Muendelezo wa Lil Wayne kujitoa Cash Money,kuondoka na Drake,Minaj na Tyga, Viko hapa


wayne-birdman 

Rapa Lil Wayne ameripotiwa na mtandao wa TMZ kuwa amefungua kesi ya madai ya dola milioni 51 pesa alizotakiwa kulipwa na Birdman toka mwaka jana kwa muziki aliotoa chini ya usimamizi wake.
Malipo mawili anayotakiwa kupokea Lil Wayne ni dola milioni 51 ya kazi za mwaka jana na dola milioni 8 za kurekodi album ya The Carter V toka December 2013 ambazo ni pesa za awali kabla ya kufanya album na dola milioni mbili baada ya album kukamilika kwa album.
Report zinasema Universal inayosambaza album za Cash Money italipa deni la milioni 10 na tayari kampuni hio imewaambia Cash Money watatue matatizo yao.
Lil Wayne akilipwa dola milioni 10 hatakuwa tena na sababu za kutaka kusitisha mkataba na Cash Money, na kuhusu album kutoka hio itabaki kuwa maamuzi ya Birdman.

0 comments: