SHIA WATUMA SALAM ZA KRISMASI, MWAKA MPYA KWA WAKRISTO

0 comments
Imam wa Msikiti wa Kigogo Post uliopo Kigogo, Dar, Hemed Jalala,  akizungumza na waandishi wa habari katika tukio hilo.Bango la kuwatakia Wakristo heri ya Krismasi na Mwaka Mpya kutoka kwa Waislam.Baadhi ya watu waliodhuhuria hafla hiyo wakimsikiliza Imam Jalala (hayupo pichani).Waandishi wa habari wakiwa kazini.
WAISLAM wa madhehebu ya Shia nchini wamewatumia Wakristo nchini salam za Krismasi na Mwaka Mpya katika moyo wa kupendana kiimani.
Ujumbe huo ulitumwa na Imam wa Msikiti wa Kigogo Post, jijini Dar es Salaam,  Hemed Jalala, akisisitiza mshikamano na upendo kwa walimwengu wote bila kujali imani zao.

Read More »

Kwako shabiki wa D’Banj….. hii ni video yake mpya INGIA HAPA KUITAZAMA VIDEO HII

0 comments
.
.
Staa kutokea Nigeria, D’Banj amekuletea hii video mpya ya single yake iitwayo Feeling the nigga ambayo katika video ameonekana aliyekuwa mwakilishi wa Nigeria kwenye shindano la Big Brother Africa Hotshots 2014 Tayo.
Itazame hapa

.
Hizi ni baadhi ya picha kutoka kwenye video hiyo ikiwemo ya aliyekuwa mwakilishi wa Nigeria kwenye Big Brother Africa Hotshots Tayo
.
.
.
.
.
.
.

 CLICK HAPA CHINI KUITAZAMA VIDEO HII








Read More »

TIBAIJUKA ASEMA BAADA YA RAIS KIKWETE KUNIFUKUZA KAZI SASA NIPO JIMBONI KWANGU KUTATUA KERO ZA WANANCHI WANGU SOMA HAPA

0 comments

Baadhi ya wananchi mkoani Kagera wamepinga  uamuzi   wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete  kwa kumuondoa madarakani waziri wa ardhi nyumba na makazi   na kuwaweka kiporo viongozi wengine walioshiri kuhujumu pesa za akaunti ya Tegeta Escrow.

 
Wakiongea  na mwandishi mwetu, wananchi wa mkoa huo wamesema hawajajua  nini hatima ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. kikwete kwa kuwaweka Kiporo mawaziri wengine  waliohusika katika sakata hilo   na kumuuondoa waziri  Tibaijuka   na pia wamebaki na sintofahamu  ambapo wamemtaka  Rais  kutoa ufafanuzi kuwa licha ya kumng’oa madarakani kiongozi huyo  Je, Pesa  hizo zitarudishwa kwenye akaunti hiyo  ya Tegeta Escrow au la.
 
Nao baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa vya mkoa huo akiwemo katibu  wa siasa na uenezi wa Chama cha Mapinduzi  mkoa wa Kagera Hamimu Mahamudu amepongeza uamuzi wa Rais alioutoa   wakati  akiongea na wazee wa jijini Dar es salaam  kwa kumuondoa kiongozi huyo.
 
Kwa upande wake, katibu wa chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema  katika manispaa ya Bukoba Victor Sherejei akisema kuwa Rais hajatoa uamuzi sahii ambapo amemtaka  Rais kuwafahamisha watanzinia kuwa Pesa za Escrow zitarudishwa  lini katika akaunti hiyo au kuwaondoa viongozi hao madarakani ndio suluhisho  na kwamba pesa hizo hazirudishi?.
 
Kwa upande wake  aliyekuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka amesema  licha  ya Rais kumuondoa katika nafasi yake aliyokuwa nayo sasa amerudi jimboni kwake kwaajili ya  kutatua kero na changamoto mbalimbali za wananchi wake kwani nafasi aliyokuwanayo ilikuwa haimpi nafisi  ya  kuwasimamia wananchi katika jimbo lake na kwamba Pesa hizo alizopewa na Rugemalila zilikuwa za kusaidia shule na alipewa kama zawadi bila kujua kama  pesa hizo zilitoka katika akaunti ya Tegeta Escrow ndo maana hakutaka kujiuzulu.


Read More »

Mliberia Yanga anatafutwa Ulaya HABARI KAMILI IPO HAPA

0 comments
Mshambuliaji hatari wa Simba, Kpah Sherman.
Na Saleh Ally
WAKATI Yanga ikiwa katika maandalizi ya mwisho kuwavaa Azam FC katika mechi ya Ligi Kuu Bara, jambo jipya limeibuka kuwa yule mshambuliaji wake hatari, Kpah Sherman raia wa Liberia, anatuhumiwa kutoroka kazini nchini Cyprus.

Taarifa kutoka Cyprus barani Ulaya kwa mmoja wa Watanzania wanaoishi nchini humo zimeeleza vyombo vya habari nchini humo, vimeripoti kuwa Mliberia huyo atafunguliwa mashitaka baada ya kutorokea Tanzania.“Nimesikia huyo mchezaji yuko huko nyumbani, ila huku vyombo vya habari vya hapa vimeripoti timu yake ina mpango wa kufungua kesi Fifa kuelezea kuhusiana na kutoroka kwake,” alisema Mtanzania huyo anayeishi nchini humo.
Juhudi za kuwapata viongozi wa Yanga ilikuwa ni ‘sheedaa’, imeelezwa Mwenyekiti Yusuf Manji yuko nje ya nchi na katibu mkuu mpya, hajaingia ofisini rasmi.Uongozi wa Klabu ya Centikaya TSK ya Cyprus, umethibitisha kushitushwa na taarifa za Sherman kuondoka nchini humo akidai ana matatizo ya kifamilia.
Lakini baadaye ukapata taarifa kuwa amejiunga na klabu kongwe ya Tanzania iitwayo Yanga nao wakaanza mipango ya kufungua mashitaka kwenye Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Akizungumza na Championi Jumatano kutoka Cyprus, Rais wa Centikaya TSK, Meric Erulku amesema ni kweli kumekuwa na hali kutoelewana.“Kweli hali hiyo imetokea, hatukuambiwa kama anakwenda kwenye majaribio na ruhusa aliyopewa haikuwa ya kwenda kufanya majaribio.
“Kweli tuna mkataba naye, haujaisha na haujavunjwa. Pia hatujalipwa na kulikuwa na mpango wa kwenda Fifa, lakini meneja wake amezungumza nasi.“Hivyo tunaendelea na hayo mazungumzo ili kujua tutafikia wapi. Kwa kuwa hapa katikati kuna sikukuu, naomba unitafute Jumanne ijayo nitakupa jibu sahihi kama tunakwenda Fifa au tumemalizana nao,” alisema Erulku maarufu kama Buzlat.
Sherman amejiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili akichukua nafasi ya Mganda Hamis Kiiza.
Tayari Sherman ameichezea Yanga mechi moja ya kirafiki dhidi ya Simba ambayo Yanga ililala kwa mabao 2-0.Hata hivyo, Mliberia huyo ameonekana kukonga nyoyo za mashabiki kiuwezo baada ya mechi hiyo moja.

Read More »

DIAMOND AANIKA SABABU 5 ZA KUMPENDA ZARI! INGIA HAPA KUPATA HABARI KAMILI

0 comments

Mapenzi bhana! Baada ya kutoka kimalavu na kumwagana na mwanadada mwenye mvuto Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ kisha kuangukia kwenye ‘utamu’ wa penzi la mwanamama anayekimbiza Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ameamua kuanika siri tano za kilichomvutia kwa staa huyo gumzo Afrika Mashariki.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na mwanamama anayekimbiza Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady.
Akizungumza katika mahojiano maalum katika ofisi za gazeti hili, Bamaga-Mwenge jijini Dar hivi karibuni, bila kupepesa macho au kuuma maneno baada ya kuulizwa kinagaubaga juu ya ukaribu wake na Zari, Diamond au Dangote hakutaka kuficha, akaamua kuweka mambo yote hadharani.
MATANGAZO
Alifunguka: “Mimi ni mwanamuziki mkubwa na mwenye heshima, wakati mwingine natakiwa kuwa na akili ya kuwa na uhusiano na watu ambao watakuwa msaada kwangu pia.
“Siwezi kuwa karibu na mtu ambaye hataniongezea kitu chochote kile. Baada ya kujitangaza sana Tanzania, nikahamia Kenya ambapo nilikuwa karibu na mwanadada Avril. Ukaribu wangu kwake, ukanifanya Kenya kutambulika.

“Baada ya kukaa kwa muda, nikataka nitambulike na Uganda pia, unafikiri ningefanya nini? Nikaliteka soko lao kwa kuwa karibu na mrembo Zari.
“Kweli nimefanikiwa na hata siku ya shoo yake (Desemba 18, mwaka huu nchini Uganda), ilikuwa ni balaa kiasi kwamba sikuamini kilichokuwa kimetokea, watu walikuwa nyomi ile mbaya. Mbali na kuwa mwanamuziki mkubwa, bado nahitaji kujitangaza zaidi.”

Zari na Diamondi wakibusiana kimahaba.
MSISIMKO
Sababu ya pili aliyoitaja ni kwamba Zari ambaye ni mama wa watoto watatu ana msisimko wa aina yake tofauti na ‘mashori’ wengine aliwaowahi kuanguka nao dhambini.

“Hakuna mwanaume anayependa kukaa na msichana asiyekuwa na msisimko wa kimapenzi. Hebu fikiria umekaa na mwanamke mwenye umbo kama la mwanaume, utapata msisimko gani hapo? Lakini mcheki mtoto alivyong’aa, anameremeta, mtoto yupo bomba, ukikaa karibu yake tu utagundua kwamba umekaa na msichana mwenye mvuto ambaye kila wakati atakufanya kuwa bize kumwangalia.”
BIASHARA
Sababu ya tatu aliyoitaja Diamond ni kwamba mwanadada huyo yupo vizuri kibiashara.
“Ninaangalia fedha, ili biashara zangu ziweze kupiga hatua sina budi kukaa karibu na mfanyabiashara mwenzangu (Zari) kwa ajili ya kushauriana biashara ziende vipi. 

“Yeye (Zari) ni mkongwe katika biashara, kuwa karibu naye naamini nitajifunza mambo mengi sana.
Amekuwa muwazi kwangu na amenipa mianya mingi ya kufanya biashara, lakini je, nisingekuwa karibu naye, michongo hiyo ningeipata vipi?”

Zari na Diamondi wakiwa kwenye pozi.
UZURI
Sababu ya nne ya kuwa na Zari, Diamond alidai kwamba mwanamama huyo ni mzuri kupita maelezo.
Alifunguka: “Mimi ni mwanamuziki mkubwa, watoto wazuri wananipenda kwa hiyo kama ningefanya uamuzi wa kuwa na mwanamke asiyekuwa mzuri, maneno yangeanza kusikikasikika na isingekuwa poa. Mbali na kuwa mfanyabiashara, kumtumia kama msaada wa kunitangaza, lakini Zari ni mzuri bwana. Ni mwanamke ambaye kwa kumwangalia tu, unaweza kusema kwamba haujawahi kukutana na mwanamke mzuri kama yeye.

ANAJITAMBUA
Sababu ya mwisho aliyoianika Diamond ni kwamba Zari yupo vizuri kichwani kwa maana ya kujitambua tofauti na wanawake wote aliowahi kutembea nao.

Mwanadada mwenye mvuto Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’.
“Nimekuwa na wanawake tofautitofauti lakini kwa Zari, ni mwanamke mwenye hekima na anajitambua sana. Si mzungumzaji kivile na huwa anapenda kufanya vitendo kuliko maneno.
“Anajua ni kipi anatakiwa kufanya na akili yake ameielekezea kwenye fedha zaidi. Hapendi masihara na fedha, anapenda kujitoa na ni mchakarikaji sana. Nampenda mwanamke wa hivyo kwa kuamini kwamba atanifanya nijitume zaidi.”

AWACHAMBUA JOKATE, WEMA NA PENNY
Diamond alipoulizwa juu ya kasoro za warembo wakali Bongo aliowahi kutoka nao wakiwemo mrembo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’, Wema na mtangazaji wa Radio E-FM, Penniel Mungilwa ‘Penny’, aliwachambua mmoja baada ya mwingine na kuhitimisha kuwa ni wazuri lakini hawamfikii Zari.

Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
UTAMBULISHO KESHO DAR LIVE
Mbali na kuziweka wazi sifa za Zari, jamaa huyo alidai kwamba atamtambulisha rasmi kwa Wabongo kesho usiku kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Burudani wa Dar Live, Mbagala jijini Dar atakapokuwa anaangusha burudani ya kibabe katika Tamasha la Wafalme akiwa na mfalme mwenzake, Mzee Yusuf na wakali wengine kibao kwa kiingilio cha shilingi 10,000/= kwa kawaida na shilingi 20,000/= kwa V.I.P.

Read More »

AMA KWELI INSTAGRAM IMETUHARIBIA WATOTO WETU WA KIKE ...HEMBU SHUHUDIA HAPA

0 comments




It was just the other day when Socialite Huddah Monroe in a TV interview referred to her once BFF in the 'socialite business' Vera Sidika as a walking corpse. This is after photos of 'Vera Sidika's skin falling apart' surfaced online a few days ago.
The bootyfull bleached beauty is on the offensive this time around posting some super sexy pics of her in something that looks like paradise. Talk of living large! Check them out below


;




Read More »

MUME WANGU ANAPENDA STAILI ZA AJABU SANA SIJUI AMEZITOA WAPI...?? AU ANA MWANAMKE MWINGINE, USHAURI JAMANIIII

0 comments





MIMI NI MAMA WA MIAKA 36, NINA WATOTO WATATU, NINA MIAKA TISA KWENYE NDOA, TULIPOONA NA MUME WANGU TULIKUWA TUKIFANYA MAPENZI STYLE ZA KAWAIDA TU, TUNABADILI STYLE LAKINI NI ZILE ZA KAWAIDA
Umefika miezi sasa mume wangu amebadilika sana, yani hatulii yani mimi nayeye hatukai nusu saa bila ugomvi, kitu kidogo tu, hasira kwangu na anapeleka hadi kwa watoto wangu, yani hadi wanamuogopa sasa hivi, wakimuona tu! Wote wanaenda kulala,
Hadi sasa nahisi mume wangu anamwanamke nje, tena ni Malaya kabisa, maana mume huyu huwa nakaa namfikiria naona kama wamenirogea vile, hajui kubembeleza kwenye mapenzi, yeye ni kuamrisha tu, tofauti na zamani, hata mimi nikimbembeleza labda nimshike shike sehemu ambazo najua akishikwa anafurahi, nimnyonyenyonye hapa na pale, zamani alikuwa anapenda sana. Siku hizi hataki kabisa, nikianza tu, anasema ah! Nimechoka mimi, kwanza nimeshaoga unanipaka matemate yako, wakati bafu liko hapo chumbani angeweza kuoga tena,


Sasa kuna kipindi nami niliamua kukaa kimya, nikawa nasubiri hadi yeye aanze, lakini sasa style alizokujanazo sasahivi mimi siziwezi, yani sio za kawaida, nina mwili mkubwa, nilizaa kwa operation, nina kovu tumboni, siwezi kujikunja kunja Napata maumivu, sasa yeye utakuta ananikunja kama samaki, yani nabanwa nakuwa mdogo, nalia sana, sio kwa raha ila ni kwamaumivu, na hata nikilia anasema nisubiri hadi amalize ndio aniache, akiniacha tu! Ujuwe lazima nitalala hata siku mbili, naumwa sana kiuno,




Kuna siku nilimuuliza kwanini ananifanya kama ananibaka vile, akasema akifanya style za zamani hasikii raha kabisa, kuna kipindi alianza kuniambia kuwa anataka anifanye nyuma, sikuamini masikio yangu, nililia sana, nikamwambia ndoa na ife, narudi kwetu, akanisihi nibaki, nashukuru hakurudia tena kutamaka ushenzi huo,


Style zake za sasa hivi sijui anazitoa wapi, yani sasahivi akiniambia kama anahitaji tu! Basi naweza meza hata dawa ili nijifanye naumwa, napoteza furaha kabisa, yani hawezi kabisa kunifanya kawaida, naombeni mnishauri nifanyaje, maana ni kweli kwa mwanamke yeyote Yule style ninazofanywa mimi, lazima angelia, mimi hadi huwa nakwenda hospitali, ila nikifika sisemi kama nimefanya style mbaya, huwa nadanganya maana naona ni aibu, nitamuaibisha mume wangu na mimi pia.

Read More »

PICHA NYINGINE ZA WEMA SEPETU NA VAN VICKER KATIKA MOVIE YAO MPYA.

0 comments





Read More »

GEORGE H.W BUSH ALAZWA HOSPITALI NCHINI MAREKANI

0 comments
George H.W Bush.
 ALIYEKUWA Rais wa 41 wa Marekani, George H.W Bush amekimbizwa katika hospitali ya Houston Methodist nchini Marekani baada ya kupatwa na tatizo la kupumua.
Alipelekwa katika hospitali hiyo kwa gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) jana usiku.
Wawakilishi wa Bush wanasema kuwa hatua hiyo ya kupelekwa hospitali ni kama tahadhari.

Bush mwenye umri wa miaka 90 alikuwa madarakani tangu mwaka 1989-1993 na ndiye Rais mzee kuwahi kuiongoza Marekani akimshinda Jimmy Carter kwa miezi michache.
Alihudumu kwa muhula mmoja baada ya kushindwa na Rais Bill Clinton.
Bush ambaye hawezi kutumia miguu yake, hivi karibuni alionekana amekaa katika kiti cha magurudumo kwenye hafla iliofanyika mwezi Novembea katika chuo Kikuu cha Texas na mwanaye aliyekuwa Rais wa 43 wa Marekani, George W Bush.

Read More »

Picha,Diamond Platnumz Akiwa Ikulu Na Tuzo Zake Tano. SOMA HAPA

0 comments
Msanii Diamond Platnumz amepata nafasi ya kipekee ya kukutana na rais leo December 23 2014 kwenye Ikulu ya Tanzania. Diamond amekaribishwa ikulu kwenda kupokea shukrani kwa kufanikiwa kuwakilisha taifa la Tanzania vizuri kwenye tuzo tofauti nje na ndani ya africa zikiwemo za kituo kikubwa cha Tv cha Channel O zilizofanyika mwaka huu huko Afrika Kusini.
Diamond Platnumz alikuwenda na tuzo zake tano na kumuonyesha Rais Jakaya Kikwete.

diamond 3 

romy 2 
 romy 3 romy j 1

Read More »

Picha,Marcio Maximo aondoka rasmi nchini kurejea kwao nchini Brazil. INGIA HAPA

0 comments

Baada ya Taarifa rasmi kutoka klabu ya Yanga December 15, 2014 kuwa kocha Mbrazil Marcio Maximo ameondoka ndani ya timu hiyo  baada ya uongozi wa Yanga kufikia makubaliano naye ya kuvunja mkataba, Marcio Maximo aondoka rasmi nchini kurejea kwao nchini Brazil na ndege ya shirika la ndege la Emirates.
 Maximo

Read More »

KAULI YA KAFULILA BAADA YA HOTUBA YA RAIS KIKWETE KUHUSU SAKATA LA ESCROW

0 comments




1. Hoja kwamba pesa zilitolewa kwa uamuzi wa hukumu ya sept 5.2013 sio sahihi kwa sababu hukumu ilisema ALL AFFAIRS OF IPTL SHOULD BE HANDED TO PAP. Haikusema kama escrow monies ni party of affairs of IPTL kwasababu zilikuwa kwenye mgororo.
  
 Hoja ya kusema hukumu ilisema ilikuja baada ya kikao cha Oct8.2013 kunduchi beach hotel ambacho kiliongeza maneno kwenye hukumu kwa kusema ALL AFFAIRS OF IPTL INCLUDING RECEIBLES FROM ESCROW AC SHOULD BE HANDED TO PAP. Huko ni kupotosha hukumu kwani hela za escrow zilikuwa na mgogoro kati ya Tanesco na IPTL na PAP kununua IPTL haimanishi mgogoro kati ya IPTL na TANESCO umekwisha bali PAP ingechukua nafasi ya IPTL kwenye mgogoro wa pesa za escrow. hili Rais kapotoshwa.

2. Kusema Muhongo atamtoa baada ya uchunguzi wake ikulu kukamilika ni mbinu ya kumlinda kwani mbona mawaziri wanne waliohusika ktk oparesheni tokomeza ripoti ya bunge ilitosha rais kutengua uteuzi wao na kisha rais akaunda tume ya rais uchunguzi. kwann kwa Muhongo inakuwa kinyume chake?

3. Bunge liliazimia mamlaka ya uteuzi ichukue hatua dhidi ya Maswi. Rais anasema suala la Maswi ameliacha kwa mamlaka ya nidhamu ambayo ni Katibu Mkuu Kiongozi, Hapa Rais amekwepa Jukumu lake kwani yy ndio anateua na kufukuza Makatibu wakuu. pia suala hili sio jipya kwa Katibu Mkuu Kiongozi ingetosha awe amekwisha kuchukua hatua za kinidhamu siku nyingi kama TRA walivofanya kwa wahusika tawi la Ilala.
 
4. Hoja kwamba kutaifisha mitambo ya IPTL kutakimbiza wawekezaji ina mapungufu kwasababu kwa mujibu wa ripoti ya CAG, PAP alifanya utapeli wa kughushi katika umiliki wa IPTL hivyo sio mwekezaji mwadilifu hivyo kutaifisha haiwezi kutisha wawekezaji. Pia ifahamike kwamba wawekezaji wengi wanatoka Ulaya na Amerika na nchi hizo ndio zimezuia misaada kutaka serikali itekeleze mazimio ya Bunge na mazimio ya Bunge ni pamoja na kutaifisha mitambo hiyo. Sasa inawezekanaje nchi hizo zinazotaka serikali itekeleze mazimio kwamba ndio zikimbie kuwekeza kwa sisi kutekeleza mazimio husika? hapa ni namna ya kulinda matapeli wanaokuja kwa jina la wawekezaji.

5.Hoja kwamba mikataba ikiwa wazi itakimbiza wawekezaji ina mapungufu kwasababu tatu:

   a. Nchi nyingi sasa duniani mikataba ipo wazi na mfano rahisi ni Ghana na bado wawekezaji hawajakimbikia kwasababu hiyo. Ndio utekelezaji halisi wa itifaki ya OPEN GOVERNANCE ambayo Tanzania tulisaini

   b. Kipengele cha Usiri (Confidentiality clause) kwa mikataba yote kinasema mkataba utakuwa siri isipokuwa kwa pande za mkataba(parties of contract) na kwa mahitaji ya dola( statutory purpose). sasa statutory purpose maana yake ni mahitaji ya Serikali, Bunge na Mahakama. sasa tatizo la sasa ni pale serikali inapokataa kutoa mikataba kwa bunge kwa hoja ya kipenge cha usiri (confidentiality clause) wakati kipengele hicho kinaruhusu Bunge kuwa na mamlaka ya kuona mikataba kama part of state organ.

  c. Pia wawekezaji hawa wanaposaini mikataba hapa wanakwenda kutafuta mitaji kwenye masoko ya mitaji kwao(stock markets). Kule kwenye masoko ya mitaji wanaweka wanalazimika kuweka mikataba hiyo wazi na wanaweka. hivyo kwa dunia ya leo ni aibu kuendelea kufanya mikataba kuwa siri. 

6. Hoja ya kodi. TRA walidai kodi kwa barua kwenda BOT  na Werema ndio aliandika barua kukataa kodi. Kwakuwa CAG alikiri ktk ripoti kuwa kodi ilipaswa kulipwa kiasi cha 23bn mana yake alosema kodi isilipwe anapaswa kuchukuliwa hatua za kutaka kusababisha hasara hiyo. ikumbukwe Basil Mramba yupo mahakamani mpaka sasa kwa kesi ya kusababisha hasara ya 11bb. Inawezekanaje hawa waishie kujiuzulu?

7. Mwisho kauli ya Mhe Rais kuwa fedha zile ni za IPTL kwasababu tu ziliwekwa kwenye escrow na Tanesco badala ya kulipwa moja kwa moja kwa IPTL kutokana na mgogoro sio sahh kwasababu pesa ya mgogoro kati ya Tanesco na IPTL haiwezi kuwa ya IPTL mpaka mgogoro umalizike na mwenyewe amekiri kuwa mpaka pesa hizo zinatolewa mgogoro ulikuwa haujamalizika. ni kwa mantiki hiyo pesa hiyo haikuwa sahh kuita ya IPTL.
 
Pia hapa niongeze kwamba Mgogoro wa IPTL kutoza zaidi Tanesco capacity charge unamanisha ni dhuluma ya IPTL tangu mwanzo wa utekelezaji wa mkataba mwaka 2002 na sio 2006 kama Mhe Rais alivosema. Hii ni kwasababu mgogoro wa IPTL ku overcharge Tanesco kwenye capacity charge msingi wake ni udanganyifu wa IPTL ktk mtaji na hivyo hesabu yake inapaswa kuzingatia tangu mwanzo wa utekelezaji wa mkataba mwaka 2002 na sio 2006 escrow ilipofunguliwa. Hii inakaziwa na Uamuzi wa mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya kibiashara (International Centre For Setllement Of Investment Disputes-ISCID) wa Feb12. 2014.

David Kafulila(MB)

Read More »

Picha,Cristiano Ronaldo Akizindua Sanamu yake ya heshima Aliyojengewa huko Medeira Ureno INGIA HAPA

0 comments
Cristiano Ronaldo ameizindua sanamu yake ya heshima aliyojengewa huko Medeira Ureno juzi , hii imekuja siku moja baada ya mchezaji pekee duniani kuweza kushinda makombe yote kwa ngazi ya klabu katika vilabu viwili tofauti.
sanamuu 2 sanamuu 3 sanamuu

Read More »

Bracket - Alive ft. Diamond & Tiwa Savage VIDEO IPO HAPA INGIA KUITAZAMA

0 comments


Mabibi na Mabwana,Bracket wametuletea hii video mpya waliyomshirikisha Diamond

http://djchokamusic.com/wp-content/uploads/2014/12/10832094_562769273867097_851001626_n.jpg

.
Hii ni video mpya ya wasanii kutokea Nigeria,Bracket iitwayo Alive waliyowashirikisha Tiwa Savage  pamoja na Diamond Platnumz ukishamaliza kuitazama mtu wangu usiache kuniandikia lako la moyoni ili Bracket na Diamond & Tiwa Savage wakipita waone watu wao mmesema nini kuhusu video hiyo.

             CLICK HAPO CHINI KUITAZAMA VIDEO


Read More »

Matokeo na Picha za Mechi ya Premier League ya Newcastle Dhidi Ya Sunderland

0 comments
pl 36
Matokeo na Picha za Mechi ya Premier League ya Newcastle Dhidi Ya Sunderland
adamjohnson
fabriciocoloccinistevenfletchernewcastle-sunderlandfannewcastlevsunderland  stevenfletchersteventaylor

Read More »

Matokeo na Picha za Mechi ya Premier League ya Liverpool Dhidi Ya Arsenal. INGIA HAPA

0 comments
pl 40
Matokeo na Picha za Mechi ya Premier League ya Liverpool Dhidi Ya Arsenal.
martin_skrtel_getty

Read More »

Wiz Khalifa kaungana na Davido na Huddah kwenye list ya Xmas hii.

0 comments


Ni gari aina ya Bugatti Veyron Rembrandt edition alilolinunua ambalo amelipa jina lake badala ya kuweka namba kama raia wengine huku pesa ya kulinunua ikitajwa kuwa ni 2.5 million ambayo kwa Tanzania ni zaidi ya 4246750000.

Wiz Khalifa amejinunulia huu mkoko kwenye kipindi hiki cha sikukuu ambacho mastaa wengine wa Afrika pia wamejinunulia magari yao akiwemo Davido wa Nigeria na Huddah wa Kenya.







huddah 2
Huddah.
dvd



Read More »