Linah na Recho Wanaswa Wakifanya Mambo ya Aibu Mbele ya Watu


Masistaduu wa Bongo Fleva, Estelina Sanga ‘Linah’ na rafiki yake, Winfrida Josephate ‘Recho’, wamefanya mambo ya aibu mbele ya kadamnasi.

 
Tukio hilo la aibu lilijiri hivi karibuni usiku kwenye bwawa la kuogelea (swimming pool) ndani ya Hoteli ya Regency-Mikocheni jijini Dar ambapo kulikuwa na ‘bethidei’ ya Recho.
 
Awali, mastaa hao walianza kwa kulishana keki kwa staili ya njiwa (kwa mdomo), jambo lililoibua minong’ono mahali hapo.

Kama haitoshi, baada ya tukio hilo, wawili hao waliweka mapozi tata wakipiga picha zilizowaonesha nusu utupu huku vinguo walivyovaa vikiacha wazi sehemu kubwa ya maumbile yao nyeti.

0 comments: