Kali Angalia Picha,Unataka midomo tofauti,Daktari anakosea,Imemtokea Mwigizaji wa kike wa filamu za X.

0 comments
0106-farrah-abraham-lips-twitter-9
Farrah Abraham mwigizaji wa filamu za wakubwa amekutwa na mkasa uliobadilisha maisha yake baada ya kufanyiwa zoezi la kuongeza midomo yake na daktari kukosea na midomo kuwa tofauti na alivyotaka.
Farrah anasema ” alifanya uchunguzi wa zoezi hili na kumtafuta daktari bora wa kazi hii, ganzi niliyochomwa kabla ya zoezi ndio imesababisha nipate tatizo hili, haikuendana na mimi ” .
lips 3

Read More »

MWANAMKE AINGIZWA CHUPA SEHEMU ZA SIRI NA KUSHAMBULIWA KWA NYAYA ZA UMEME

0 comments

Mkazi wa Kitangiri jijini Mwanza, Biera Edwin (22) amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure akipatiwa matibabu baada ya kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili wake kwa tuhuma za kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mume wa mtu.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola hakupatikana kuzungumzia tukio hilo, lakini Biera mwenyewe alisema kabla ya kufanyiwa kitendo hicho mama ambaye ni jirani yao alimtuma mtoto wake amwite nyumbani kwao, alipokwenda mama huyo alianza kumshambulia.
Alisema alimshambulia akishirikiana na marafiki zake na kumjeruhi vibaya kwa nyaya za umeme, kumwingizia chupa kwenye sehemu zake za siri na baadaye kuchoma nguo zake.
Binti huyu kwa sasa amelazwa katika wadi ya majeruhi kwenye Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure akipatiwa matibabu na alisema baada ya kufanyiwa ukatili huo pia waliteketeza nguo zake kwa moto.
Kama da wa polisi mkoa wa mwanza,Valentino mlowola

Naye dada wa majeruhi, Nice Cosmas anaeleza kuwa akiwa nyumbani kwao, mama huyo wa jirani alituma watoto wake ambao walieleza kuwa wakamchukue mtu wao.
Alisema walipokwenda hapo jirani alimkuta ndugu yake akiwa hana nguo huku akiwa amejeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake.
Alisema walilazimika kurudi nyumbani kumchukulia nguo za kumvisha na kisha kutoa taarifa kwa mamlaka husika kabla ya kumpeleka hospitali kwa matibabu.
Baadhi ya viongozi wa mtaa wa Kitangiri A walisikitishwa na kitendo hicho na kuomba vyombo vya sheria kuwachukulia hatua kali wahusika.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Kitangiri A, Issa Salum alisema wanataka haki itendeke kwani kitendo hicho ni nusu ya mauaji.
Naye Mjumbe wa Serikali za Mitaa, Mariam Yusuf alisema mama huyo wa jirani alipaswa kutoa taarifa kwa mabalozi ama kwa wazazi wa binti huyo kama alikuwa na uhakika na madai yake kabla ya kuchukua ukatili dhidi ya binti huyo.


Read More »

NEW ALART: CCM KUANZA FAGIO LA VIONGOZI WIKI IJAYO

0 comments

Chama cha Mapinduzi (CCM) wiki ijayo kitaanza rasmi vikao vyake kwa ngazi ya Taifa vitakavyo chunguza maadili ya viongozi ikiwa ni maandalizi ya kuwapata wagombea wanaokubalika na wananchi katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alitoa taarifa hiyo jana katika mkutano maalumu wa kuwashukuru Watanzania kwa kukichagua chama hicho katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Desemba 14, mwaka jana. Alisema chama chake kinajipanga kuwa na viongozi wasio wamangimeza na wenye moyo wa kuwatumikia wananchi.
Katibu huyo Mkuu aliwashukuru Watanzania kwa kukipa ushindi chama chake na kubainisha kuwa kitaifa, CCM imeshinda kwa asilimia 81.
Hata hivyo, alisema katika maeneo ambayo imeshindwa kama Wilaya ya Pangani, itafanyika tathmini na watajipanga kuhakikisha Uchaguzi Mkuu ujao wanapa ushindi wa kishindo.Alisema watahakikisha wanashinda katika maeneo yote waliyofanya vibaya.

Read More »

Alichosema Ney Wa Mitego Kuhusu Nikki Mbishi Kuacha Muziki

0 comments
ney
Kupitia exclusive interview na Power Jams, Ney wa Mitego amezungumzia hatua ya Nikki Mbishi ya kuacha muziki nakusema “Ukiona kitu hakikulipi ni bora uachane nacho, mtu anaweza kuangalia kitu na kujua hakimfai na bora afanye mambo mengine
Ney aliendelea kusema ” Sijui kwanini amechelewa, nimefurahi kuona maamuzi mazuri kijana mwenzangu aliyofanya, amejitambua na kuamua kuangalia vitu vingine, niko tayari kumshauri kama bado hajapata cha kufanya” .

Read More »