Man U yamsajili kipa wa Barcelona

Victor Valdes akisaini kuichezea Man U.

MANCHESTER, England  
KLABU ya Manchester United imethibitisha kumsajili kipa wa zamani wa Barcelona, Victor Valdes kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu.
Valdes mwenye umri wa miaka 32, alikuwa akifanya mazoezi na klabu hiyo tangu Oktoba, mwaka jana baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu akisumbuliwa na maumivu ya goti.
Valdes ameeleza kuwa amefurahishwa na usajili huo na yupo tayari kufanya kazi na kipa chaguo la kwanza la timu hiyo, David de Gea ambaye ni raia mwenzake wa Hispania.

0 comments: