NEW ALART: CCM KUANZA FAGIO LA VIONGOZI WIKI IJAYO


Chama cha Mapinduzi (CCM) wiki ijayo kitaanza rasmi vikao vyake kwa ngazi ya Taifa vitakavyo chunguza maadili ya viongozi ikiwa ni maandalizi ya kuwapata wagombea wanaokubalika na wananchi katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alitoa taarifa hiyo jana katika mkutano maalumu wa kuwashukuru Watanzania kwa kukichagua chama hicho katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Desemba 14, mwaka jana. Alisema chama chake kinajipanga kuwa na viongozi wasio wamangimeza na wenye moyo wa kuwatumikia wananchi.
Katibu huyo Mkuu aliwashukuru Watanzania kwa kukipa ushindi chama chake na kubainisha kuwa kitaifa, CCM imeshinda kwa asilimia 81.
Hata hivyo, alisema katika maeneo ambayo imeshindwa kama Wilaya ya Pangani, itafanyika tathmini na watajipanga kuhakikisha Uchaguzi Mkuu ujao wanapa ushindi wa kishindo.Alisema watahakikisha wanashinda katika maeneo yote waliyofanya vibaya.

0 comments: