HABARI MPYA: BAADA YA FREDRICK WEREMA KUJIUZULU, RAIS KIKWETE AMTEUA MWANASHERIA MPYA WA SERIKALI




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana George Mcheche Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Uteuzi wa Bwana Masaju ulianza jana, Ijumaa, Januari 2, 2015 na ataapishwa keshokutwa, Jumatatu, Januari 5, 2015, Ikulu, Dar Es Salaam.

Kabla ya uteuzi wake, Bwana Masaju alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Bwana Masaju pia amepata 

kuwa Mshauri wa Sheria wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

0 comments: