Picha,Nje Ya Chumba Cha Diamond Na Zari,Ulinzi Ulikuwa Hivi. INGIA HAPA

0 comments
askari 5
Mlinzi kutoka jeshi la Uganda 
askari
Hawa askari tuliwaona wakati Diamond Platnumz amewasili Uganda na kupokelewa Airport kwa mbwembwe sana.
askari 2 
Kumbe ulinzi wao uliendelea mpaka siku ya sho ambapo mmoja wao aliwekwa Nje ya chumba cha Diamond na Zari. Ni Mlinzi kutoka jeshi la Uganda akilinda usalama Wa@diamondplatnumz na @zarithebosslady  Hii picha akiwa nje ya chumba akiwasubiri wakati wakijiandaa.

Read More »

Aya Sasa Siku Ishafika December 19, ile ahadi ya Ali Kiba imetimia. Video ya “Mwana” iko hapa tayari INGIA HAPA KUICHECK HII SIO YA KUKOSA KUANGALIA

0 comments
Kiba II
maujanjayamjini.blogspot.com ilikupa kipisi cha video ya ‘Mwana’ ya msanii Ali Kiba, leo iko hapa tayari.
Kazi imefanywa na Godfather wa Afrika Kusini, karibu uinjeoy video hiyo hapa nitafurahi ukiniandikia comment yako. 

           CLICK HAPO CHINI KUICHECK VIDEO


Read More »

Unaifahamu timu yenye wachezaji wazee kuliko zote England? INGIA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments
united
Barani ulaya kila kitu hutawaliwa na tarakimu ambazo huwakilisha takwimu ambazo huhifadhiwa ili kuweka kumbukumbu ya jinsi ya kuendesha masuala mbalimbali kuanzia siasa , uchumi , biashara binafsi za watu na hata kwenye ulimwengu wa michezo .
Kwenye michezo takwimu ambazo zimezoeleka ni zile za kuonyesha jinsi wachezaji wanavyofanya kazi uwanja kwa maana ya asilia ya juhudi na mahali ambako kocha na wasaidizi wake wa masuala ya ufundi wanaweza kutambua ubora na udhaifu .
Hivi karibui takwimu zimeitaja klabu ya Manchester City kuwa timu ambayo ina wastani wa umri mkubwa kuliko klabu zote zinazoshiriki ligi za soka nchini England .
Manchester City imetajwa kuwa klabu yenye wachezaji wenye umri mkubwa kuliko wote.
Manchester City imetajwa kuwa klabu yenye wachezaji wenye umri mkubwa kuliko wote nchini England.
Takwimu hizi zimeonyesha kuwa Manchester City ina wastani wa umri wa miaka 28.8 kwa wachezaji wake umri ambao ni mkubwa kuliko klabu zote kubwa za ligi tano bora barani ulaya kwa maana ya Epl , Primera Liga , Serie A , Bundesliga na Ligue 1.
Kwa jumla Man City imeshika nafasi ya 7 katika utafiti uliofanyw akwa kutazama wastani wa umri wa wachezaji wa klabu zipatazo 500 barani ulaya kuanzia ligi kuu mpaka madaraja ya chini.
Manchester City ina wachezaji 12 ambao wana umri kuanzia miaka 29  kwenda mbele wakiwemo Kina Martin Demichelis , Frank Lampard ,Bacary Sagna , Yaya Toure , Gael Clichy , Jesus Navas na wengine .
Wachezaji kama Nemanja Vidic wanaifanya Ligi ya Serie A iwe ligi inayoongoza kwa kuwa na wastani wa umri mkubwa kwa wachezaji.
Wachezaji kama Nemanja Vidic wanaifanya Ligi ya Serie A iwe ligi inayoongoza kwa kuwa na wastani wa umri mkubwa kwa wachezaji.
Takwimu hizi zinaonyesha kuwa Manchester City kwa timu za England ndio timu yenye wachezaji wenye umri mkubwa kuliko zote huku ikifuatiwa na Cyrstal Palace , Stoke City,West Bromwich Albion na QPR .
Kwa upande wa timu ambazo zina wastani wa umri mdogo ni Newcastle United , Manchester United , Southampton , Arsenal na Liverpool .
Ligi ya Uholanzi inaongoza kwa kuwa na wachezaji wenye wastani mdogo kwenye umri .
Ligi ya Uholanzi inaongoza kwa kuwa na wachezaji wenye wastani mdogo kwenye umri .
Ligi ya Italia Serie A inaonyesha kuwa ndio ligi yenye wastani wa umri mkubwa kwa wachezaji wake huku ligi ya Uholanzi ikionekana kuwa ligi yenye wastani wa umri mdogo kwa wachezaji wa timu zake .

Read More »

Takwimu zinazoonyesha ubora wa Real Madrid. SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments
real celebrating
Klabu ya Real Madrid ya nchini Hispania bila ubishi wowote ndio klabu bora kwa sasa ulimwenguni kote , hii ni kutokana na aina ya matokeo ambayo wanayapata kwneye mashindano mbalimbali ambayo wanashiriki kuanzia ligi ya Hispania , Kombe la Mfalme , Ligi ya mabingwa barani ulaya na michuano ya kombe la dunia inayoendelea huko nchini Morocco ambako mabingwa hao wa Ulaya wameingia hatua ya Fainali .
Jumla yote Madrid imeshinda michezo 21 katika mashindano yote rekodi ambayo wanazidi kuivunja huku kukiwa hakuna dalili zozote za timu hii kupata matokeo tofauti na ushindi  huku wakiwa wamevunja rekodi ya kushinda mechi 18 mfululizo iliyowahi kuwekwa na Barcelona iliyokuwa chini ya Mholanzi Frank Rijkaard katika msimu wa mwaka 2005/06.
Kwa kasi hii rekodi pekee ya kushinda mechi mfululizo iliyobaki kuvunjwa itakuwa ile iliyowahi kuwekwa na Ajax Amsterdam kwenye msimu wa mwaka 1971/72 ambapo timu hiyo ilishinda michezo 26 .
Wachezaji wa Real Madrid wakiwa mazoezini.
Wachezaji wa Real Madrid wakiwa mazoezini.
Ubora huu unaonekana kwenye matokeo unatokana na aina ya wachezaji ambao Real Madrid inao wakiongozwa na mchezaji bora kwa sasa Cristiano Ronaldo .
Takwimu kadhaa zinaonyesha kuwa Real Madrid wamekuwa bora kwenye kila idara na ni vigumu sana kuwazuia .
Katika michezo 21 ambayo timu hii imecheza hadi kufikia sasa , imefanikiwa kufunga jumla ya mabao 79 , ikiwa imeruhusu kufungwa mabao 10 pekee .
Katika mabao hayo 79 ambayo Madrid imefunga jumla ya mabao 19 yamefungwa kwa kutumia mguu wa kushoto , mabao mengine 42 yakiwa yamefungwa kwa kutumia miguu ya kulia na mengine 15 yakiwa yamefungwa kwa kicha .
Zaidi ya hapo , mabao 9 yamefungwa nje ya eneo la hatari au kisanduku cha penalty (penalty box) na mabao 70 yakiwa yamefungwa ndani ya eneo hilo  na mabao 8 yamefungwa kwa njia ya adhabu ya mkwaju wa penati .
Katika kipindi hiki chote wachezaji kadhaa wamechangia katika mafanikio ambayo Real imeyapata kwenye michezo yake 21 ambayo imeshinda mfululizo kuanzia kwa Cristiano Ronaldo , Gareth Bale , Karim Benzema , James Rodriguez , Toni Kroos, Isco ,Sergio Ramos , Pepe ,na kipa Iker Cassillas ambaye hatimaye amerudisha hadhi yake iliyowahi kutishia kupotea chini ya kocha Jose Mourinho .
Nyuma ya mafanikio yote haya ni kocha Mtaliano Carlo Ancelotti ambaye amefanikiwa kuwafanya wachezaji wote wa Real Madrid kuwa kitu kimoja na kupambana mwanzo mpaka mwisho kuhakikisha wanatimiza lengo ambalo ni kujaribu kuibuka na ushindi kwenye kila dakika 90 wanazokuwa uwanjani dhidi ya wapinzani wa aina tofauti .
Kocha Mtaliano Carlo Ancelotti amefanya kazi kubwa ya kuifanya Real Madrid kuwa timu bora barani Ulaya .
Kocha Mtaliano Carlo Ancelotti amefanya kazi kubwa ya kuifanya Real Madrid kuwa timu bora barani Ulaya .

Tarehe Mpinzani(timu) Mashindano Magoli(real) Magoli(wapinzani) Umiliki Mpira Ufasaha wa pasi Pasi Mashuti
16/09/14 Basle Champions League 5 1 54.35 90.36 560 17
20/09/14 Deportivo la Coruna La Liga 8 2 59.83 91.75 679 15
23/09/14 Elche La Liga 5 1 64.74 90.91 660 20
27/09/14 Villarreal La Liga 2 0 49.72 85.66 502 7
01/10/14 Ludogorets Champions League 2 1 60.93 87.77 548 15
05/10/14 Athletic Bilbao La Liga 5 0 60.12 86.76 589 19
18/10/14 Levante La Liga 5 0 61.3 90.72 636 17
22/10/14 Liverpool Champions League 3 0 54.17 88.38 680 12
25/10/14 Barcelona La Liga 3 1 42.19 85.38 431 11
29/10/14 Cornella Copa Del Rey 4 1 73.22 89.58 758 11
01/11/14 Granada La Liga 4 0 66.77 88.06 628 15
04/11/14 Liverpool Champions League 1 0 60.13 90.99 710 15
08/11/14 Rayo Vallecano La Liga 5 1 43.83 81.38 435 15
22/11/14 Eibar La Liga 4 0 62.3 85.51 559 17
26/11/14 Basle Champions League 1 0 53.32 84.35 543 6
29/11/14 Malaga La Liga 2 1 57.86 88.4 474 18
02/12/14 Cornella Copa Del Rey 5 0 63.08 89.71 680 10
06/12/14 Celta Vigo La Liga 3 0 48.78 81.75 389 17
09/12/14 Ludogorets Champions League 4 0 61.77 91 600 19
12/12/14 Almeria La Liga 4 1 60.5 79.91 458 12
16/12/14 Cruz Azul FIFA Club World Cup 4 0 58.28 89.16 609

Read More »

HII WATOTO AWARUHUSIWI KUINGIA HAPA CHECK PICHA ZA LAANA ZA UYU MDADA DAH NI HATARI AISEE........!!!!!!!

0 comments
Utaelewa tu tupo karne ipi na kizazi cha Jina gani.
Je unadhani hizi picha zilikusudiwa au zilipigwa bahati mbaya.



Read More »

JK:AKATISHA ZIARA YA MIZENGO PINDA SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI

0 comments

Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Waziri Mizengo Pinda amekatiza kwa muda, ziara yake katika Falme za Kiarabu kwa maelezo kwamba ameitwa nyumbani na Rais Jakaya Kikwete kwa shughuli maalumu.
Waziri Mkuu ambaye yuko katika ziara ya kutembelea nchi za Falme za Kiarabu, ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano na kutafuta wawekezaji, amekatisha ziara hiyo siku mbili baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kujiuzulu kutokana na kashfa ya Escrow.

Waziri mkuu Mizengo Pinda.
Werema alijiuzulu juzi na Rais Kikwete akaridhia hatua hiyo, huku umma ukisubiri hatua zaidi dhidi ya mawaziri na watendaji wa Serikali waliotajwa katika sakata hilo.Katika barua yake ya kujiuzulu, Jaji Werema alisema ushauri wake wa kisheria kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow haukueleweka na hivyo kuchafua hali ya hewa.
Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, leo Waziri Mkuu alitarajiwa kufanya mazungumzo na washiriki wa maonyesho ya B2B pamoja na kutembelea maeneo mengine lakini ziara hiyo imefutwa na badala yake anaondoka asubuhi kurudi nyumbani.Baadaye leo Pinda alitakiwa kwenda Doha, Qatar kwa ziara kama hiyo hadi Desemba 23.
Baada ya kukamilisha jukumu aliloitiwa, Waziri Mkuu anatarajiwa kurejea Falme za Kiarabu Jumamosi kuendelea na ziara yake.
(Chanzo: BBC)

Read More »

breaking news ESCROW: PROF. TIBAIJUKA AKATAA KUJIUZULU..ASEMA KAMA KUJIUZURU NI FASHENI BASI YEYE HAYUKO KIFASHENI

0 comments

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka, akiongea na wanahabari hivi punde ndani ya Hyatt Regency Hotel Dar es Salaam amesema haoni sababu ya kujiuzulu kutokana na sakata la akaunti ya Escrow.
Aongeza kuwa watu wanaona suala la kujiuzulu kama fasheni ila yeye hayupo katika fasheni hiyo.

Read More »

Flora Mbasha, akimbilia mahakama ya kisutu, akiomba kuvunja ndoa kati yake na mumewe Story Kamili Ipo Hapa

0 comments
Photo: Mwimbaji maarufu wa nyimbo za Inili, Flora Mbasha, amekimbilia mahakama ya hakimu mkazi kisutu, akiomba kuvunja ndoa kati yake na mumewe, Emmanuel Mbasha. Flora anadai sababu za kuomba kuvunja ndoa hiyo apewe talaka ni kutokana na tabia ya mumewe kumpiga, kumnyanyasa na kushindwa kumpatia matibabu.

Una lipi la kuwaambia wanandoa hawa?


Mwimbaji maarufu wa nyimbo za Inili, Flora Mbasha, 

amekimbilia mahakama ya hakimu mkazi kisutu, akiomba 

kuvunja ndoa kati yake na mumewe, Emmanuel Mbasha. 

Flora anadai sababu za kuomba kuvunja ndoa hiyo apewe 

talaka ni kutokana na tabia ya mumewe kumpiga, 

kumnyanyasa na kushindwa kumpatia matibabu.








Una lipi la kuwaambia wanandoa hawa?

Read More »

DIAMOND AMLA DENDA LIVE ZARI THE BOSS LADY NDANI YA LIFT NCHINI UGANDA Soma Hapa Kila Kitu

0 comments


Read More »

CHADEMA YATOA TAMKO: Yaitaka Serikali kuwachukulia hatua waliohusika na wizi wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.

0 comments
Photo: Chama cha demokrasia na  maendeleo-Chadema- kimeitaka serikali kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafikisha mahakamani viongozi waliohusika katika wizi wa fedha katika akaunti ya Tegeta -Escrow- licha ya wengine kuandika barua kujiuzulu wadhifa zao.->http://bit.ly/1z4oBah


Chama cha demokrasia na  maendeleo-Chadema- kimeitaka serikali kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafikisha mahakamani viongozi waliohusika katika wizi wa fedha katika akaunti ya Tegeta -Escrow- licha ya wengine kuandika barua kujiuzulu wadhifa zao.

Akizungumza na waandishi wa habari, naibu katibu mkuu wa Chadema, Mhe.John Mnyika amemtaka rais Jakaya Kikwete kuyafanyia kazi maadhimio ya bunge ya kuwaondoa na kuwafikisha katika vyombo vya sheria viongozi hao, hata kama watajiuzulu nyazifa zao.
 
Akielezea uchaguzi wa serikali za mitaa, naibu katibu mkuu wa chama hicho Zanzibar Bwana Salum Mwalimu amemtaka waziri wa tamisemi Mhe. Hawa Ghasia kutangaza matokea chaguzi za serikali za mitaa kwa nchi nzima badala ya kuwahachia viongozi wa vyama vya siasa kuendelea kuwadanganya wananchi kuwa vyama vyao vimepata ushindi wa kishindo.
 
Kwa upande wake baadhi ya wananchi wameitaka serikali kufuatilia ajira za wageni katika baadhi ya benki nchni kutokana na ongezeko la wizi ambao yanaambatana na baadhi ya watendaji kujiuzulu nyadhifa zao baada ya muda.

Read More »

Rais wa Serikali ya wanafunzi UDOM amekiri kuwepo kwa idadi kubwa ya wanafunzi wanaojihusisha na ukahaba

0 comments
Photo: Rais wa Serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha UDOM Masatu Kyabwene amekiri kuwepo kwa idadi kubwa ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu Dodoma kujihusisha na biashara ya ukahaba kutokana na kukosa mikopo.
 “Kuna baadhi ya wanafunzi chuoni kwangu wana maisha magumu sana kutokana na kukosa mkopo,wakati mwingine wananifuata mimi na kunielezea shida zao ili niwasaidie,wengine ni yatima hawana baba wala mama wa kuwalipia ada,siyo siri maisha ya wanafunzi hawa ni magumu sana”amesema.

Nini maoni yako kuhusu jambo hili?

Rais wa Serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha UDOM Masatu 

Kyabwene amekiri kuwepo kwa idadi kubwa ya wanafunzi wa 

vyuo vya elimu ya juu Dodoma kujihusisha na biashara ya 

ukahaba kutokana na kukosa mikopo. Akizungumza na paparazi 

alisema

“Kuna baadhi ya wanafunzi chuoni kwangu wana maisha magumu 

sana kutokana na kukosa mkopo,wakati mwingine wananifuata 

mimi na kunielezea shida zao ili niwasaidie,wengine ni yatima 

hawana baba wala mama wa kuwalipia ada,siyo siri maisha ya 

wanafunzi hawa ni magumu sana” 

Tatizo la kucheleweshwa kwa mikopo limekuwa sugu sana katika 

vyuo vikuu hapa tanzania ikiwemo chuo cha mzumbe morogoro 

ambapo wanafunzi wa mwaka wa pili hawajui hatma yao ya 

kupata mkopo tangu wapate matokeo yao ya mitihani.


Read More »

Angalia video clip hii ikimwonyesha ZARI (@ZariTheBosslady) wakati akimpokea DIAMOND (@diamondplatnumz) airport ya UGANDA

0 comments



10831760_1518195745097755_183207238_n


VIDEO IPO HAPA CLICK KUIANGALIA HAPO CHINI


Read More »

Picha,Mapokezi Ya Diamond Platnumz Uganda , Zari Alimpokea Airport Kwa Njia Hii Ingia Hapa Kuona Kila Kitu....!!

0 comments
zari 20
Msanii Diamond Platnumz ameondoka Tanzania leo mchana na kuelekea Uganda kwaajili ya Party yab Zari The Boss Lady. #ZariAllWhiteCirocParty inayofanyika Kampala. Hizi ni picha za Diamond alivyowasili kwenye uwanja wa ndege na kupokelewa na Zari.
zari noma
zari 19
zari 21
zari 16 zari 17

Read More »

Ingia hapa kuna PICHA jinsi Zari ampokea Diamond Kampala............ jionee hapa!!!

0 comments
10831760_1518195745097755_183207238_n

Zari baada ya kumpokea Diamond

Diamond Platnumz ametua Kampala jijini Uganda tayari kwaajili ya kutumbuiza Alhamis hii kwenye show ya Zari All White Ciroc Party‬ jijini humo. Diamond alipokelewa kwenye uwanja wa ndege na mpenzi wake Zari Ttale aka The Bosslady.

10853050_609935065778956_1732448788_n
Wawili hao wamekutana kwa mara nyingine baada ya hivi karibuni kuwa pamoja kwenye tuzo za Channel O.

Read More »

Ile issue ya Escrow, hii ni taarifa ya Kiongozi mmoja kujiuzulu leo December 16 Soma Hapa Kwa Habari Kamili

0 comments

Werema


Wiki chache zilizopita wakati Kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kikiendelea, macho ya watu wengi na masikio yalikuwa na hamu ya kutaka kuujua mwisho wa sakata la Escrow.
Wakati watu wengi wakisubiri maamuzi yatakayotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete kuhusiana na Ripoti juu ya issue ya ubadhilifu wa fedha kwenye akaunti ya Escrow, leo December 16 kuna taarifa iliyotufikia muda mfupi iliopita kuhusu kiongozi mmoja wa Serikali kujiuzulu.


 Taarifa iliyoripotiwa na kituo cha ITV inasema aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amejiuzulu siku ya leo na barua yake tayari imefika Ikulu ambapo Rais Kikwete ameridhia maamuzi hayo na kumshukuru kwa uamuzi huo kwa kuwa ushauri wake kuhusiana na suala la Tegeta Escrow haukueleweka.

Read More »

Sasa ametangaza rasmi kustaafu soka… Na huku ndiko anakoelekea kwa sasa… Ingia Hapa Kwa Habari Kamili

0 comments
Theirry-Henry-in-action-o-007 Kwenye ulimwengu wa soka leo kuna story kubwa ambayo imeenea Duniani kutokana na staa mkubwa wa soka na mkongwe kutangaza kustaafu soka na kujiunga na shughuli nyingine.
Kwa wale wapenzi wa soka Thierry Henry sio jina geni kwao, amekuwa nyota ambaye ameng’aa kwenye mchezo huo kwa muda mrefu sana akichezea vilabu mbalimbali ikiwemo Arsenal na Barcelona.
download
Jamaa ametangaza rasmi kustaafu soka dakika chache zilizopita na kusema kuwa kuanzia mwakani ataanza kujishughulisha kama Balozi wa Sky Sports huku akisema kuwa anajisikia furaha kuchezea vilabu vikubwa na pia anaamini anajiunga na kituo kikubwa cha Television na mattarajio yake ni kuwa mchambuzi bora wa michezo kwenye kituo hicho.

Read More »

Uganda In Burundi Out ndani ya Simba Sc. Soma Hapa Kwa Habari Kamili

0 comments
simba okwi


Ni kama vile klabu ya Simba ina mapenzi na taifa la Uganda baada ya klabu hiyo kukamilisha jumla ya wachezaji watano raia wa kigeni ambao wanatoka kwenye taifa hilo la Afrika Mashariki .

Simba imetangaza na kuthibitisha kuwa wachezaji wake watano wa kigeni kwa msimu huu ni Emmanuel Okwi, Daniel Serunkumma, Simon Serunkumma, Joseph Owino na Juko Mursheed.
Emmanuel Okwi na Joseph Owino ni wawili kati ya wachezaji watano raia wa Uganda walioko Simba.
Emmanuel Okwi na Joseph Owino ni wawili kati ya wachezaji watano raia wa Uganda walioko Simba.
Wachezaji wawili kati ya hao (Okwi na Owino ) na watatu wengine (Serunkumma Simon, Dany na Juko) wamesajiliwa katika kipindi hiki ambapo dirisha dogo la usajili liko wazi.
Nafasi za wachezaji watatu hao raia wa Uganda zimekuja kujaza nafasi za wachezaji wawili toka Burundi ambao ni Amisi Tambwe na Pierre Kwizera pamoja na Mkenya Paul Mungai Kiongera .
Dnny Sserunkumma ni raia mwingine wa Uganda aliyeko Simba.
Danny Sserunkumma ni raia mwingine wa Uganda aliyeko Simba.
Kiongera bado ataendelea kuwa mchezaji wa Simba hadi atakapopona jeraha lake la goti ambapo amekwenda kufanyiwa upasuaji nchini India huku Tambwe na Kwizera wakiwa wameachwa moja kwa moja .
Mrundi  Perre Kwizera ameachwa baada uongozi wa Simba kutoridhishwa na kiwango chake.
Mrundi Perre Kwizera ameachwa baada uongozi wa Simba kutoridhishwa na kiwango chake.

Mkenya Paul Kiongera ameachwa japo Simba itamtumia msimu ujao.
Mkenya Paul Kiongera ameachwa japo Simba itamtumia msimu ujao.
Mrundi mwingine aliyeachwa ni mfungaji bora wa msimu uliopita Amisi Tambwe.
Mrundi mwingine aliyeachwa ni mfungaji bora wa msimu uliopita Amisi Tambwe.


Read More »

Simba yaongeza nguvu kwa kusajili beki, unajua anatoka timu gani? Soma Hapa

0 comments
simba_logo_med_hr


Katika usiku ambao umekuwa na movement nyingi za wachezaji na makocha , klabu ya Simba imekamilisha usajili wa beki wa pembeni toka timu ya Mtibwa Sugar, Hassan Kessy.

Beki huyo ambaye ametokea kuwa mmoja kati ya wachezaji wa kutumainiwa kwenye klabu hiyo ya wakata miwa wa huko Manungu Turiani mkoani Morogoro, anaungana na wachezaji wapya waliosajiliwa katika kipindi hiki cha dirisha dogo ambao ni Simon Sserunkuma, Danny Sserunkuma, na Juko Murshid wote kutoka Uganda.
Kessy ambaye ametajwa kuwa moja kati ya wachezaji wanaokaribia kuwa mmoja ya wachezaji wa Timu ya Taifa Stars alichezea Mtibwa kwa mara ya mwisho katika mchezo wa kirafiki ambao ilifungwa na Azam Fc 3-1.
hassan kessy
Beki huyu anasajiliwa baada ya mazungumzo ya muda mrefu yaliyofanyika chini ya usimamizi wa viongozi wa Simba wakiongozwa na Geoffrey Nyange Kaburu na Kiongozi wa Mtibwa, Jamal Bayser.
Tetesi zaidi zinasema kuwa Simba imemsajili beki huyo kwa thamani ya shilingi milioni 30.

Read More »

Maamuzi ya Timu ya Yanga juu ya Mbrazil Emerson…

0 comments
Moja ya vichwa vya habari vilivyokuwa vimepambwa na habari kumhusu Emerson.
Taarifa za usajili na kuachwa wachezaji zinazidi kuingia na safari hii inasemekana kuwa kiungo Mbrazil Emerson amekuwa mhanga wa kwanza wa kuondoka kwa kocha Mbrazil Marcio Maximo baada ya mchezaji huyo kuachwa na Yanga.
Mbrazil huyo anaondoka Yanga baada ya kucheza mechi moja pekee dhidi ya Simba ambako Yanga ilifungwa 2-0.
Emerson alishindwa kuwaridhisha mashabiki wa Yanga ambao wengi walionyesha kukerwa na uwezo mdogo wa kiungo huyo katika dakika 45 alizocheza kwenye mechi dhidi ya Simba.
Emerson alikuja nchini siku chache zilizopita ambapo alipaswa kuziba nafasi iliyoachwa wazi na mshambuliaji Genilson Santos Santana Jaja ambaye hakurudi baada ya kuondoka nchini kufuatia kusimama kwa ligi.
emerson

Read More »

Simba yamsajili beki wa Mtibwa. Ingia Hapa Kwa Habari Kamili

0 comments

hassan kessy

Katika usiku ambao umekuwa na movement nyingi za wachezaji na makocha , klabu ya Simba imekamilisha usajili wa beki wa pembeni toka timu ya Mtibwa Sugar Hassan Kessy .
Beki huyo ambaye ametokea kuwa moja kati ya wachezaji wa kutmainiwa kwenye klabu hiyo ya wakata miwa wa huko Manungu Turiani mkoani Morogoro anaungana na wachezaji wapya waliosajiliwa katika kipindi hiki cha dirisha dogo ambao ni Simon Sserunkuma , Danny Sserunkuma , na Juko Murshid wote toka Uganda .
Kessy ambaye ametajwa kuwa moja kati ya wachezaji wanaokaribia kutiwa kwenye timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars aliicheza Mtibwa kwa mara ya mwisho katika mchezo wa kirafiki ambao ilifungwa na Azam Fc 3-1 .
Beki huyu anasajiliwa baada ya mazungumzo ya muda mrefu yaliyofanyika chini ya usimamizi wa viongozi wa Simba wakiongozwa na Geoffrey Nyange Kaburu na Kiongozi wa Mtibwa Jamal Bayser .
Tetesi zaidi zinasema kuwa Simba imemsajili beki huyo kwa thamani ya shilingi milioni 30 .

Read More »

Breaking News Rasmi…Marcio Maximo aondoka Yanga. Ingia Hapa Kwa Habari Kamili

0 comments


maximo+manji+leo.tif
Habari rasmi toka ndani ya klabu ya Yanga zinasema kuwa kocha Mbrazil Marcio Maximo ameondoka ndani ya klabu hiyo .
Habari hizi zinakuja dakika chache baada ya Maujanjayamjini kuripoti tetesi zinazohusu mustakabali wa kocha huyo Mbrazil.
Maximo anaondoka Yanga baada ya uongozi wa klabu hiyo kukubaliana naye kuvunja mkataba wake baada ya kushindwa kuelewana juu ya jinsi ya kuiendesha klabu hiyo kwenye masuala ya ufundi .
Yanga ilishikilia msimamo wa kumuajiri mkurugenzi wa ufundi ambaye alipangwa kuwa Charles Boniface Mkwasa jambo ambalo Maximo hakukubaliana nalo.
Nafasi ya Maximo sas aitachukuliwa na Mholanzi Hans Van Der Pluijm ambaye aliifundisha timu hiyo kwa nusu msimu baada ya kufukuzwa kwa Mholanzi mwenzie Ernst Brandts .
Tukio hili linaendeleza historia ya Yanga kufukuza makocha baada ya kufungwa na Simba kwenye mechi ya Nani Mtani Jembe baada ya kufukuzwa kwa Ernst Brandts msimu uliopita kufuatia kipigo cha 3-1 mbele ya Simba iliyokuwa inaongozwa na Dravko logarusic.

Read More »

Breaking News , Yanga yamsajili Amisi Tambwe toka Simba. Soma Hapa Kwa Habari Kamili

0 comments



tambwe yanga
Taarifa zilizoingia kwenye mtandao huu dakika chache zilizopita ni kwamba Dar-es-salaam Young Africans imemsajili mshambuliaji wa Simba aliyeachwa Amisi Tambwe .
Yanga imemsajili Tambwe dakika chache zilizopita ambapo anakuja kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Hamis Kiiza ambaye amejiunga na URA ya Uganda .
Tambwe amesajiliwa na Yanga baada ya kuachwa na Simba.
Tambwe amesajiliwa na Yanga baada ya kuachwa na Simba.
Tambwe alikuwa mfungaji bora wa ligi msimu uliopita ambapo alifunga mabao 19 kwenye ligi lakini alishindwa kuwika msimu huu baada ya kutopewa nafasi ya kutosha chini ya Patrick Phiri.
Simba imemuacha Tambwe baada ya kumsajili Danny Serunkuma toka Gor Mahia ya nchini Kenya .
Yanga imekamilisha usjaili huu saa chache kabla ya dirisha dogo la usajili kufungwa kama ilivyopangwa na Tff .

Read More »

HAUSIGELI ALIYEMTESA MTOTO UGANDA AHUKUMIWA MIAKA 4 JELA

0 comments

 Jolly Tumuhirwe (22).

HAUSIGELI aliyenaswa kwenye video akimtesa mtoto nchini Uganda, amehukumiwa kwenda jela miaka minne katika mahakama moja nchini humo.


Jolly Tumuhirwe wakati akimtesa mtoto Arnella mwenye miezi 18.

Mfanyakazi huyo Jolly Tumuhirwe (22) aliiambia mahakama kuwa anajutia kile alichokifanya na anaomba msamaha kwa familia na jamii nzima.
Amehukumiwa kwa kosa la kumtesa mtoto Arnella mwenye miezi 18.

Read More »