Mh. John Mnyika awasilisha udhaifu wa mchakato wa mabadiliko ya katiba kwa katibu wa bunge


Mbunge wa jimbo la Ubungo Mh John Mnyika amewasilisha kwa katibu wa bunge taarifa ya hoja binafsi kuhusu kile alichodai kuwa ni udhaifu wa mchakato wa mabadiliko ya katiba ili bunge lijadili udhaifu wa ukiukwaji wa sheria katika mchakato huo ili lipitishe azimio la kuahirisha mchakato huo mpaka madhaifu ya msingi yatakaposhughulikiwa.
Akizungumzana na mtandao huu katika ofisi za bunge Mh Mnyika pia amemtaka rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kuheshimu makubaliano ya viongozi wa vyama vya siasa kwa kuwa kuendelea na mchakato huo si tu kukiuka makubaliano ya TCD bali pia ni kukiuka sheria zilizouanzisha mchakato huo.

0 comments: