POLISI DAR WAZIMA VURUGU KWA MABOMU YA MACHOZI



Polisi jijini Dar es Salaam wamelazimika kufyatua risasi hewani na kupiga mabomu ya machozi kufuatia kuibuka kwa vurugu katika hoteli ya Land Mark ambapo shughuli ya uapishaji wa wenyeviti wa Serikali za Mitaa ulikuwa ukifanyika.
Vurugu hizo, zimeibuliwa na kambi ya upinzani ambayo ilikuwa ikilalamikia kuwa Mwenyekiti mmoja wa Chama tawala CCM aliyeapishwa hakuwa ameshinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, uliofanyika mwaka jana.



0 comments: