ZARI HAWEZI KUZAA NA DIAMOND, MUME AANIKA SIRI NZITO!





Oohoo! Wakati staa mkubwa wa muziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akichekelea kitendo cha mpenzi wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘Zari’ au ‘The Boss Lady’ kunasa mimba yake, habari ya mjini huko Kampala, Uganda ni juu ya aliyekuwa mume wa mwanamama huyo,
Ivan Ssemwanga kufunguka na kusema: “Naapa Zari hawezi kuzaa na Diamond.”HABARI YA MJINI
Wikiendi iliyopita, vyombo vya habari na mitandao nchini Uganda ambako kuna makazi mengine ya Zari mbali na Afrika Kusini, kulipambwa na habari hizo baada ya mwanaume huyo aliyezaa na mwanamama huyo watoto watatu kuanika siri nzito juu ya ishu hiyo.
‘Ubuyu’ huo ulidadavua kwamba, kwanza jamaa huyo mwenye utajiri wa kutupwa alianza kwa kuelezea namna alivyoshtuka aliposikia Zari ni mjamzito.
Alisema kwamba alishangaa kusikia Zari ni mjamzito wakati ana umri wa karibia miaka 40 na watoto watatu ambao amekuwa akiwapuuza na kuendelea kuzurura na mpenzi wake mpya, Diamond sehemu mbalimbali ndani na nje ya Bara la Afrika.

0 comments: