Watu wenye ulemavu wa ngozi kuandamana hadi Ikulu

 
 
Akiongea na waandishi wa habari afisa habari wa TAS Josephat Tonner amesema kuwa ni dhamira ya chama kujua kwa nini serikali imeendelea kuangalia vitendo vya kikatili wanavofanyiwa watu wenye albinism nchini huku vitendo hivyo vikiendelea.
Aidha, katika hali isiyo ya kawaida majira ya saa nne na robo leo asubuhi mtu mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mwalimu Mussa aliamua kutembea bila nguo katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi eneo la daraja la salenda mpaka barabara ya Kenyata jijini
Dar es Salaam huku watu wakimtazama na kupita bila kujali.
Hali hiyo iliwalazimu badhi ya watu kuchukua hatua za kumvisha nguo kijana huyo huku wakielezea kuwa ni kukosekana kwa utu kwa watu kumpita hasa watu waliopewa dhamana ya ulinzi wa binadamu bila kuchukua hatua yeyote, huku kijana huyo akieleza mkasa uliomfanya ateembee uchi wa mnyama.

0 comments: