KWA NINI BEI YA MAFUTA KWA WALAJI HAISHUKI KWA KASI? SOMA HAPA

0 comments

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe.
 
Kuanzia Mwezi Julai mwaka 2014 mpaka Desemba, bei ya mafuta ghafi imekuwa ikishuka kutoka $110 kwa pipa mpaka $56 kwa pipa. Mporomoko huu wa bei wa zaidi ya 40% haujaleta unafuu kwa mtumiaji wa kawaida wa mafuta ikiwemo wenye daladala na kupelekea nauli za usafiri wa umma kupungua.
Leo bado bei ya mafuta kwenye vituo vya mafuta ni tshs 2029 kwa Petroli na 1909 kwa dizeli, bei ambayo ni karibia ile ile kwa miezi michache iliyopita.
EWURA, inasemekana, wamesema kuwa bei za hapa nchini hushuka baada ya miezi 2 kwa sababu waagizaji huagiza kwa ujumla mafuta mengi zaidi na hivyo kutofaidika na punguzo la bei.
Hata hivyo bei zimeanza kushuka toka mwezi Julai na hatujashuhudia unafuu wowote kwa wananchi. Ingekuwa bei ya mafuta imepanda tungeona bei zimepanda mara moja na sababu za kununua ' bulky' huwa hazitolewi.
Ni kweli kwamba Tanzania hununua mafuta yaliyosafishwa na hivyo bei inayoshuka sio hiyo. Lakini hao wasafishaji hununua mafuta ghafi yenye bei ndogo hivi sasa kwa hiyo ni dhahiri lazima bei za pampu zipungue.
Vile vile ni kweli kwamba thamani ya shilingi ya Tanzania imeporomoka hivyo wananchi hawawezi kuona unafuu wa bei ya mafuta kwa sababu hununuliwa kwa fedha za kigeni na kuuzwa kwa Sarafu yetu. Hata hivyo kasi ya kushuka kwa bei ya mafuta ni 40% wakati shilingi imeshuka kwa chini ya 10%.
Katika hali ya kawaida na kwa kutumia mfumo wa kukokotoa bei wa EWURA, angalau bei ya mafuta ingeshuka kwa kati ya 15% and 25%.
Ni dhahiri mamlaka za nchi na hasa EWURA wanapaswa kueleza kwa umma ni Kwanini bei za mafuta hazishuki kulingana na bei ya bidhaa hiyo katika soko la Dunia.
Wananchi wana haki ya kujua na kama hakuna Maelezo basi bei hizo zishuke na wananchi wafaidike na punguzo hilo.
Zitto Kabwe, Mb


Read More »

Soma Hapa Mwigizaji Wastara Azungumzia Mahusiano Yake Na Bondi.

0 comments
WASTARANABONDI2
Kwenye friday nite live ya eatv, mwigizaji Wastara amezungumzia mahusiano yake na mwigizaji maarufu wa filamu Tanzania “Bondi” nakusema  “Nikiwa karibu na mwanaume yeyote sasa watu huzusha maneno ila mimi na Bondi tunafanya kazi pamoja tu, ni manager wangu na husimamia kazi zangu, siwezi kufanya kila kitu mwenyewe
Wastara yuko mbioni kuanza kufanya filamu mpya na kuanzia Januari 5 2014, atakuwa kambini.

Read More »

JOKATE: SIPENDI ‘SINI’ ZA KUTOMASWA! SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments
Mwanamitindo ambaye pia ni msanii wa filamu Bongo, Jokate Mwegelo.
Stori: Laurent Samatta
MWANAMITINDO ambaye pia ni msanii wa filamu Bongo, Jokate Mwegelo amesema kuwa hapendi kuigiza sini za mapenzi hasa zile anazotakiwa kushikwashikwa na mwanaume hasa asiyemjua.
Jokate alifunguka hayo wakati paparazi wetu alipotaka kujua namna ambavyo wazazi na mpenzi wake wanavyolipokea suala la yeye kuigiza sini za kushikwashikwa na wanaume tofauti katika filamu ndipo alipofunguka kuwa suala hilo limekuwa likipigwa vita na wazazi wake lakini analazimika kufanya kwa sababu ndiyo kazi aliyoichagua.
Jokate Mwegelo akipozi.
“Wazazi wangu wanachukia sana jambo hili na huwa wanasema bora niache filamu, hata mimi mwenyewe huwa sipendi ila huwa navumilia kwa kuwa ni kazi, sina jinsi,” alisema Jokate.

Read More »

Avril,Collabo Na Ommy Dimpoz Inakuja Soon.

0 comments

avril 3
Nikimuona ndio single ya mwisho kutoka kwa Avril iliyotoka 2014 na kufanya vizuri kwenye radio na tv nje na ndani ya Kenya. Kupitia instagram yake Avril ametufahamisha kuwa kazi mpya aliyofanya na Ommy Dimpoz inakuja Soon.
avril 1 avril 2

Read More »

NDOA YA LULU YABUMA:ADAI ANAETAKA KUMUOA AWE NA SIFA HIZI...SOMA SIRI HIYO HAPA IKO HAPA

0 comments

Mwigizaji wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’. 

BAADA ya kuwa na malengo ya kuolewa mwaka 2014, mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameibuka na kusema imeshindikana lakini hajilaumu wala hamlaumu mtu yeyote kwa kutotimiza suala hilo kwani anaamini Mungu ndiye anayewezesha kila kitu.
Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Lulu alisema mwaka 2014 alikuwa na malengo mengi likiwemo suala la ndoa lakini kwa kuwa Mungu ndiye muweza, atapanga upya suala hilo na anaamini litakuja kutimia.
“Ndoa ni mipango ya Mungu, huwezi kulazimisha hata siku moja, sisi wanadamu huwa tuna mipango yetu lakini ili ifanikiwe lazima kuwe na baraka za Mungu,” alisema Lulu.

Akizidi kupiga stori na paparazi wetu, Lulu alisema kwa mwaka huu na mwakani hawezi kuweka malengo ya ndoa kwani bado kuna mambo yake hajayaweka sawa hivyo suala la kuolewa ataliweka hadharani baada ya miaka miwili ijayo.
‘Lulu’ akipozi.

“Sina mpango hata kidogo kwa mwaka huu wala mwakani labda baada ya hii miaka kupita ndiyo ninaweza kupanga tena suala la ndoa,” alisema Lulu.

Alipotakiwa kumtaja mpenzi aliyenaye kwa sasa, Lulu aligoma kufunguka lakini akakubali kuanika siri za mwanaume anayetaka kuwa mumewe.
“Kwanza nahitaji mwanaume atakayenielewa kwa kila kitu, pia awe na mapenzi ya kweli na atakayeniangalia kama Lulu na siyo kama Elizabeth pekee. Anapaswa kutambua na kusapoti kazi zangu za sanaa,” alisema Lulu.
Kuhusu mikakati yake ya sanaa mwaka huu, Lulu alisema ana mpango wa kuendelea na masomo huku akiwa pia na ‘project’ kubwa mbili ambazo anatarajia kuzifanya.
“Nina project kubwa mbili mwaka huu, muda utakapofika kila mmoja atazijua maana nitaziweka wazi,” alisema Lulu.

Read More »

BAADA YA NIKKI MBISHI KUTANGAZA KUACHA MUZIKI, HAYA NDIO MANENO YA CHID BENZ

0 comments

.
.
Baada ya msanii wa Hip Hop Nikki Mbishi aka Baba Malcom kutangaza kuwa ameacha kufanya kazi ya muziki sasa Chid Benz amekanusha taarifa hizo na kusema kuwa ameshafanya mazungumzo na msanii huyo  na kumtaka asichukue uamuzi huo mapema kwani hata yeye amepitia katika changamoto hizo.
Chid Benz alichukua nafasi hiyo kuwataarifu mashabiki wa muziki kupitia ukurasa wa facebook na kuandika ‘Nakanusha habari za Nikki mbishi kuacha mziki,nimeongea nae kama kaka na kumgusia mengi,najua amenielewa na nimemwambia asikubali wale wanaomkubali waanze kukubali wengine.mimi nimekumbana na vingi na watu weengi waliaminishwa kama nimeshushwa kimziki,jimefanyiwa mengi ambayo kwa muda ule nsingeweza kuelezea kila mtu nini kinaendelea,so if kikitokea kibaya kinatangazwa mpk kwenye taarifa za habari mbona mziki hauchezwi?ningekua sina nguvu hio nisingesumbua watu kuniweka front page..but bado nipo na nimekomaa.na naishi na naona wanaopewa kipaumbele na najua bado mimi ni mimi.Iron
.

Read More »

ALICHOKIANDIKA TUNDU LISU KABLA YA WALE VIJANA WATATU KUTOKA GEITA KUKAMATWA NA POLISI

0 comments


  

Kuna vijana watatu kutoka mkoani Geita,
wanakuja kwa mguu kuja kuonana na rais
Kikwete ikulu, ili kueleza kero zao kuhusu nchi
yao, je? watakaribishwa ikulu? au wataitwa
wahuni na wavuta bangi? nakumbuka rais
amewahi kuwakaribisha watu wengi ikulu kama
Ray c, Diamond, mzee yusufu, n.k, ambao ni
waimbaji majukwaani, wala sio watetezi wa
wanyonge, wengine ni wala madawa ya kulevya
tu, mh. Rais wanakuja hao vijana watatu kutoka
Geita nakushauri uwapokee, otherwise
utaonekana una upendeleo kwa kuwakaribisha
watu unaowataka wakati ikulu sio mali yako. 

Read More »

BREAKING NEWS: MMILIKI WA VIP ENGINERING RUGEMALIRA AMEFUNGUA KESI MAHAKAMA KUU AKIIDAI SERIKALI BILION SH. 398

0 comments


Mmiliki wa VIP Enginering, aliyekuwa anamiliki hisa IPTL Ndugu Rugemalira amefungua kesi mahakama kuu akiidai serikali jumla ya Sh. 398 bilion zilizokuwemo/zinazotakiwa kuwemo katika Escrow Account ya Tegete na zilizolipwa kwa kampuni ya PAP na kuleta mjafala mkubwa bungeni.

Katika madai yake, mwenye hisa hatambui malipo yote yaliyolipwa na serikali kwa kampuni ya PAP kwani kampuni hiyo haikuwa na nyaraka halali kutoka kwa msajili wa makampuni BRELA, Taxe Clearance Certificate kutoka TRA, kuandikishwa Tanzania Investment Center na wala mmliki wake kuwa na vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini kutoka idara ya Uamiaji.

Katika hoja yake mdai anasema kuwa ni jukumu la serikali kuwahakiki wawekezaji wa nje ili kuwalinda wawekezaji wa ndani pindi tu wanapoingia ubia na wawekezaji wa nje.

Ameendelea kudai kuwa, kwa uzembe huo wa serika kwa kutotimiza uhakiki wake wa kigeni ulisabibisha kampuni yake ya VIP Engineering kuingia ubia na Kampuni Feki na kumsababishia hasara ya sh. Bilion 56 kwani alizimika kuvunja ubia wao na kumfungulia mashitaka mbia mwenza PAP baada ya kugundua ubabahishaji wa uhalali wa kampuni hiyo. Hivyo ameitaka tena serikali kulipa gharama zote alizotumia kuendesha kesi sh.36.8 bilion.

Aidha amedai kuwa aliwafahamisha serikali kutolipa malipo yoyote yaliyokuwemo kwenye account ya Escrow na endapo serikal ingeona kuna haja ya kufanya hivyo basi ilipe kwa VIP au IPTL account ambayo yeye alikuwa signatory.

Katika uwasilishaji wake mahakamani hapo anadai kutofahamu au kutambua kulipwa kwa PAP. Hivyo serikali inatakiwa kulipa tena madai yote kwa VIP au IPTL. Amewapa serikali siku 14 tu toka 1 Januari,2015 kuwa wamelipa malipo yote.

Katika madai hayo, ili kuyadhitisha ameambatinisha :
1. Report ya Mkaguzi mkuu wa hesabu za serika inayodhibitisha baadhi ya pesa kulipwa kwa PAP
2. Mkaguzi mkuu kudhibitisha kuwa mlipwaji hajawahi kusajiliwa kama mlipa kodi wala kupewa Taxe clearance certificate.
3. Report ya mdhibi mkuu wa Rushwa kuthibitisha kuwa kampuni iliyolipwa haikusajiliwa BRELLA na wala haikuwa na sifa au uhalali kufanya kazi yoyote ya ugavi dhidi ya Shirika lolote la Uma.
3. Report ya Bunge kama muhimili mwingine wa nchi kupitia kamati yake ya hesabu za serikali na mashirika ya uma kutodhibitisha/kudhibitisha juu uhalali wa PAP, mmiliki wa kampuni ya PAP na utendaji wake wa kazi.
4. Mapendekezo ya kamati ya bunge kwa serikali dhid ya PAP, mali zake na mmiliki wake.
5. Mapendekezo ya bunge kwa serikali yanayodhibitisha kuwa PAP haikuwa halali.
6. Mapendezo ya bunge kwa serikali juu ya watendaji wote walioshilikiana kwa pamoja ya kuilipa kampuni isiyo halali.
7. Baadhi ya magazeti likiwemo gazeti la serikal kudhibitisha mkuu wa nchi kupokea na kuridhia mapendezo hayo.
8. Magazeti pamoja na la serikali kudhibitisha serikali kwa kuwaadhibu watendaji wote waluofanya udhembe wa kulipa kampuni isiyo halali.
9. Mkanda wa video ya Rais wa nchi katika hotuba yake kukili watendaji wake kuilipa kampuni isiyo halali na kawasimamisha kazi kwa uzembe huo.
10. Barua ya Mwanasheria mkuu wa serikali kwa Rais ya kuomba kujiuzuru kwa kufanya uzembe huo wa kulipa kampuni isiyo halali.
11. Barua ya Rais kwa Mwanasheria mkuu kukubali kujiuzuru kwake kwa kutoa ushahuri wa kulipa kampuni isiyo halali.
Kesi hiyo uenda ikaamsha tena hisia za wananchi juu ya malipo ya Escrow account. Ni mtihani mwingine kwa serikali kwani Bunge na wanachi hawako tayari kuona pesa kama hiyo ikilipwa tena.

Read More »

KIONGOZI WA CHADEMA ASIMAMISHWA KAZI..MWINGINE APEWA ONYO KALI

0 comments

Naibu Katibu Mkuu  CHADEMA  Zanzibar,  Salum  Mwalimu akiutubia mkutano wa hazara  mjini  Nansio Wilaya ya  Ukerewe, Mwanza lengo kushukulu wananchi kwa kukipatia ushindi katika uchaguzi wa Serikali  za  mitaa uliopita. Wilaya  hiyo Chadema imepata  viti 47 vya Serikali za vijiji huku ccm  ikipata 27 na CUF viwili.
Ukerewe. Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu amemsimamisha kazi mjumbe wa kamati ya utendaji ya chama hicho Wilaya ya Ukerewe, Wilbrod Machemli kwa kushindwa kutimiza wajibu wake, ikiwa ni pamoja na kutotangaza ujio wa kiongozi huyo.
Rungu hilo pia limemkuta katibu wa Chadema wilaya hiyo, Libelatus Mlebele ambaye amepewa onyo kali.
Akizungumzia hatua hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Nansio jana, Mwalimu ambaye ameanza ziara mkoani hapa juzi kwa lengo la kuwashukuru wananchi baada ya kukichagua chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, alisema hakuridhishwa na maandalizi yaliyofanywa na viongozi hao.
Kutokana na hali hiyo, Mwalimu alimwagiza Mwenyekiti wa wilaya wa chama hicho, Jacobo Munyaga kwa gharama zake amwandalie mkutano mwingine kabla ya mwisho wa mwezi ujao.
Mwalimu pia alitilia shaka matumizi ya fedha yaliyotajwa kutumika kutangaza uwepo wa mkutano wake.
Alisema Chadema hakipo tayari kulinda viongozi wazembe na wasiowajibika na kuwaonya wajumbe wa kamati tendaji hasa katibu ambaye bado yupo katika uangalizi wa miezi sita kwa maelezo kuwa anaweza kuondolewa kazini.
Kabla ya kuchukua uamuzi huo, Mwalimu aliwaita mbele wakazi wanne wa kata za Kakerege, Nansio, Nakatungulu na Kagera ambao walikiri kutosikia matangazo ya ujio wake.
Hatua hiyo aliichukua baada ya kuwasili katika Uwanja wa Mongera wa mjini Nansio saa 9:30 alasiri huku kukiwa na idadi ndogo ya watu ikilinganishwa na ziara zake za nyuma.
Mbali na hilo, pia Mwalimu ametumia mkutano huo kukemea matumizi mabaya ya fedha za serikali yanayofanywa na viongozi waandamizi wakati huduma za kijamii zikizidi kuwa mbaya.
Alisema ziara za mara kwa mara za nje ya nchi zisizo za lazima zinazofanywa na Rais Jakaya Kikwete pamoja na viongozi wengine hazina tija kwa taifa.
Naye mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, Joseph Mkundi akizungumza katika mkutano huo, alisema katika katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wao wamepata mafanikio makubwa.
Alisema mbali na kusimamia vyema matumizi ya fedha za serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, pia halmashauri hiyo imekamilisha mipango ya kununua greda moja la kutengeneza barabara lenye thamani ya Sh400 milioni hivi karibuni chama hiko kimeluwa kikipigania kukishinikiza serikali kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi.
Hata hivyo, alisema mbali ya halmashauri hiyo kupata hati safi ya matumizi ya fedha za umma pia hivi karibuni huko jijini Nairobi Kenya, Halmashauri hiyo ilipata tuzo ya kukidhi vigezo vya sheria ya ununuzi ya umma kati ya wilaya 166 za nchi nzima.


chanzo: gazeti la mwananchi

Read More »

ATANGAZA KUUZA FIGO KWA SH90 MILION SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments

Mkazi wa Morogoro, Andrew Germanis Chimulimuli ametangaza kuingiza sokoni figo yake ambayo amesema anaiuza Sh90 milioni ili kukabiliana na ugumu wa maisha.
Chimulimuli aliyefunga safari kutoka Ifakara, Morogoro hadi jijini Dar es Salaam ili kufanya biashara hiyo alisema ameamua kutoa kiungo chake hicho muhimu kutokana na ugumu wa maisha unaomkabili.
“Nimeamua kujitolea nafsi yangu ili niisaidie familia yangu, kwa sababu mimi si kitu kama sina fedha, ndiyo maana nimejitolea kutoa figo yangu nipate fedha,” alisema Chimulimuli.
Chimulimuli alisema anataka kuiuza figo hiyo kwa gharama ya Sh90 milioni ingawa alikubali kufanya mazungumzo ya kupunguza bei pindi atakapopatikana mteja.
Takwimu za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii zinaeleza kuwa kuna wagonjwa 470,000 nchini ambao figo zao zimeshindwa kufanya kazi kabisa na wanahitaji upandikizaji.
Ingawa uamuzi wa Chimulimuli unaweza kuwa msaada kwa Watanzania wenye mahitaji, lakini kimaadili ya afya na kisheria, jambo hilo linakatazwa kufanywa kiholela hadi pale linapofuata taratibu.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Figo Tanzania, Jaji Frederick Werema aliwahi kuliambia gazeti hili kwamba anashangazwa na hatua za baadhi ya watu kuchukua uamuzi wa kuuza figo kwa ajili ya kujipatia fedha.
“Kutoa figo ni kosa la jinai, lakini siyo hivyo tu, kutoa figo ni lazima ufuate taratibu za kisheria na za kitabibu,” alisema Jaji Werema miezi kadhaa iliyopita.
Biashara ya figo
Aprili mwaka jana, gazeti hili lilifanya uchunguzi na kubaini kuwa wapo Watanzania wanaouza figo zao kiholela kwa ajili ya kujipatia fedha.
Gazeti hili liliwasiliana na vijana kadhaa ambao kwa nyakati tofauti walikubali kuwa wanauza figo zao na baadhi wakieleza kuwa tayari walishauza kwa gharama za kati ya Sh50 milioni hadi Sh80 milioni.


Chimulimuli alisema kutokana na ugumu wa maisha, kipato chake kimekuwa kigumu sana na hakiwezi kukidhi mahitaji ya familia.
“Mtu akikuona kwa nje anaweza kukuona kama upo sawa na una maisha mazuri lakini ukweli ni kuwa nina maisha magumu sana,” alisema. Kuhusu hatima yake kiafya, alisema yeye ni msafiri na hawezi kuishi milele na hivyo bora auze figo yake iwe msaada kwa wengine wenye mahitaji.
“Ni bora nifanye kitu cha halali kinachoigharimu afya yangu mwenyewe badala ya kuiba au kufanya uhalifu mwingine,” alisema Chimulimuli.
Uchangiaji wa figo
Daktari bingwa wa figo katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Linda Ezekiel alisema uchangiaji wa figo ni mchakato mrefu na si suala la fedha tu.
Dk Ezekiel alisema mchakato wa kuchangia figo ni mrefu kwani mchangiaji hutakiwa kuwa na kundi la damu linalofanana na mgonjwa.
Alisema vipimo vya afya hufanyika ambapo maradhi yanayoweza kuambukiza kama homa ya ini, magonjwa ya zinaa na Virusi vya Ukimwi, navyo huangaliwa kwa umakini mkubwa.
“Ni lazima tuhakikishe mtu ameridhia kabisa kufanya hivyo na katika hali hiyo ni lazima tumfanyie mtu ushauri wa kisaikolojia na afahamu hatua za utoaji huo sambamba na madhara anayoweza kuyapata,” alisema.
Kuhusu changamoto ya maradhi hayo Dk Ezekiel alisema kusafisha figo ‘dialysis’ ni gharama kubwa ambapo kwa tiba moja mgonjwa hutakiwa kulipa Sh300,000 na tiba hiyo hufanywa angalau mara tatu kwa wiki.
Hata hivyo Dk Ezekiel alisema kwa anayechangia figo na kubaki na moja hawezi kupata madhara kiafya kwani figo moja ina uwezo mkubwa wa kufanya kazi zake.

Read More »

SAKATA LA ESCROW: KAFULILA AJIPANGA KUPELEKA HOJA BINAFSI KUMNG'OA PINDA SOMA HAPA

0 comments

SASA kuna kila dalili kuwa mwangwi wa kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow iliyotikisa mkutano wa 16 na 17 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, utaendelea kusikika kwa namna ya kuishinikiza Serikali kuwajibika zaidi.
 
Dalili hizi zimeonyeshwa waziwazi na baadhi ya wabunge hususani waliokuwa vinara wa kupambana na kashfa hiyo ambao hawajaridhishwa na hatua zilizochukuliwa na Rais Jakaya Kikwete dhidi ya watendaji wa Serikali na viongozi wa kisiasa walioguswa na ripoti ya uchunguzi wa kashfa hiyo.
 
Mmoja wa wabunge walio katika mkakati huo ambao kimsingi unalenga kumng’oa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ni David Kafulila wa Kigoma Kusini.
 
Kafulila katika mahojiano yake na waandishi wa habari alisema hatua zilizochukuliwa na Rais Kikwete kushughulikia maazimio nane ya Bunge haziridhishi na kuongeza kuwa kabla ya kuketi kwa mkutano wa 18 wa Bunge anapaswa kuwa amemfukuza kazi Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
 
Alisema Waziri Muhongo ni muhusika muhimu katika kashfa hiyo, kwa sababu alidiriki kusimama bungeni na kulidanganya taifa kuwa fedha zilizokuwa zimehifadhiwa katika Akaunti ya Tegeta Escrow hazikuwa za umma hadi uchunguzi wa vyombo vya dola ulipothibitisha pasipo shaka kuwa ni za umma.
 
“Hatufanyi haya kwa lengo la kumkomoa mtu, hapana kabisa. Sisi tuna dhamira ya dhati ya kutetea maslahi ya taifa kwa hiyo hatuko tayari kumuona Rais akiendelea kumuacha kiporo Waziri Muhongo.
 
“Rais anaonekana kusuasua kuchukua uamuzi dhidi ya Waziri Muhongo, sasa kama itatokea akashindwa kutengua uteuzi wake hadi Bunge lijalo tutawasilisha hoja binafsi ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu tukiwa na kusudio la kumng’oa kwenye wadhifa wake, hiyo ndiyo njia pekee ya kumwondoa Waziri Muhongo,” alisema Kafulila.
 
Alipoulizwa iwapo mkakati huo wa kumng’oa Waziri Mkuu Pinda unaungwa mkono pia na wabunge wa CCM, alisema hawezi kuzungumzia msimamo wa wanasiasa wengine hata hivyo, ujasiri waliouonyesha baadhi ya wabunge wa chama hicho wakati wa mjadala uliopitisha maazimio ya Bunge unaondoa shaka ya kupata uungwaji mkono wa kutosha.
 
Mbali na Kafulila, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge wa Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe, alipoulizwa msimamo wake kuhusu jambo hilo, akiandika kwa maandishi kupitia barua pepe alisema anaamini Serikali itatekeleza maazimio yote ya Bunge.
 
Ingawa tayari Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue amekwishamsimamisha kazi Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, kupisha uchunguzi dhidi yake kwa kashfa ya Escrow, bado yapo mashinikizo yanayotaka hatua zaidi zichukuliwa kwa mujibu wa maazimio nane ya Bunge.
 
Mbali na Katibu Mkuu Sefue, Jaji Mkuu Othaman Chande bado yuko kimya kuhusu majaji wa Mahakama Kuu walioguswa katika kashfa hiyo.
 
Awali viongozi wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kwa nyakati tofauti walikaririwa na vyombo vya habari wakitoa matamshi yenye mwelekeo wa kulishinikiza Bunge kuiwajibisha Serikali iwapo Rais Kikwete hatatekeleza maazimio yote nane ya Bunge.
 
Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba, ndiye aliyekaririwa kwanza akieleza kuwa endapo Rais Kikwete atashindwa kumwajibisha Prof. Muhongo, wabunge walio ndani ya Ukawa watawasilisha hoja na kushawishi wengine kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu sambamba na kuitisha maandamano nchi nzima.


Wakati shinikizo hili likizidi kushika kasi, Rais Kikwete katika hotuba yake ya kufunga mwaka aliendelea kusisitiza msimamo wake wa kumuweka kiporo Prof. Muhongo kwa maelezo kuwa uchunguzi dhidi yake haujakamilika.

Read More »

HABARI MPYA: BAADA YA FREDRICK WEREMA KUJIUZULU, RAIS KIKWETE AMTEUA MWANASHERIA MPYA WA SERIKALI

0 comments



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana George Mcheche Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Uteuzi wa Bwana Masaju ulianza jana, Ijumaa, Januari 2, 2015 na ataapishwa keshokutwa, Jumatatu, Januari 5, 2015, Ikulu, Dar Es Salaam.

Kabla ya uteuzi wake, Bwana Masaju alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Bwana Masaju pia amepata 

kuwa Mshauri wa Sheria wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Read More »

MKURUGENZI WA HALMASHAURI IRAMBA SINGIDA ALIPUKIWA NA BOMU, POLISI WATHIBITISHA..JWTZ WAINGIA KAZINI

0 comments

Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Iramba Singida, Halima Mpitaamenusurika kifo baada ya kulipukiwa na kitu ambacho kinadhaniwa kuwa bomu la kutengenezwa kienyeji.

Kamanda wa Polisi Singida, Thobias Sidoyeka amethibitisha kutokea kwa tukio hilo nyumbani kwa Mkurugenzi huyo wakati akijiandaa kwenda kazini, mlipuko huo ulitoka kwenye bahasha ambayo aliipokea juzi kutoka kwa Katibu Muhtasi wake.

Ndani ya bahasha hiyo kulikuwa na ujumbe “Poleni sana, hatuwezi kufanya dili la milioni 90 halafu mkala peke yenu, sisi mkatudhulumu tukawaacha”, baada ya kuisoma alienda nayo nyumbani bila kujua kama kuna kitu kingine ndani.

Wakati akijiandaa kwenda kazini siku ya jana ndipo mlipuko huo ulipotokea, hakuna aliyekamatwa ila Polisi wanaendelea na upelelezi wakishirikiana na JWTZ ili kubaini kama mlipuko huo ulitokana na bomu.

Read More »

VURUGU KUBWA YATOKEA MAKABURINI SHINYANGA, NDUGU WAPASUA MWILI WA MAREHEMU! SOMA HAPA

0 comments

Habari tulizozipata hivi punde zinasema kuwa kumetokea vurugu za aina yake katika makaburi ya Masekelo katika manispaa ya Shinyanga wakati wa mazishi ya mwanamke mmoja aitwaye Benadetha Steven(35) aliyekuwa anaishi katika mtaa wa Mapinduzi maarufu mtaa wa Juma Matv katika kata ya Ndala aliyefariki dunia juzi wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga.

Tukio hili limetokea mchana huu wakati wa mazishi ya mwanamke huyo anayedaiwa kufariki dunia kutokana na uvimbe wa tumboni uliokuwa unamsumbua hivyo ndugu wa marehemu kuamua kumfanyia mambo ya kimila ili kuondoa mkosi katika ukoo wao.

Habari zinasema kuwa ndugu wa mwanamke huyo anayetokea Musoma (Mkurya) walikuwa wanataka ndugu yao apasuliwe tumbo wafanye mambo ya kimila makaburini lakini uongozi wa eneo husika wakasema utaratibu huo ungefanyika hospitalini badala ya hadharani watu wakishuhudia.

 Tunaambiwa kuwa mwanamke huyo alikuwa ameolewa Shinyanga na alipofariki mwili wake ulihifadhiwa katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga.

Mgogoro huo ulianzia nyumbani kabla ya kwenda makaburini,ndugu walitulia na wakati mazishi yanaendelea ndipo ndugu wa marehemu wakaingia kaburini kuzuia wananzengo wasitupie udongo makaburini.

"Mchungaji alipomaliza ibada ya mazishi akaruhusu mwili uzikwe,wananzengo wakaanza kutupia udongo,ghafla ndugu wa marehemu wakaingia kaburini na kuzuia wananzengo,wakatoa mwili wakauchana kwa wembe,wakachinja kuku,wakamwagia damu mwili wa marehemu na kumwingiza kwenye tumbo la marehemu huyo kuku,kisha wakaaanza kuzika upya", shuhuda aitwaye Sijali Jumanne alisema.

"Kitendo cha ndugu kung'ang'ania kufanya mambo yao,kiliwakera wananchi wakaamua kutoka makaburini,na jeshi la polisi limefika eneo la tukio na kuwakamata ndugu wote wa marehemu",aliongeza shuhuda huyo.

Read More »

PANYA ROAD 36 WATIWA MIKONONI MWA JESHI LA POLISI BAADA YA KUFANYA FUJO JIJINI NA KUZUA TAHARUKI.

0 comments
Jeshi la polisi nchini linawashikilia vijana 36 wa kundi maarufu Panya Road wanaodaiwa kufanya vurugu na kupora mali za watu na kusababisha taharuki katika jiji la Dar es salaam huku baadhi ya wananchi wakitoa maoni tofauti kuhusiana na tukio hilo.
Akitoa ufafanuzi wa taharuki hiyo msemaji wa jeshi la polisi SSP ADVERA BULIMBA ambaye mbali na kuwatoa hofu wananchi kuwa hali hiyo haitajitokeza tena amesema jeshi hilo limejipanga vizuri kukabiliana na vikundi vyovyote vinavyotaka kuvuruga amani ya nchi na kwamba endapo polisi wasingewadhibiti vijana hao mapema tangu wakiwa makaburini baada ya kumzika mwenzao aliyeuwawa na wananchi baada ya kuiba hali ingekuwa mbaya zadi.
 
Kufuatia tukio hilo paparazi imezunguka maeneo mbalimbali ya jiji yaliyodaiwa kukumbwa na tafrani hiyo ambapo baadhi ya wananchi wa maeneo ya magomeni ambako vurugu zilianzia wameelezea namna zilivyoanza hadi kusababisha watu kuanza kukimbia hovyo na wengine kuacha maduka yao wazi  na taarifa kusambaa maeneo mengine.
 
Katika maeneo ya mwananyamala na ubungo baadhi ya waliozungumzia sakata hilo wameitaka serikali kuangalia makundi ya vijana na ikiwezekana wapatiwe elimu ya ujasiriamali bure ili waweze kuendesha maisha huku wengine wakishauri vijana wasiokuwa na kazi mitaani wapelekwe jeshini wakafundishwe stadi za kazi pamoja na uzalendo ili kuepuka vitendo hivyo.
 
Taharuki hiyo ilitokea usiku wa tarehe mbili chanzo kikiwa ni kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la MOHAMED AYUB kuuwawa na wananchi tarehe mosi mwaka huu katika maeneo ya tandale kwa mtogole kwa tuhuma za wizi ambapo tarehe 2 maziko yalifanyika na taarifa zilizolifikia jeshi la polisi zilidai kuwa baada ya maziko vijana wenzake walijipanga kufanya fujo ili kulipiza kisasi.

Read More »

TAZAMA PICHA ZA DIAMOND PLATNUMZ ALIVYOWAPAGAWISHA MASHABIKI WAKE WA RWANDA SIKU YA MWAKA MPYA INGIA HAPA

0 comments

Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa amebebwa na wacheza shoo wake siku ya mwaka mpya Kigali, Rwanda.

Diamond Platnumz akifanya yake.
Nyomi ya kufa mtu waliofika siku ya shoo hiyo.
Akifanya yake na wacheza shoo wake.
Mfanyabiashara mrembo na muimbaji wa Uganda, Zarinah Hassan 'Zari'  au 'The Boss Lady' mpenzi mpya wa Diamond Platnumz akiwa katika pozi.
Muonekano wa siku ya shoo hiyo.
Diamond Platnumz (katikati) akifanya yake akiwa na Yamoto Bendi.

Read More »

PANYA ROAD WATIKISA JIJI LA DAR

0 comments




Kikundi kinachodaiwa kuwa Panya Road wametikisa maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam na kupora vitu, kujeruhi watu wakiwa na mapanga mikononi mwao maeneo ya Sinza, Tandale, Mwananyamala na maeneo mengineyo usiku wa leo. Maduka na baa zimefungwa na kupelekea polisi kupiga risasi hewani kuwatawanya watu waliokuwa wamekaa kimakundimakundi.
Fujo zaidi zilianzia mchana leo wakati kiongozi wao aitwaye Diamond alipouawa maeneo ya mpakani mwa Tandale na Mwananyamala darajani usiku wa kuamkia mwaka mpya kwa kukatwakatwa na mapanga.
Baada ya kumzika mwenzao leo wakajipanga kwa ajili ya kufanya fujo. Kilichotokea, polisi walikuwa eneo hilo tena ndani ya difenda kwa ajili ya kuhakikisha kuna amani wakati wa maziko.
Maziko yalipokwisha, vijana hao wakatawanyika, ila baadae wakaanza kujikusanya na kuanza kuleta fujo tena baada ya kuhakikisha kwamba polisi wameondoka.

Read More »

JOKATE: DIAMOND HANA AKILI TIMAMU SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments

Staa wa urembo, muziki, filamu na ujasiriamali Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ au ‘Jojo’ amemrushia maneno makali aliyewahi kuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuwa hana akili timamu kufuatia maneno aliyotoa kuwa enzi za uhusiano wao, eti mwanadada huyo alikuwa akichenga kumzalia mtoto.
Staa wa urembo, muziki, filamu na ujasiriamali Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ au ‘Jojo’.
MAHOJIANO
Katika mahojiano maalum ya hivi karibuni kupitia Kipindi cha Mtu Kati cha Runinga ya GlobalTV Online chenye makao yake makuu ndani ya Ofisi za Global Publishers zilizopo Bamaga-Mwenge, Dar, Diamond alitoa madai kuwa, amekuwa akihaha kupata mtoto.
Alisema kwamba, katika harakati zake hizo, warembo ambao alishatoka nao kimapenzi akiwemo Jokate walikuwa wakimchezea mchezo mchafu ili wasimzalie kwa kuwa alikuwa akiwaambia anahitaji mtoto kwa udi na uvumba.
MZOZO MKUBWA
Hata hivyo, madai hayo ya Diamond yalizua mzozo mkubwa kwenye mitandao ya kijamii huku warembo hao wakipigwa za uso hivyo kutafuta namna ya kujitetea.“Hao akina…(wanatajwa warembo wa Diamond) watakuwa wana matatizo ya uzazi siyo bure.
“Ndiyo maana Dangote (Diamond) ameona bora aende kwa Zari (msanii wa Uganda, Zarinah Hassan) ambaye tayari ana mwanga wa kuzaa (ana watoto watatu),” ilisomeka sehemu ya maoni juu ya madai hayo ya Diamond kwenye Mtandao wa Instagram.
Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ akiwa na Diamond.
SIKIA MADAI YA DIAMOND
Diamond alifunguka: “Jokate na Wema (Sepetu) nilitamani sana wanizalie lakini walikuwa wakichengachenga, mambo mengine ujue si ya kuzungumza lakini inauma.”
JOKATE AJIBU MAPIGO
Kufuatia tuhuma hizo nzito huku kukiwa na madai pia, kwamba Jokate aliwahi kupigwa mimba ‘akaipanchi’, mwanadada huyo alipotafutwa na mwandishi wetu kujibu ‘shitaka’ linalomkabili alianza kwa kumshangaa staa huyo wa Ngoma ya Ntampata Wapi inayokimbiza kwa sasa.
Jokate alisema anamshangaa Diamond kuyazungumza maneno hayo hadharani na inaonesha asivyokuwa na akili timamu au ambayo haijakomaa.
JOJO ASHUKA NA MISTARI
“Diamond atuache, kila siku anatuzungumzia, hana akili timamu.
“Inadhihirisha kweli hana akili kwa kuwa mtu mwenye akili zake timamu hawezi kwenda kwenye chombo cha habari na kueleza hayo aliyoyasema,” alisema Jokate akionesha kukasirishwa na maneno ya Diamond.
Wema akiwa na Diamond.
WEMA HATAKI MALUMBANO
Ukiacha Jokate na Wema ambaye naye aliwekwa kwenye kapu moja la kuchenga kumzalia, hakutaka kumjibu Diamond kwa kuwa hataki malumbano au makuu na mtu.
PENNY ALISHAJIBU
Pia jamaa huyo alimzungumzia aliyekuwa mwandani wake mwingine, Penniel Mwingilwa ‘Penny’ kuwa yeye alitoa mimba zake mbili kwa visingio tofauti.Katika majibu yake kupitia gazeti tumbo moja na hili, Risasi Jumamosi, toleo la wiki iliyopita, Penny alisema kuwa Diamond awe mkweli na aseme tatizo lake kwani anavyojua yeye hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba.
NENO LA MHARIRI
Baada ya kila mmoja kupata nafasi ya kufunguka kivyake, ni vyema sasa malumbano yakaisha na kuuanza mwaka 2015 kwa kuchapa kazi ili kujiletea maendeleo binafsi na taifa kwa jumla.

Read More »

ASKOFU AELEZA ALIVYOINGIZIWA MAMILIONI YA ESCROW INGIA HAPA KUPATA HABARI KAMILI

0 comments
Askofu Nzigilwa
Ziliwekwa akaunti binafsi, adai ni za kanisa
 Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Eusebius Nzigilwa, amevunja ukimya kuhusu mgao wa Sh. milioni 40 alioupata kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya VIP Engineering & Marketing Limited, James Rugemalira.

Ukimya wa Askofu Nzigilwa unatokana na sakata la uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 300 kutoka akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Akaunti hiyo ilifunguliwa baada ya waliokuwa wanahisa wa Kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ikiwamo VIP kuingia katika mgogoro na Shirika la Umeme nchini (Tanesco).
Taarifa kwa vyombo vya habari jana ilisema fedha alizopewa Askofu Nzigilwa na Rugemalira, zilikuwa za matoleo kwa ajili ya maendeleo ya Kanisa.
Alisema kiutaratibu siyo vibaya kwa waumini kutoa michango na matoleo kwa Kanisa na watumishi wake.
Katika taarifa hiyo ambayo Askofu Nzingilwa alipotafutwa alithibitisha kwamba ni yake, alifafanua kuwa alifahamiana na familia ya Rugemalira tangu akiwa Paroko Msaidizi wa Parokia ya Makongo Juu, Dar es Salaam na hata baada ya kuteuliwa kuwa Askofu Msaidizi wameendelea kushirikiana na kuwasiliana katika masuala mbalimbali ya kikanisa na kijamii.
“Samahani nipo kwenye kazi fulani hatuwezi kuongea kwa sasa. Ni kweli kuna taarifa nimeitoa leo kwa Tumaini Media na nimewaambia waitume pia kwa vyombo vingine vya habari,” alisema Askofu Nzingilwa alipowasiliana na NIPASHE kwa kutumiwa ujumbe mfupi wa maneno (sms).
Askofu Nzingilwa katika taarifa hiyo aliyoisaini juzi, alisema mwanzoni mwa Februari 2014, Rugemalira alimuomba namba ya akaunti yake ya benki ya Mkombozi ili aweke matoleo yake.
Alisema aliombwa akaunti yake na Rugemalira mapema Februari, mwaka jana na kwamba hakuwahi kufahamu kiasi cha fedha kilichowekwa kwenye akaunti yake hadi alipoangalia taarifa ya benki Februari 27, mwaka jana iliyoonyesha aliingiziwa Sh. milioni 40.4.
“Niliwasiliana na Rugemalira na kumwambia nimeona kiasi kikubwa cha fedha katika akaunti yangu, naye akaniambia hayo ni matoleo yake ambayo anaamini yatasaidia katika shughuli zetu za kitume na kichungaji. Nikamshukuru kwa ukarimu huo mkubwa,” alibainisha Askofu huyo.
Alisema matoleo hayo yalipokelewa kwa moyo mnyofu kutoka kwa mtu anayefahamika kwa ukarimu wake katika kusaidia Kanisa na watumishi wake.
“Kampuni anazomiliki na biashara anazofanya Rugemalira kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, haviwezi kumpa shaka mtu anayemfahamu kuhusu uwezo wake au kampuni yake kutoa mchango mkubwa kama huo,” alisema.
Alisema ni desturi ya kawaida katika Kanisa kwa waamini kutoa michango na matoleo mbalimbali kila mmoja kwa kadri ya uwezo na ukarimu wa moyo wake na kwamba matoleo ya waamini hutumika katika shughuli za uinjilishaji na uendeshaji wa Jimbo, Parokia na taaisi zake.
Askofu huyo aliongeza kuwa hutumika katika miradi maalum iliyokusudiwa na matoleo hayo na kwa kadri ya matakwa na lengo la mtoaji.
“Nilipokea matoleo hayo kwa roho safi na moyo mweupe na wa shukrani kama tunavyofanya siku zote tunapopokea ukarimu wa michango na matoleo ya waamini wetu. Na tangu matoleo hayo yalipotolewa Februari, mwaka jana, hakuna mamlaka yoyote iliyowahi kuniuliza ,” alifafanua na kuongeza:
“Nawaomba waamini tuendelee kujitoa kwa hali na mali katika kulijenga Kanisa la Mungu; kila aliyepewa talanta na Mungu aitumie kwa kuzalisha matunda mema ili kulijenga kanisa letu na hatimaye kuurithi ufalme wa mbinguni.”
Hata hivyo, alisema Kanisa hilo litaendelea kuwa mstari wa mbele katika kutetea haki, ukweli na uadilifu, na halitarudi nyuma wala kukaa kimya katika kukemea maovu katika jamii.
UHUSIANO NA FAMILIA YA RUGEMALIRA Alisema familia ya Rugemalira ni waumini wakatoliki wanaosali katika Parokia ya Bikira Maria Malkia wa Rozari Takatifu, Makongo juu katika Jimbo Kuu la Dar es Salaam na kwamba ni washiriki wazuri katika shughuli za ibada na wamekuwa na moyo mkubwa wa ukarimu katika kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo ya Kanisa ndani na nje ya jimbo.
“Binafsi, nimeifahamu familia hii muda mrefu kutokana na majitoleo yao katika shughuli za Kanisa na uhusiano baina yangu na familia hiyo ulizidi kuimarika pale alipopangwa kufanya huduma za kichungaji katika Parokia ya Makongo Juu nikiwa Paroko Msaidizi, mwaka 2008,” alibainisha na kuongeza:
“Kipindi hicho ilikuwa katika harakati za ukamilishaji wa ujenzi wa nyumba ya mapadre na mikakati ya ujenzi wa Kanisa jipya la Parokia na walikuwa wachangiaji wazuri katika kufanikisha.”
Hata hivyo, aliwaomba waumini wa kanisa hilo kuendelea kujitoa kwa hali na mali katika kulijenga Kanisa la Mungu.
Aidha, Askofu huyo alisema utume wa kanisa siku zote umekuwa ukiwezeshwa na kutegemezwa kwa nguvu ya Mungu Roho Mtakatifu anayeliongoza kanisa katika ukweli wote, na kwa sadaka, matoleo na michango mbalimbali ya hali na mali kutoka kwa waamini na watu wengine wenye mapenzi mema waliopo ndani na nje ya nchi.
“Kwa waumini kutoa michango na matoleo kwa kanisa na watumishi wake ni jambo la kawaida katika desturi za imani yetu tangu nyakati za mitume,” alisema Askofu Nzigilwa.
KASHFA YA ESCROW Mei, mwaka jana, Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, aliibua kashfa ya kuchotwa kwa zaidi ya Sh bilioni 306 katika akaunti ya Tegeta Escrow, ambayo ilipingwa vikali na baadhi ya wabunge na viongozi wa serikali na Mbunge huyo kutakiwa kufuta kauli kwa kulidanganya Bunge.
Mbunge huyo aliendelea na msimamo wake na kutaka Bunge kuunda kamati ya kuchunguza sakata hilo.Juni mwaka jana, Bunge liliagiza Ofisi ya CAG kufanya ukaguzi wa fedha hizo na ripoti yake kuwasilishwa Bungeni.
Baada ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kukamilisha kazi yake, ripoti hiyo ilikabidhiwa kwa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), chini ya uenyekiti wa Zitto Kabwe.
Kamati hiyo ilifanya uchunguzi na kuweka wazi ripoti na mapendekezo yake ya awali ambayo yalizua mjadala mkali bungeni kiasi cha kutishia Bunge kushindwa kufikia maamuzi ya pamoja na baadaye Spika Anne Makinda, aliunda kamati ya maridhiano ambayo ilikubaliana katika maazimio yaliyowasilishwa Bungeni na Zitto.
Novemba 26, mwaka jana, Zitto, aliwasilisha ripoti iliyowataja viongozi wa dini, serikali na watu wengine waliopokea fedha za Tegeta Escow.
Viongozi wa dini waliotajwa na Zitto kiasi cha fedha walichopokea kwenye mabano ni Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini (Sh. milioni 80)  Askofu Eusebius Nzigirwa na Padri Alphonce Twimanye Simon (Sh. milioni 40.4), ambao walipewa fedha hizo kupitia Benki ya Mkombozi.
VIONGOZI WA SERIKALI WALIOWAJIBIKA Desemba 16, mwaka jana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, alijiuzulu nafasi kutokana na ushauri alioutoa.
Desemba 22, mwaka jana, Rais Jakaya Kikwete, alimfukuza kazi Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ambaye katika kashfa hiyo alipokea kiasi cha Sh. bilioni 1.6, huku akimuweka kiporo Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Desemba 23, mwaka jana, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alimsimamisha kazi Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake.
VIONGOZI WENGINE WALIOPATA MGAWO Viongozi waliopata mgawo wa Rugemalira Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (bilion 1.6); Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (milioni 40.4); Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Daniel Yona (milioni 40.4); Mbunge mstaafu Paul Kimiti (milioni 40.4); Msajili wa zamani wa Hazina na Mjumbe wa Bodi ya Tanesco, Dk. Enos Bukuku (milioni 161.7).
Wamo pia Jaji Profesa Eudes John Ruhangisa (milioni 404.25) na Jaji Aloysius Mujulizi (milioni 40.4).
Watumishi wa umma ni aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa wa Rita, Philip Saliboko (milioni 40.4); aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Emmanuel Ole Naiko (milioni 40.4) na Mtumishi wa TRA, Lucy Appolo (milioni 80.8).


CHANZO: GAZETI LA NIPASHE

Read More »